Wakenya, naskia kuna Wakurya na Wachaga upande wa Kenya, can you share with us your views on them?

Wadigo,wameru, wamakonde,wanyasa wapo Kenya na Tanzania
Wanyakonde na wanyasa hawapo Kenya. Alafu sidhani kama wameru wa Kenya na wale wa Tanzania wanakaribiana
 
Nimewahi kukaa na wakamba, their language sounds like Kurya.

Nadhani wanaelewana wakiongea
Hawaelewani kabisa. Wakamba are eastern bantus while Kurias are western Bantus. Eastern bantus and western Bantus lugha zao haziendani. Ndio maana wakisii wanaelewana na wakuria coz both are western Bantus just the same way kikuyus and kambas pia huelewana coz they are eastern Bantus
 
Sometimes i wonder where tanzanians got this kenyan names
Nyambura
Chege
Kairuki-kariuki
Mungai etc
Nadhani ni kwasababu ya changamoto za hapa na pale, kwa huku tz kuna wangoni, wao walikimbia vita zamani sana south africa wakafika mpaka kusini mwa Tz kwenye mkoa unaitwa Ruvuma.
 
Wakurya wa kenya sana sana tumejikita katika kilimo cha mazao sana miaka ya karibuni kutokana na kupungua kwa ukubwa wa mashamba tofauti na ilivyo TZ ambapo wameegemea ufugaji wa ngombe. Upande huu wa kenya wakurya wanapatikana County(Jimbo\gatuzi) la migori ila tumekua tukituma maombi tupate pia sisi county.

Tumepakana na Jamii ya Luo,Suba na Maasai na uhasama kwa sababu ya wizi wa mifugo upo kati ya kuria na Maasai.Kilimo biashara kinachoendelezwa huku Kuria kenya ni kilimo cha viazi vitamu, mahindi ufugaji wa ngombe na tumbaku. Miji mikubwa iliopo Ni kama Isebania\sirare, Kehancha, Ntimaru kegonga Mabera.
 
Wanyakonde na wanyasa hawapo Kenya. Alafu sidhani kama wameru wa Kenya na wale wa Tanzania wanakaribiana
Kakuongopea nani kenya hamna wamakonde? Au wanyasa.

Katika makabila 44,wamakonde na wahindi, ulishawahi kwenda ile njia ya mombasa to malindi?
 


MK254 yupo katika #6 🀣
 
Mhm mkuu hawa Wanyambo wa Karagwe Kagera na Waluhya wa Kenya wana unasaba mbona hata geography haisomi kabisa naona wanyambo wana unasaba na wanyarwanda SIJABISHA NAOMBA KUELIMISHWA

Wahangaza kwa kiasi kikubwa ndio wanyarwanda (watutsi) ila wanyambo wameegemea zaidi kwa wahaya. Kiufupi Ukifika uhayani kuna makundi mengi mfano waziba wa bukoba, wanyaihangiro wa muleba na hao wanyambo wa karagwe. japo huwa kuna mtafaruku kujua wanyambo ni wahaya

Connection ya wahaya na waluhya yaweza kuwa hii.. Wahaya inasemekana origin yao ni Bunyoro ambayo kwa kiasi kikubwa ipo Eastern Uganda, Waluhya wapo Western Kenya hivyo ukiangalia jiografia utaona wanapakana.

Ukiangalia flow utaona western Kenya, Eastern Uganda hadi North western Tanzania ambapo ndipo wahaya wanapatikana ...
 

Umeiweka vizuri sana

Mara ya kwanza kumsikia Mnyambo anaongea kwa simu nilidhani Mluhya maana Kiluhya nakifahamu (mashemeji wangu), ila kwa namna fulani maneno yalikua yanapishana lakini kwa asilimia kubwa wanachangia maneno mengi sana hata desturi na tamaduni.
 
Kakuongopea nani kenya hamna wamakonde? Au wanyasa.

Katika makabila 44,wamakonde na wahindi, ulishawahi kwenda ile njia ya mombasa to malindi?
Huenda wamakonde wapo ila idadi yao ni chini sana halafu sidhani kama wanaongea lugha sawa na wamakonde wa Tanzania (not sure about this though). Wanyasa nao hawapo Kenya kabisa.
 
Wanyakonde na wanyasa hawapo Kenya. Alafu sidhani kama wameru wa Kenya na wale wa Tanzania wanakaribiana
Wamakonde are few and they were given citizenship three years ago. Although they came to Kenya from Mozambique in the 1960s, so they are not an original Kenyan tribe.
 
MK254 eti Mnyambo? Hehe
 
Kakuongopea nani kenya hamna wamakonde? Au wanyasa.

Katika makabila 44,wamakonde na wahindi, ulishawahi kwenda ile njia ya mombasa to malindi?
Hao Wamakonde sio original Kenyan tribe. Hao walitembea kutoka Mozambique na kufika Kenya in the 1960s. Walipewa uraia wa Kenya miaka mitatu iliyopita na Rais Kenyatta.
 

Wewe nakuelewa yaani bado kukijua kiluguru cha morogoro tu 😁😁😁
 
Eroo loonchore, kae moda ninye? Mpuusu! [emoji1]
 
Yes, wadigo wanapatikana kote kote. Mfano, balozi wa sasa wa Kenya nchini Tanzania mhe. Danny Kazungu, ni mdigo wa kutokea Malindi Kenya.
 
Fyi, there are also kambas in both countries.

It's crazy when you realize just how similar the demographics are in the two countries
 
Huyo ata nashuku ni Mkuria but most Kenyans assume anyone by the name Chacha, Mwita, Marwa, ni mkisii. The most prominent Kuria huku would be senator Machage of Migori county
Not most Kenyans,it's you who assumes,kisii wanajulikana wanatumia Sana "O" just like luos ,kwa wakuria hakuna O kwa wingi, they are many kurias in government ,hata the current Ps for devolution Nelson marwa is from kuria.
 
Nchi ambazo Zina muingiliano wa jamii Africa mashariki kwa wingi Ni Tanzania na Kenya ,Kuna maasai,luo,suba, meru,kuria,digo, Kuna kabila tanzania la mijikenda Sina uhakika Kama wanatumia lugha sawa na mijikenda la Kenya kwa sababu mijikenda huku Ni mkusanyiko wa kabila ndogo Tisa wadigo wakiwa ndani,pia Kuna wakikuyu tanzania na wakikuyu Kenya ,Kuna wakamba Tanzania pale morogoro japo kwa wingi wapo kenya,Kuna Tanzania kabila la kisi japo Sina uhakika Kama wanatumia lugha sawa na wakisii wa kenya. Pia nilisikia prof.palamagamba akisema anatoka Iringa tanzania japo hakutaja kabila lake kwa jina lakini alisema Hilo kabila lake huku Kenya linaitwa kipsigis ambalo Ni kabila dogo la jamii kubwa ya kalenjin.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…