Wakili msomi Peter Kibatala: Wasifu (CV) wake na historia yake katika kuendesha kesi

Wakili msomi Peter Kibatala: Wasifu (CV) wake na historia yake katika kuendesha kesi

Mjina Mrefu

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2016
Posts
3,045
Reaction score
3,389
Wakuu,

Ni kuhusu huyu wanayemwita wakili msomi.. Yaani Peter Kibatala. Kila siku nasikia Kibatala, Kibatala. Tujuzane wakuu.

CV yake

Kashinda kesi ngapi?

Kashindwa kesi ngapi?

Tujuzane tumjue huyu wakili anayeitwa msomi

======

Peter Kibatala said:
Nimewahi kuwa Makamu wa Rais wa TLS;2012-2014.
Nimewahi kuwa voted kama Most Influential Young Tanzanian upande wa Law.

Nimeendesha cases za watu maarufu wafuatao:

1. Wakili wa kwanza kupangua mashtaka ya Ugaidi Nchini katika cases za Ugaidi za Wilfred Lwakatare na mwenzake [Mahakama Kuu Kanda ya Dar 2013] na Henry Kilewo na wenzake [Mahakama Kuu, Tabora 2013].
2. Case ya Elizabeth Michael Kimemeta @ Lulu.
3. Case ya Uchaguzi ya Fred Mpendazoe pamoja na case nyingi za Uchaguzi kama vile Halima Mdee na Suzan Kiwanga.
4. Cases zote za Uchochezi za Tundu Lissu ambazo ama alishinda au zilifutwa.
5. Cases za kufutiwa Uwakili Fatma Karume [ambapo baada ya kufutiwa Uwakili alishinda mbele ya Jopo la 3 Judges Mahakama Kuu na AG anakata Rufaa].
6. Case ya Kajala Mahakama Kuu.
7. Case ya Wema Sepetu [kabla Msando hajaichukua].
8. Case ya kina Mbowe ya Maandamano yaliyopelekea Akwilina kuuawa [walishinda Rufaa Mahakama Kuu na kuamriwa warudishiwe fines zao].
9. Case ya Ugaidi ya Mbowe ambayo ilifutwa na DPP hatimaye.
10. Cases mbalimbali za Halima Mdee za maandamano ya BAWACHA [ilifutwa na Mahakama].
11. Cases za Gwajima [ya kupatikana na silaha na ya kumtukana Pengo na zote alishinda].
12. Case ya jinai ya Mbunge wa zamani Mtwara Mjini Hasnain Murji ya kupinga gas kutolewa Mtwara [alishinda].
13. Cases za Uchochezi za Yericko Nyerere [alishinda mbili Kisutu, na moja Rufaa Mahakama Kuu Dar].
14. Case ya Uchochezi ya Sugu [alishinda Rufaa Mahakama Kuu Mbeya na rekodi kufutwa].
15. Sasa naendesha case ya Mauaji ya mke wa "Bilionea" Msuya.
16. Case ya kupinga uenyekiti Augustin Mrema TLP [alishinda].
17. Case ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Air Tanzania David Mattaka [aliachiwa huru na kupigwa fine ndogo].
18. Case ya kupinga kauli ya Waziri Mkuu wa zamani Mizengo Pinda kusema "wanaondamana wapigwe tu" [Mahakama Kuu ilisema Wabunge hawana kinga isiyo na mipaka kwa kauli wanazotoa Bungeni, principle ambayo ni ya muhimu sana].

Naendesha case ya kudai haki ya Uraia Pacha kwa niaba ya watu wa Diaspora
 
Ukitaka ya Peter (wangoni wanaita peteri) basi tuletee ya msomi wa Lumumba "Godwin Kunambi" aliyekua mwanasheria wa CCm na sasa analinda interest za mzee kipara Dodoma kama DED! hivi kuna kesi aliwahi shinda?? jamaa level zake kama Monday likwepa rais wa bao!
 
Kijana mdogo tu ambaye anaipenda kazi Yake ukipata kumuona mda anaifanya Kazi yake utapata kujua kijana anajua anachokifanya habatishi

Nadhani hata aliosoma nao shule wanaweza kuwa mashuhuda kuwa inaonekana hata shule uko alikuwa anafanyae vizuri sababu anajiamini sana na anapenda anachokifanya
 
Ukitaka ya Peter (wangoni wanaita peteri) basi tuletee ya msomi wa Lumumba "Godwin Kunambi" aliyekua mwanasheria wa CCm na sasa analinda interest za mzee kipara Dodoma kama DED! hivi kuna kesi aliwahi shinda?? jamaa level zake kama Monday likwepa rais wa bao!
Mm na Lumumba wapi na wapi mkuu
 
Kibatala ni Mwanasheria wa kawaida sana!

Nimesoma mahojiano yake jana Mahakamani kuhusu kesi ya Dikteta Uchwara ana maswali ya kitoto sana!

Tatizo lenu wengi " Lugha" haipandi mngetazama Citizen Tv, KTN na K24 muone nini maana ya Wanasheria wasoma na sio upuuzi wa eti KIBATALA!
Maswal ya kitoto yale? Uliona yule Shahid alivyojichanganya na maswali yale yale usemayo ni ya kitoto?
 
Kibatala ni Mwanasheria wa kawaida sana!

Nimesoma mahojiano yake jana Mahakamani kuhusu kesi ya Dikteta Uchwara ana maswali ya kitoto sana!

Tatizo lenu wengi " Lugha" haipandi mngetazama Citizen Tv, KTN na K24 muone nini maana ya Wanasheria wasoma na sio upuuzi wa eti KIBATALA!
Lengo la cross examination ni kumfanya shahidi aonekane si mkweli ili hakimu au jaji na wazee wa baraza wautlie shaka ushahidi anaotoa.
Baada ya maswali ya Kibatala juzi wewe bado unaona kuwa yule fundi washi anaaminika?
 
Back
Top Bottom