Wakazi: Diamond Platnumz ni maarufu ila hajui kuimba, "ukweli unauma mpaka mnanipigia simu za vitisho"

Wakazi: Diamond Platnumz ni maarufu ila hajui kuimba, "ukweli unauma mpaka mnanipigia simu za vitisho"

Wakazi yuko sahihi Diamond hata atoe ngoma ya dakika mbili halafu humo ndani awe anacheka mwanzo mwisho utaona ngoma hiyo itavyokuwa trend na usikute ikapewa na tuzo

Hayo yote yamerahisishwa kutokana na jina (umaarufu) na ndio maana hata hawa ma underground wana amini wakipata nafasi ya kufanya kazi kwenye lebel yao watatoka tu, kwasababu kitachowafanya wajulikane sio ubora wa kile wanachokiimba

Means hata kwa level zao za huku chini wanaamini hata wakaze msuli namna gani bado ubora wa nyimbo hautakuwa kigezo wao kutoka

Nakubaliana na Wakazi
Watanzania si ninyi mmeupenda sana ule wimbo wa jamaa anapiga chafya(ama chuu chuu) mpaka mkamuita aje awapigie chafya hapa bongo??
 
Sisi tunataka kujua huo umaarufu kaupata wapi ikiwa hajui chochote kwenye kuimba, kama mnavyodai?

Hao wanaojua kuimba ni nani na nani? Watajeni hapa kisha mtueleze kwanini wao sio maarufu kama Diamond.

Kuwa mwanamziki sio kujua kuimba tu, ukiachana na kuimba Mond kawazidi wengine vitu vingi sana kuhusu mziki.

Kuhusu wakazi, ni moja kati ya wasanii ambao wamedumu kuwa ma-underground kwa miaka mingi sana.
Kwamba msela amedumu kwenye u-underground kwa mda mrefu sana Hahahaa.
 
Hip hop imemshinda sasa anataka uanaalakati anazani atateuliwa km niki wa pili
Uteuzi na uwanaharakati hauwez na hatopata sabubalishakosea chama
Moja yan sababu inayosababisha watanzania tubaki maskini ninkitendo cha kutokueshimu na kukubali

Leo unakuta mtu km mbunge msukuma anamponda mbunge profesa muhongo wakat hao watu hawafanai wala hawaendani na mtu km profesa muhongo kujibixana na msukuma ni kupoteza mda
Ila ndo watanzania tunataka alieko juu tumshushe kwa njia yyte
Wakazi huwezi kumfananisha na nikki wa pili

Niki wapili alikiwa ni chawa, mlamba miguu, asskisser aliyepitiliza mpaka akapewa huo u DC

Tena umenikumbusha kati ya wasanii ambao nimekuwa nawaongelea negative basi hapa mtaiona nafuu ya diamond katika kuwakosoa wasanii

Kipindi cha magufuli ambapo tweeter ilipigwa ban, na kufanya access iwezekane kwa vpn tu, huyu jamaa alijitokeza na ku tweet kuwa watu wanaizushia serikali uwongo kwani yeye ameweza kuingia tweeter bila vpn na kwenda mbali kuwa watu wanafanya hivyo kumchafua magufuli tu

Baada ya hapo zikaja gharama kubwa za mabando, jamaa akasimamia ukucha kuwa wananchi wasilie lie kuhusu bando kwanj sio kitu necessary kama kula, ni jambo linaweza kuepukika tu kuliko kuisumbua serikali kuhusu kupunguziwa gharama za bando

Haya akaja tena kwenye tozo akaongea ujinga kibao just kuwa upande wa serikali

Sio huyo tu, hadi masanja naye ni wa type hiyo hiyo na anasemwa sana.

Lakini utofauti unavyokuja tukiwasema hawa hatutajwi kama watu wenye wivu wa mafanikio ya hao watu au haters kwasababu nikki wapili hajaweza kuwa na mashabiki wengi wakumtetea kama ilivyo kwa diamond na alikiba kila platfom kuna utimu

Kwa hiyo nasisitiza kuwa diamond kwenye ywezo wa kuimba bado sana, labda kama utanifananishia yule diamond wa "utanipenda" lakini huku kwa nyegezi ni ujinga na aibu kukubaliana na hoja hiyo kuwa mwana anaimba vizuri
 
Huu ndo ujinga wa watu wengi sana kufikiria mtu akisemwa negative itatokana na watu kuwa na wivu na mali zake, ni UJINGA
Tena ujinga haswaaaa.
Wakazi sio wa kwanza kumponda Diamond, producers Majani na Master J walishasema kwamba jamaa hawezi kumba ingawa ana umaarufu. Pitieni youtube msikilize maoni ya producers. Achaneni na wakazi
 
Ninachokijua figo za Mond zikifeli kama za mbunge mstaafu hayslazimika kupitisha bakuli
 
Tena ujinga haswaaaa.
Wakazi sio wa kwanza kumponda Diamond, producers Majani na Master J walishasema kwamba jamaa hawezi kumba ingawa ana umaarufu. Pitieni youtube msikilize maoni ya producers. Achaneni na wakazi
Ni msanii mwenye maneno ya shombo sana kwa wasanii wengine huwa nashangazwa na watu wanaotaka unapomuongelea msela uwe politely wakati ye anatapika

Leo nimekutana na clip hii, sijajua jamaa aliongea kama utani wa kimuziki lakini body language inapingana kabisa na dhana ya utani
 
Ni msanii mwenye maneno ya shombo sana kwa wasanii wengine huwa nashangazwa na watu wanaotaka unapomuongelea msela uwe politely wakati ye anatapika

Leo nimekutana na clip hii, sijajua jamaa aliongea kama utani wa kimuziki lakini body language inapingana kabisa na dhana ya utani
View attachment 2152982
Infact umeandika facts. Chibu ana shombo mno. Labda kwa sababu katokea uswazi. Sio kosa lake
 
Sasa mkuu wewe unamuonaje Wakazi??

Haina ubishi kuwa ni Legend kwenye group la ma-underground, kuna watu mpaka leo ukisema Wakazi hawamjui.
Yes inategemeana na huyo mtu yuko interested na aina gani ya mziki

Mi mwenyewe naskiaga zuchu zuchu lakini sijawahi muona kumjua, na probably nilimuona ila sikujua kuwa ndio yeye

Hayo yote yanawezekana kama huna interest na type hiyo ya burudani
 
Msanii kutoka Tanzania, Wakazi amesema kwamba Diamond Platinumz ni maarufu ila sio mzuri katika uiambaji.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Twitter, Wakazi alisema kwamba kuna tofauti kubwa kati ya umaarufu na ubora wa msanii, na hivyo kuwa maarufu haimaanishi kuwa mzuri katika sanaa ya muziki.
Wakazi ana nini na bwana Naseeb.
Ni ukweli lakini kila mtu apambane na mziki wake
 
Wakazi ana nini na bwana Naseeb.
Ni ukweli lakini kila mtu apambane na mziki wake
Wakazi amesema hana tatizo lolote yeye anaongea kama mchambuzi mwenye uzoefu wa masuala ya muziki
 
Wakazi amesema hana tatizo lolote yeye anaongea kama mchambuzi mwenye uzoefu wa masuala ya muziki
Unajua ni sawa wewe uende kumshauri Bakhresa kuhusu biashara wakati biashara unayofanya haijafanikiwa kama yake. Utaonekana snitch tu ukianza oh, unajua bwana Bakhresa unafanya biashara kienyeji sana japo umefanikiwa 🤣
 
Diamond ana maneno ya shombo,dharau.Diamond sio msanii anayejua kuimba kuliko wasanii wote Tanzania.Lakini yeye kabla hakuwa maarufu alikuwa ni mtu wa hali ya chini sana,hakuna njia yoyote ambayo ingemfanya awe na huu umaarufu chanya bila kufanya kitu kizuri.maana yake kuna wakati alikuwa anaimba vizuri ikamfikisha alipo na hata alipoamua kubadilika tayari alishaprove ambavyo alitakiwa aprove ndio maana akawa na die hard fans mpaka leo.

Halafu sidhani kama kuna sababu ya wakazi kusema hayo aliyosema,labda awe na chochote dhidi ya diamond.vyovyote iwavyo mi nadhani kiujumla diamond amewazidi wasanii wenzake wa bongo fleva mbali,huo ni ukweli ulio wazi ambao bahati mbaya utadhihirika tu kama jamaa atatangulia mbele za haki hivi sasa.
 
Diamond ana maneno ya shombo,dharau.Diamond sio msanii anayejua kuimba kuliko wasanii wote Tanzania.Lakini yeye kabla hakuwa maarufu alikuwa ni mtu wa hali ya chini sana,hakuna njia yoyote ambayo ingemfanya awe na huu umaarufu chanya bila kufanya kitu kizuri.maana yake kuna wakati alikuwa anaimba vizuri ikamfikisha alipo na hata alipoamua kubadilika tayari alishaprove ambavyo alitakiwa aprove ndio maana akawa na die hard fans mpaka leo.
Halafu sidhani kama kuna sababu ya wakazi kusema hayo aliyosema,labda awe na chochote dhidi ya diamond.vyovyote iwavyo mi nadhani kiujumla diamond amewazidi wasanii wenzake wa bongo fleva mbali,huo ni ukweli ulio wazi ambao bahati mbaya utadhihirika tu kama jamaa atatangulia mbele za haki hivi sasa.
Use someone's fame to be famous

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Sasa hapo wivu una husika vipi?

Kumkosoa mtu hakuwezi kuwa na maana ya wivu

Labda nikukumbushe tu kuwa hata huyo diamond kafanya interviews kibao ambapo humo kawakebehi watu na kuwashusha viwango, je na hiyo unaihesabu kama wivu?

Tukubaliane hapa, kwamba diamond naye ana wivu kwa wasanii wengine kwa kauli zake za kuwakosoa wengine kwenye interviews

Vinginevyo wewe utakuwa ni mnafki usiekuwa muungwana, na ni mtu ambaye unafata meza yenye bia nyingi kwasababu ya utimu.
Ni wivu tu. huyo Wakazi apambane kutengeneza brand yake sio kuishusha ya mwenzie. hapa mtaani ukiuliza watu watatu kwa ghafla kuhusu Wakazi watakujibu hawamjui.
 
Ukiwa critical thinker kwenye jamii ya watu wenye upeo mdogo kama kitenes unakua unaonekana wewe ndio mwehu
Wakaz yuko sahihi kabisa ila watu wamepofushwa na mahaba
Mkuu unamaanisha vile tunaona ma professor wetu akili hawana vile wanafanya maamuzi ya kiwaki kumbe sisi ndo hatuna akili?
 
Back
Top Bottom