Wakati wa uongozi Profesa Juma, Mahakama ilishindwa kusimama na wananchi dhidi ya udhalimu wa awamu ya 5

Wakati wa uongozi Profesa Juma, Mahakama ilishindwa kusimama na wananchi dhidi ya udhalimu wa awamu ya 5

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Profesa Ibrahim Hamis Juma anastaafu mwaka huu, 2023. Jaji Mkuu alipata mamlaka hayo kipindi cha awamu ya tano, na kimsingi, ilikuwa ni mahala pa yeye kutenda alichohubiri madarasani kwa maisha yake yote ya kitaaluma kuhusu mgawanyo wa madaraka.

Ni wakati wa uongozi wake JPM aliteua Jaji wa Rufani jukwaani bila kufuata utaratibu wa kisheria wa Tume ya Utumishi wa Mahakama. Na Kuna Hakimu aliteuliwa na JPM kuwa Jaji kisa tu kambana mfanyabiashara kule Kahama, na baada ya JPM kumteua, hukumu alizokuwa anaandika ni sawa na wale kuku wenye manyoya yaliyocharuka

Ni wakati wa utawala wake, mahakama ilitumika kama bomba la maji, wale wasiotakiwa na awamu ya tano, harakaharaka walikimbizwa mahakamani, na mahakama ikawa inaimbiwa chorus za upelelezi unaendelalea, na mahakama ikishaambiwa hivyo, inabaki kama nyuki wa mashineni.

Ni kwa mara ya kwanza wakati Prof Juma akiwa Jaji Mkuu, wagombea wote wa uchaguzi 2020 hawakupeleka shauri lolote mahakamani.

Mahakama ilitambulika kama moja ya vifaa vya jiwe alivyotumia kuwaumiza watu ambao hawapendi.

Mpaka Prof Juma anaondoka madarakani mwaka huu, mahakama haijatoa maamuzi mazito yaliyotingisha jamii na tasnia ya sheria, tofauti na enzi ya kina Jaji Nyalali, Sammata na Ramadhani.

Ni mahakama ya Prof Juma ambayo, udhaifu wake, ndio umefanya hata SSH aunde Tume ya Kupitia mfumo wa haki jinai.

Mahakama ya Prof Juma ilikuwa dhaifu sana kuliko mahakama chini ya majaji wakuu wengine.

Ukiacha majengo yanayojengwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia, mahakama ili-fail katika core function zake, utoaji haki. Haki hata itolewe chini ya mti, ndicho anachotaka mwananchi.

Mawakili walikuwa wanakamatwa au kutishiwa kukamatwa kwa sababu tu wanawakilisha wateja wao mahakamani.

Mahakimu walikuwa wanapewa zawadi ya Ujaji kwa kutoa hukumu za kidhalimu, mfano mzuri kesi ya Sugu mbeya.

Kwa ambao hawajui, kulitokea wimbi kubwa la mahakimu kushindana kufanya udhalimu anaoupenda Jiwe, ili Jiwe asikie, awape Ujaji.

Mahakama pia ihakikishe katika mapitio ya mfumo wa haki jinai, na yenyewe iwasilishe hoja zake, hasa zinazohusu waendesha mashtaka. Wanafanya wanavyotaka, na mahakama inaonekana hamna lolote, na kimsingi, wanaonekana Wana nguvu kuliko mahakama. In most cases, wananchi wanaona Bora umuite mwendesha mashtaka, mmalizane, aandike Nolle, au muingine katika plea bargaining, kuliko kusubiri mahakama.

Kwa heri Prof. Juma.
 
Jaji mkuu wa hovyo kuwahi kutokea. Alipojiingiza kwenye suala la Lissu nikamuona kilaza.
Alikaa kwa majaribio akiwa 'kaimu jaji mkuu' kwa miezi kadhaa ndipo akaapishwa Ila huu muhimili ulivurugika kabisa enzi yake. Ila katiba yetu pia ilichangia pakubwa hili.

Namna kesi ya Mbowe ilivyoendeshwa na kutolewa uamuzi ilionyesha mapungufu makubwa kwenye huu muhimili.

Pascal Mayalla zitto junior
 
Huyo Juma, kwa kweli ni aibu tupu. Hana cha kujivunia kwenye hiyo nafasi.

Huyu ndiye aliyeziagiza mahakama kuwa zitoe hukumu kwa kuangalia majukumu na malengo ya Serikali. Alishiriki vikao vya siri na viongozi wa CCM dhidi ya upinzani na dhidi ya Musa Assad, huku kwa unafiki akijifanya ni rafiki yake. Ndiye aliyefanya makubaliano na Jiwe, Assad atolewe kwenye nafasi yake, ndiye alishirikiana na Ndugi kumwomba Jiwe na wao wawe na kinga ya kutoshtakiwa ili wawe huru kutenda chochote hata kilicho kinyume na katiba na sheria za nchi bila ya kuwa na hofu ya kutokuja kushtakiwa.

Aondoke haraka sana.
 
Huyu ndiye aliyeziagiza mahakama kuwa zitoe hukumu kwa kuangalia majukumu na malengo ya Serikali.
Je, unaujua mitandao wa Tanzil?. Unajua maagizo yote ya CJ yanawekwa kule Tanzil?. Sijawahi kuona agizo hilo, kama kweli kuna agizo kama hilo please share!.
Alishiriki vikao vya siri na viongozi wa CCM dhidi ya upinzani na dhidi ya Musa Assad, huku kwa unafiki akijifanya ni rafiki yake. Ndiye aliyefanya makubaliano na Jiwe, Assad atolewe kwenye nafasi yake, ndiye alishirikiana na Ndugi kumwomba Jiwe na wao wawe na kinga ya kutoshtakiwa ili wawe huru kutenda chochote hata kilicho kinyume na katiba na sheria za nchi bila ya kuwa na hofu ya kutokuja kushtakiwa.
I don't believe this!, thibitisha!.
Aondoke haraka sana.
Aende wapi wakati his time is up?.
NB. Leo ni siku ya sheria, tumfuatilie atazumgumza kutokea Dodoma, Mgeni rasmi ni Samia

P
 
Huyo Juma, kwa kweli ni aibu tupu. Hana cha kujivunia kwenye hiyo nafasi.

Huyu ndiye aliyeziagiza mahakama kuwa zitoe hukumu kwa kuangalia majukumu na malengo ya Serikali. Alishiriki vikao vya siri na viongozi wa CCM dhidi ya upinzani na dhidi ya Musa Assad, huku kwa unafiki akijifanya ni rafiki yake. Ndiye aliyefanya makubaliano na Jiwe, Assad atolewe kwenye nafasi yake, ndiye alishirikiana na Ndugi kumwomba Jiwe na wao wawe na kinga ya kutoshtakiwa ili wawe huru kutenda chochote hata kilicho kinyume na katiba na sheria za nchi bila ya kuwa na hofu ya kutokuja kushtakiwa.

Aondoke haraka sana.
Duuh
 
Duuh yaani hizi post za kuteuliwa kama mkipata kiongozi mwenye roho mbaya basi Nchi inaugua.
 
Back
Top Bottom