Wake wa Marais wetu na Mambo yao

Wake wa Marais wetu na Mambo yao

kufanya kitu kizuri anaweza kuwa kafanya, hatukatai but tumeambiwa ni MWIZI...sasa sijui mtamtetea kwa lipi?

Lakini kama Zambi anafikiri hivyo kwanini asiweke ushahidi Hadharani kuonyesha kwamba kweli kapevuka kwenye hoja na anaweza kutetea hoja zake, kwa ninavyojua mpk sasa Mama Anna na Mzee Mkapa wapo Safii tena sanaaaaaaaaaa.
 
..nani aliwashikia bunduki hao Waalimu ili wakakope kwa Mama Mkapa?

..nilitegemea hiyo benki inayotoza riba 200% ingekufa mara moja kwa kukosa wateja.

...njaa jamani,hata mimi ningekuwa wao ninge sign tuu hata kama ni 1000%
 
...njaa jamani,hata mimi ningekuwa wao ninge sign tuu hata kama ni 1000%

Go sell your soul to the devil huna jipya wewe.Njaa ndio ikufanye ufanye maamuzi ya kijinga and so costfull?
 
Swali la kwanza la kuwauliza ni hili...

Wataje ni vigezo gani walivyovitumia wakati wa credit evaluation.

The higher the risk...The higher the interest rate.

Kwa mfano uhakika wa kazi, madeni mengine, mwajiri wako nk.

Kimtizamo..Hapo kama ni walimu....Basi riba yao ilitakiwa kuwa ndogo sana kwani kazi wanayo ya uwalimu na wengineo wameajiriwa na serikali yenyewe.

Na ama mashule hayo hayo yanayomilikwa na mafisadi.

Inawezekana walitumia kigezo cha ucheleweshwaji wa mishahara ya walimu kama kigezo cha kuwa charge interest rate kubwa ambayo inaonyesha kupita kiasi.

Hapo kama walifanya hivyo...Bado ni UNYANYASAJI WA WALIMU!
Na Tanzania msipoichukuwa nchi MMEKWISHA!

Hivyo kwa kuanzia...Tunaomba vigezo vya credit vilivyowekwa wakati wa kudetermine interest rate ya mikopo yao hiyo.

HILI NI MUHIMU....Pia Kama kulikuwa na collateral nk.
 
Sishangai sana pia kwamba riba ni 200%, unajua bongo hawa wafanya biashara ya pesa wanatuumiza sana walala hoi! Wanaujanja wa kueleza figure zao wakificha makato halisi unayo garamia mkopaji ama mteja.

Nilishangaa pia jamaa yangu alichukua mkopo CRDB akaambiwa riba ni 15%, so akachukua 12mil kwa five yrs, ila alipo kuja piga mahesabu alijikuta analipa over 17 mil. ambayo ni 47% na si 15%, yaani kuna hesabu fulani zinapigwa hapo, huenda hata huyo mama wanachukua kwa riba ya 60% wakija changanua labda kwa miaka 3-5 wanajikuta wanalipa hiyo 200%

Amabacho sielewi, hivi BOT I mean mfumo wa banki nchini hauwezi kuwa regulated kiasi kwamba riba zikashuka kama nchi za wenzetu?

Riba kama ni mkopo wa biashara...Inategemea na Business plan yako mara baada ya mambo kama feasibility study pamoja na assets zako ulizonazo kuwasilishwa hapo benki na kufanyiwa tathmini.

Kwahiyo unapokwenda kuchukuwa mkopo musome kwanza terms and condition kabla ya kusaini na si kwasabau ni milioni 12 basi watu wanakurupuka.

Halafu pia kuwe na utaratibu kuwa kama ukiweza kulipa deni lako kwa kutowa pesa nyingi zaidi za zile za makubaliano kila mwezi ama mwaka nk..Basi unakuwa na uwezo wa kulipa principle kwa muda mfupi na wakati huo huo kuanza kulipa interest!

Kwa hiyo muda ni kitu cha muhimu hapo kwenye ulipaji wa mkopo.

Muda na kiasi unacholipa..Ukilipa zaidi ni vizuri.

Nasikia kuna wengine wanachukuwa mikopo ya biashara wananunua tu vitu vingine vya tofauti.

Ni muhimu kuwa na Business plan iliyotulia.

Biashara ni kama imani na hivyo ni lazima uwe na imani na unachokwenda kufanya na pia confidence na kujuwa haki zako.
 
Naomba mniambie kuna sababu ya kuendela kuaamini na kuwaachia wachaga waendele kuwepo serikalini?
 
Sishangai sana pia kwamba riba ni 200%, unajua bongo hawa wafanya biashara ya pesa wanatuumiza sana walala hoi! Wanaujanja wa kueleza figure zao wakificha makato halisi unayo garamia mkopaji ama mteja.

Nilishangaa pia jamaa yangu alichukua mkopo CRDB akaambiwa riba ni 15%, so akachukua 12mil kwa five yrs, ila alipo kuja piga mahesabu alijikuta analipa over 17 mil. ambayo ni 47% na si 15%, yaani kuna hesabu fulani zinapigwa hapo, huenda hata huyo mama wanachukua kwa riba ya 60% wakija changanua labda kwa miaka 3-5 wanajikuta wanalipa hiyo 200%

Amabacho sielewi, hivi BOT I mean mfumo wa banki nchini hauwezi kuwa regulated kiasi kwamba riba zikashuka kama nchi za wenzetu?

Kuna hesabu rahisi sana
zinaitwa 1. Simple interest 2.compound interest

Kama ikitokea kua umezisahau basi mimi nipo nitakuelewesha kadili niwezavyo.
 
Naomba mniambie kuna sababu ya kuendela kuaamini na kuwaachia wachaga waendele kuwepo serikalini?

Hilo ndiyo jibu lako kuhusiana na swali langu la msingi kuhusu credit evaluation methods za hao wakopeshaji?
 
1.Simple interest.
Tuseme wewe umekopa Tsh 1000/= na riba yake ni 10% mda wa miaka mnne
itakua hivi.
faida/interest = Kianzio*mda*riba = 1000*0.1*4 = 400

faida +kianzio ulichokopa = 400+1000= 1400 ndio utakayotakiwa kulipa.

2.compound interest
Tuseme wewe umekopa Tsh 1000/= na riba yake ni 10% mda wa miaka mnne
itakua hivi.Kila mwaka kianzio kinakua .

mwaka wa kwanza
faida/interest = kianzio*mda*kima =1000*0.1*1 = 100
hivyo baada ya mwaka wa kwanza jumla kitakua 1000+100=1100/=

Mwaka wa pili.
Kianzio ni jumla ya faida tuliyopata na kianzio hivyo
faida/interest = kianzio*mda*kima = 1100*0.1*1 =110
jumla = 1100+110=1210

mwaka wa tatu
kianzio= 1210
faida =1210*0.1*1= 121
jumla 121+1210=1331/=

mwaka wa nne
kianzio ni 1331
faida = 1331*0.1*1 = 133.1
jumla =1331+133.1= 1464.1\=
hii ndio utatakiwa kulipa Tsh 1464.1 kama unatumia compound interest
 
1.Simple interest.
Tuseme wewe umekopa Tsh 1000/= na riba yake ni 10% mda wa miaka mnne
itakua hivi.
faida/interest = Kianzio*mda*riba = 1000*0.1*4 = 400

faida +kianzio ulichokopa = 400+1000= 1400 ndio utakayotakiwa kulipa.

2.compound interest
Tuseme wewe umekopa Tsh 1000/= na riba yake ni 10% mda wa miaka mnne
itakua hivi.Kila mwaka kianzio kinakua .

mwaka wa kwanza
faida/interest = kianzio*mda*kima =1000*0.1*1 = 100
hivyo baada ya mwaka wa kwanza jumla kitakua 1000+100=1100/=

Mwaka wa pili.
Kianzio ni jumla ya faida tuliyopata na kianzio hivyo
faida/interest = kianzio*mda*kima = 1100*0.1*1 =110
jumla = 1100+110=1210

mwaka wa tatu
kianzio= 1210
faida =1210*0.1*1= 121
jumla 121+1210=1331/=

mwaka wa nne
kianzio ni 1331
faida = 1331*0.1*1 = 133.1
jumla =1331+133.1= 1464.1\=
hii ndio utatakiwa kulipa Tsh 1464.1 kama unatumia compound interest

Acha siasa...Nataka uweke vigezo za credit evaluation kwasababu hivyo ndivyo vyenye kudetermine kiwango chako cha interest rate.

Acha kuturudisha nyuma kwa kutupa definitions za compound na simple inerest rate.

Tunataka vigezo kwasababu kwa uelewa wangu...Hata hao walimu wenyewe wasingepewa hiyo mikopo kama wasingekuwa walimu.

Kwa mantiki hiyo basi..Tunaomba vigezo vilivyotumika kwani ni lazima haiwezi kuwa tu flat rate kwa kila mtu!

Wanaweza kutangaza rate ya chini na wewe kwenda huko na kujikuta unachajiwa kiwango cha juu.

Sasa hapo ni lazima muwaulize hiyo benki.

Kwa upande wa walimu...Wanaweza kutusaidia kutueleza kama ni documents gani na ama informations gani walizotakiwa kuzipeleka benki kabla hawajakubaliwa kupewa mikopo na kabla hawajaambiwa kuwa wameangukia kwenye group gani la interest rate.

Wananchi wasinyanyaswe kabisa na kunyonywa hivi!

Kwani tunajuwa kuwa si kila mtu anaweza tu kwenda benki na kukopa...Anaweza kwenda kujaribu lakini kuna vigezo vilivyowekwa kabla hawajatoa mkopo huo.

Tunataka vigezo hivyo vilivyotumika kwa walimu hao.
 
jamani hili swala ajibu mzindakaya mwanafamilia wa mr clean!!!!!

mama mkapa mbona ameiba vidogo jamani hao wa epa mbona hamsemi na yeye si binadamu na anatamani mbona mawaziri wengi tu wameiba na wengine wanaua vijana wetu pale magomeni na sinza kwa pesa nyingi tu haramu na kuna nyumba zinajulikana zinatengenneza mizigo kusafirisha nje!!!!wangapi hawawajui wale vijana pale airport wanaosindikiza wauza unga mpaka mlangoni na kuwapokea mpaka kwenye gari!!!!hizi story nimeahakikishiwa na mmoja wa mdogo wangu yuko usalama alikuwa pale wamempeleka moja ya mashirika ya umma ....

mwacheni alichoona kuchukua nae achekue jamani/!!!!!salimu bado uko dar ????????
Mr Impossible
kuiba ni kuiba tu tusiweke madaraja hasa kipindi hiki ambacho tunataka kila aliye/anayeiba ajisafishe na arudishe kile alichoiba. Tuwajadili wezi wote na kuwahadaa hadharani mpaka waone ubaya wa kuiba mali za umma
 
Kuna hesabu rahisi sana
zinaitwa 1. Simple interest 2.compound interest

Kama ikitokea kua umezisahau basi mimi nipo nitakuelewesha kadili niwezavyo.

Hizo hesabu zinafuatia mara baada ya credit evaluation in order to determine credit worthyness of the customer.
 
Mbunge adai Mke wa Rais Mstaafu Tanzania anawaibia walimu
Na Muhibu Said, Dodoma
Mwananchi

WAKATI tuhuma dhidi ya Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na mkewe Anna, kwamba walijihusisha na biashara wakiwa Ikulu zikiwa hazijatolewa maelezo ya kina hadi leo, Anna anakabiliwa na tuhuma mpya kwamba amekuwa akishiriki katika mikataba ya kilaghai ya kuwaibia walimu.

Tuhuma hizi mpya dhidi ya Anna zimetolewa na Mbunge wa Mbozi Mashariki (CCM), Godfrey Zambi, wakati wa majadala wa kupitisha makadirio ya matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 bungeni juzi jioni.

Pamoja na Anna, pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Ibrahim Kaduma, naye aliingizwa kwenye tuhuma hizo wakidaiwa kuwaibia walimu mamilioni ya shilingi kupitia kampuni yao ya kutoa mikopo.

Mbunge huyo alidai kuwa Kampuni ya Bayport Financial Services, ambayo inajishughulisha na utoaji wa mikopo kwa watumishi wa umma, inamilikiwa na Anna na baadhi ya vigogo wastaafu serikalini, akiwamo Kaduma, imekuwa ikiwakopesha walimu Sh1milioni, huku ikiwataka walipe Sh3milioni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kampuni ya Bayport inamilikiwa na mke wa Rais Mstaafu, Anna Mkapa. Lakini wapo wengine wazito walioitumikia nchi hii, kama Kaduma. Mwalimu akikopa Sh1milioni analipa Sh3milioni. Hii imetoka wapi kama si wizi??alihoji Zambi bila kueleza muda wa ulipaji wa mkopo ulitolewa na kampuni hiyo.

Akijibu hoja hiyo ya Zambi, Waziri Profesa Jumanne Maghembe, alisema kiwango cha ulipaji mkopo kinategemea muda wa kulipa, kauli ambayo ilisababisha karibu ukumbi mzima wa Bunge kuzomea, kuashiria kwamba wabunge hawajaridhishwa na majibu hayo.

Hata hivyo, Waziri Maghembe alijibu tuhuma hizo akisema: "Kama mkopo huo ni wa muda mfupi, hiyo riba ni kubwa. Hata hivyo, nawaahidi kwamba suala hilo tutalifuatilia ili kupata ukweli wake."

Pia Waziri Magheme alitoa hadhari kwa walimu kuwa makini wanapoingia katika mikataba mbalimbali hasa ya kukopa.

Baada ya Bunge kuahisishwa, mwandishi wa Mwananchi alimuomba Zambi ampe ufafanuzi juu ya mikopo hiyo na muda wa kurejesha.

Alidai kwamba, kwa mujibu wa nyaraka alizonazo, mkopo huo unatakiwa ulipwe katika kipindi cha miaka mitatu, ambayo ni sawa na asilimia 67 ya riba inayotozwa kwa mwaka na alidai kuwa kampuni hiyo haijaweka bayana riba ambayo mkopaji anatakiwa atozwe.

Mbunge huyo alidai kuwa kiasi hicho cha fedha, ambacho kinatakiwa kilipwe, ni zaidi ya asilimia 200 ya malipo na riba inayotozwa kutokana na mkopo huo.

Alidai kuwa kwa mujibu wa nyaraka hizo, kampuni hiyo ilipewa kibali cha kuendesha shughuli zake na Ikulu, lakini ndani ya kibali hicho ambacho ndani yake kuna maelezo yanayeosema kuwa lolote litakalotokea katika biashara hiyo, litamalizwa na kampuni na mteja wake.

"Kampuni hiyo inakopesha watumishi wa umma. Walioingia kwenye mtego huo ni walimu. Na walimu ndio walionipa taarifa hizo. Hivi sasa huko Mbeya kuna crisis (mgogoro) kubwa," alisema Zambi.

Tuhuma hizo zimetolewa na Zambi siku chache baada ya asilimia kubwa ya wabunge kuibana serikali kuitaka iboreshe kipato cha walimu kinachotokana na mishahara yao.

Mwananchi jana ilifika katika ofisi za Bayport kwa nia ya kupata ufafanuzi juu ya tuhuma zilizoelekezwa kwake na mbunge huyo, hata hivyo mwandishi wetu baada ya kusubiri kwa saa kadhaa kwenye ofisi hizo jengo la Water Front jijini Dar es Saam, alipewa mihadi ya kukutana na msemaji wa kampuni hiyo leo.

Tuhuma hizi mpya dhidi ya Mama Mkapa zinatolewa huku kukiwa na mlolongo mrefu wa tuhuma dhidi yake, zikiwamo za kufungua kampuni ya ANBEM yeye na mumewe, Rais Mkapa wakiwa Ikulu na kujihusisha na biashara.

Akiwa kijijini kwake Lupaso, Mtwara, Rais Mkapa aliwataka wananchi kupuuza tuhuma zinazotolewa dhidi yake kwa madia kwamba ni za uongo. Hakufafanua ni tuhuma ipi ni ya uongo na ipi ni ya kweli.
 
Kwakweli kama si kinga ya Bunge nadhani Mheshimiwa na kaka yangu God Zambi angeliingia matatani, maana utafiti unaonyesha wazi kuwa si kweli kuwa waalimu hawa wanakopeshwa 1million halafu wanalipa 3million.

Waliompa haya malalamiko wamempotosha kaka Zambi aidha kwa makusudi au na yeye ameamua kusaka pa kutokea ktk siasa za sasa.

Kuna habari kuwa hiyo taasisi itazijibu tuhuma hizo na kwa hakika kama si bunge Zambi kaka yangu angejikuta yuko mahakamani maana language aliyoitumia jana kwa sisi tuliomsikiliza haikuwa na huruma hata kidogo kwa watuhumiwa na ni imani yangu malipizi yake ktk mahakama yangelifanana na kukosekana kwa huruma dhidi ya Zambi.

Otherwise tusubiri tuone na wao watasemaje maana hili linazungumzika kiurahisi na hapo ndipo mwanya utapatikana.

Well said FDR (Jr).

Ingawa sipendi kabisa kuona mtu akijitajirisha kupitia migogo ya walio anyonge zaidi yake, ni vema tukasubiri tuone huyo Zambi atatoa evidence gani ili ku-substantiate hizi allegations kuhusa Anna Mkapa na huyo Prof. wa Mzumbe, Bw. Ibrahim Kaduma kabla ya kumhukumu/kumchafulia mama wa watu jina kuwa ni fisadi. Binafsi nina serious doubts kuhusu tuhuma hizi.

Nasema hivyo kwasababu kama hii kampuni imesajiliwa kihalari, inalipa kodi na kufuata sheria zote zilozowekwa mbele, basi suala la riba ya juu hilo sio tatizo. Kuna nchi nyingi tu watu wanalipa riba mpaka asilimia 300 (monthly), sembuse asilimia 67 kwa mwaka? After all, hao wakopaji hawawekewi mtutu wa bunduki mgongoni na kuamuriwa, "haya kopa kiasi hiki!"--No, wanakwenda wenyewe kwa hiari yao wakijua kuwa watalipa riba hiyo (67%) iliyopangwa.

Ninachokiona hapa ni excitment ndani ya wabunge wa CCM wakitaka kusema anything (hata kama ushahidi ni zero) ili waonekane kuwa wao ndio haswa watetezi wa kweli wa wanyonge.

So having said that, kama ni kweli kuwa kampuni hii inayaotajwa hapa(I think nimesoma IPP--inaitwa 'Bayport'), ime-violate mambo fulani fulani, then I'm pretty sure sheria itafuata mkondo wake.
 
Acha siasa...Nataka uweke vigezo za credit evaluation kwasababu hivyo ndivyo vyenye kudetermine kiwango chako cha interest rate.

Acha kuturudisha nyuma kwa kutupa definitions za compound na simple inerest rate.

Tunataka vigezo kwasababu kwa uelewa wangu...Hata hao walimu wenyewe wasingepewa hiyo mikopo kama wasingekuwa walimu.

Kwa mantiki hiyo basi..Tunaomba vigezo vilivyotumika kwani ni lazima haiwezi kuwa tu flat rate kwa kila mtu!

Wanaweza kutangaza rate ya chini na wewe kwenda huko na kujikuta unachajiwa kiwango cha juu.

Sasa hapo ni lazima muwaulize hiyo benki.

Kwa upande wa walimu...Wanaweza kutusaidia kutueleza kama ni documents gani na ama informations gani walizotakiwa kuzipeleka benki kabla hawajakubaliwa kupewa mikopo na kabla hawajaambiwa kuwa wameangukia kwenye group gani la interest rate.

Wananchi wasinyanyaswe kabisa na kunyonywa hivi!

Kwani tunajuwa kuwa si kila mtu anaweza tu kwenda benki na kukopa...Anaweza kwenda kujaribu lakini kuna vigezo vilivyowekwa kabla hawajatoa mkopo huo.

Tunataka vigezo hivyo vilivyotumika kwa walimu hao.

Mimi sio mwana uchumi wala mwa siasa
Tatizo wewe unataka kucomplicate ishu sijui kwa vile umesoma uchumi ,Hata hivyo ma Engineer nao namba wanazipata .

Bank nyingi zinatumia compound interest wala usitake kuleta siasa
unaweza kopa sh 10/= na ukasema nitazilipa baada ya miaka 500 na ukija kukamirisha hilo deni la sh 10 baada ya miaka 500 utajikuta umelipa bilions of shillings.
Na ukipiga mahesabu yako ya simple simple + siasa utakuta riba ilikua 50000%.
 
Mimi sio mwana uchumi wala mwa siasa
Tatizo wewe unataka kucomplicate ishu sijui kwa vile umesoma uchumi ,Hata hivyo ma Engineer nao namba wanazipata .

Bank nyingi zinatumia compound interest wala usitake kuleta siasa
unaweza kopa sh 10/= na ukasema nitazilipa baada ya miaka 500 na ukija kukamirisha hilo deni la sh 10 baada ya miaka 500 utajikuta umelipa bilions of shillings.
Na ukipiga mahesabu yako ya simple simple + siasa utakuta riba ilikua 50000%.

Vigezo vipo depending na mikopo hiyo.

Kama ni wa kilimo vigezo ni tofauti..Kama business nk.

Na kama ni vigezo vya walimu hao..Basi kilichotumika ni kazi..Kama jinsi ripoti hiyo inapoweka wazi kuwa ni ya wafanyakazi wa mashirika ya umma.

Kwa hiyo rate yao imekuwa kubwa lazima kwasababu ya mishahara yao kucheleweshwa ma kutolipwa na hivyo kuifanya risk kuwa juu na hence higher interest rate.

Kwa hiyo kama serikali hiyo hiyo inawacheweleshea mishahara walimu...Halafu inawapa mikopo ya riba kubwa kwa kigezo hicho hicho cha kutokuwa na uhakika wa cheki zao mwisho wa mwezi si UNYOYAJI HUO?

Ni lini wameshawahi kuwajali walimu?

KAMA WALIMU WANGELIPWA INAVYOTAKIWA WANGEENDA KUKOPA MILIONI YA NINI?

Serikali haiwajali walimu na walimu shirikini kwenye madai ya UHURU!
 
Vigezo vipo depending na mikopo hiyo.

Kama ni wa kilimo vigezo ni tofauti..Kama business nk.

Na kama ni vigezo vya walimu hao..Basi kilichotumika ni kazi..Kama jinsi ripoti hiyo inapoweka wazi kuwa ni ya wafanyakazi wa mashirika ya umma.

Kwa hiyo rate yao imekuwa kubwa lazima kwasababu ya mishahara yao kucheleweshwa ma kutolipwa na hivyo kuifanya risk kuwa juu na hence higher interest rate.

Kwa hiyo kama serikali hiyo hiyo inawacheweleshea mishahara walimu...Halafu inawapa mikopo ya riba kubwa kwa kigezo hicho hicho cha kutokuwa na uhakika wa cheki zao mwisho wa mwezi si UNYOYAJI HUO?

Ni lini wameshawahi kuwajali walimu?

KAMA WALIMU WANGELIPWA INAVYOTAKIWA WANGEENDA KUKOPA MILIONI YA NINI?

Serikali haiwajali walimu na walimu shirikini kwenye madai ya UHURU!

Riba kubwa wapi wewe ?
Mimi ninachoamini hadi sasa kinacho wa cost ni mda wa kulipa deni na wala si riba .Naongea hapa kama Engineer na si mwana siasa.

Mwalimu mshahara wake Tsh 70,000/= ana familia ya watoto wanane ama zaidi Na amekopa milion 5 kujenga nyumba.Kwa vyovyote vile akiambiwa mfano arudishe kila mwezi kiasi gani atasema 20,000. ukija kuangalia mda huo wa kulipa deni + siasa za kudandia migongo + mahesabu ya kisiasa utakuta kuja kumaliza deni riba itakua 500%.
 
Jmushi
Mwanatanu ame google hii info

» Posted by Elizabeth Nelson in Category: Africa, Deals, Investment Funds at 12:03 am

Investment AB Kinnevik, a Stockholm-based international investment firm, announced that it has invested USD 14 million in the African microfinance institution (MFI) Bayport Financial Services. The financing is provided as a combination of debt and equity.........

........According to a Kinnevik press release, the financing of Bayport is the second major investment in the area of New Ventures for Kinnevik this year. In May, the firm invested in Gateway TV, a company which offers satellite-based pay-TV services in Sub-Saharan Africa. It is expected that the service will be available in 8 countries by the end of 2007. In total, Kinnevik has invested USD 124 million (SEK 800 million) in New Ventures, and the market value of new ventures at the end of second quarter 2007 was approximately USD 150 million (SEK 969 million).

Bayport, founded in 2002, currently has 1,000 employees and 61 branches in Zambia, Tanzania, South Africa, Ghana and Uganda. Bayport serves 150,000 clients, the majority of whom are employed but are unable to access conventional sources of credit. About 20 percent of the MFI's clients are civil servants who live in rural villages. Bayport deploys teams that travel to villages to disperse loans to people who would otherwise be unable to access financial services.

Bayport clients use the loans for a variety of purposes. Thirty to 40 percent take out loans to pay for education. Twenty percent borrow to fund home improvements. The rest of the loans serve various functions, including funding small businesses and consolidating more expensive debt.

Bayport's loans range in size from just USD 20 up to USD 1,500. The average loan issued is USD 250–no small amount considering that a teacher in Zambia earns just USD 200 per month. Annual interest is between 70 and 90 percent. The MFI's repayment terms range from one to 36 months, and repayment rates are high (96.5 percent in Zambia).
 
Riba kubwa wapi wewe ?
Mimi ninachoamini hadi sasa kinacho wa cost ni mda wa kulipa deni na wala si riba .Naongea hapa kama Engineer na si mwana siasa.

Mwalimu mshahara wake Tsh 70,000/= ana familia ya watoto wanane ama zaidi Na amekopa milion 5 kujenga nyumba.Kwa vyovyote vile akiambiwa mfano arudishe kila mwezi kiasi gani atasema 20,000. ukija kuangalia mda huo wa kulipa deni + siasa za kudandia migongo + mahesabu ya kisiasa utakuta kuja kumaliza deni riba itakua 500%.

Walimu na wafanykazi angalieni vigezo na maneno haya na mjifunze muache UNAFIKI!
Na kama kuna mwananchi atakayeipigia kura ccm kama mambo yatabakia hivi...Basi na mimi nitakata tamaa rasmi.
Nawaachia wananchi KESI.
 
Jamani hizi financial institution zingine zinatia kichefu chefu maana zinakuja kwa mgongo wa kumkomboa mfanyakazi au mfanya biashara au mkulima, simply kwa nia ya kumuibia.
Watu wengi hapa Tanzania nimegundua when they just get seduced to take loans hawajiulizi maswali zaidi ya kukimbia kuchukua. That's where the problem arises.
Unaona kwa ripoti ile kampuni hiyo imeweka wazi kwamba wanalipisha riba ya 70% to 90% kwa mwaka na mkopo unakwenda hadi miaka 3 hii ni riba kubwa sana!
Kama walivyoshauri wengi kwa riba hiyo na hasa kama ni compound interest inaweza kuwa mwisho wa mkataba mkopaji karipa 200% hii si ajabu.
Kinachoumiza mioyo ya watu wengi ni kwamba Mama Mkapa akijua wazi kwamba hili linafanyika kwa kutumia kampuni yake huku akiaminiwa kama mke wa kiongozi safi aliwaingiza walimu mkenge bila kuwambia ukweli.
Na wanaowalaumu walimu wanawalaumu bila sababu maana walimu si wataalam wa financial deals, bali kwa shida zao wanatafuta kila anayeweza kuwasaidia wamalize shida walizo nazo kama elimu kwa wana wao, afya kwa matibabu ghali ya Tanzania na kununua mahitaji ya muhimu kwa ajili ya familia zao.
Hapa ndipo tu mama huyu anastahili kulaumiwa. Otherwise ni fisadi kama mafisadi wengine.
By the way mbona hawamu mbili zilizopita ma first lady wamekuwa mabingwa wa ufisadi?
Mama JMK b careful nawe usije ukatufisadi basi!
 
Back
Top Bottom