Wakati Watanzania tukiendelea 'Kulewa' na Hotuba ya 'Kumkaanga' Ndugai, tujue Magufuli Umeme ni Tsh 27,000/ na Samia ni Tsh 320,000/

Navyojua bei ya 27,000(mijini) ilitangazwa na Kalemani kipindi hiki hiki cha Mama.
 
Wewe jamaa huwa una akili sana ila kosa lako ni moja kukosea kuchagua makolo.
 
vitu viandikwe kwa Evidence na si bla blaa watu tangu kipindi cha magufuli hatukuwahi kusikia unaunganushiwa umeme kwa 27,000 au wewe ulikuwa na connection zako za vishoka kuhujumu shirika.
 
Huo umeme ni wa rea kama kuna mtu wa mjini alieunganishiwa kwa hio bei tajwa ni wachache ilikua ukilipa bla bla ni nyingi mpka utoe ka hongo au kuna koneksheni ndo mambo yanakua mujarabu

Watu wengi mijini waliunganishiwa umeme kwa 27000, hata kama kulikuwa na ucheleweshaji kwa baadhi ya maeneo. Na sio kweli kwamba ukilipa 320000 ndio longo longo zitaisha. Kabla ya Magufuli watu walilipa hadi milioni+ na bado ilibidi watoe rushwa tena ili kupata haki yao ya kuunganishiwa umeme.
 
Wanasubiri 2025 waanze kutumia hotuba za Magufuli kama rejea yakuombea kura.
 
Wewe ni popoma kama popoma wengine.Umeme wa REA bei ni 27,000 na Umeme wa Mjini bei ni hiyo toka enzi ya huyo Bwanako Mwendazake hadi sasa.

Ushahidi huu hapa👇

 
Kama ni hivyo kwanini usiunganishiwe tu bure na umeme usiwe unalipa maana hata mabwawa ya kuzalisha umeme ni mali ya Tanesco.
 
Usiseme nchi hii bado sana bali usema Arista bado sana. Magufuli kahubiri dili za tanesco miaka 5 lakini bado unauliza ulegelege wa tanesco, aisee wewe bado sana.
 
Nguzo na mitre uletewe kwa elf 27000 kweli?
Hizo nguzo na mita ni mali ya nani ?

Ni sawasawa useme nyumba kweli ukae kwa elfu 50 kwa mwezi wakati nimejenga kwa mamilioni (unasahau kwamba hio nyumba ni yako na huyo mkazi unampa huduma ya malazi to infinity yaani unakula hizo elfu 50, 50 hata kupelekea wewe kuongeza nyumba ya pili na tatu)

27K kitu gani hawashindwi hata kuunganisha watu bure...., ili waweze kulipia hio service
 
27,000 ilikua kwenye makaratasi, lipa iyo ufungiwi umeme ng'o
utapiga benchi mpaka bwana mkubwa arudi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…