Kwamba ndoa yako haina shida lakini hauitaki tu? Huku kwetu huwezi kueleweka, kwa weupe huko ndio ungeweza kueleweka na hiyo sababu yako ingesimama kama sababu toshelevu. Kwamba hakuna tatizo, sitaki tu ndoa na naona sikuwa designed kwa ajili hiyo, i made a mistake na blah blah zingine.
Kuna wengine wanajisikia hivyo, na wanaona wafanye vitimbi ili wapate sababu ya kuacha au kuachwa. 😅 Africa kugumu sana sijui kama tunaweza kuishi bila unafiki.
Swali kwako, Ukitoka humo una uhakika kuwa hautaitaka tena? Tabia ya mwanadamu ni kuchoka/kukinai na kukihitaji kitu tena baada ya muda.