Wakili Msomi: Yanga wamefanya uzembe kwa Feisal

Wakili Msomi: Yanga wamefanya uzembe kwa Feisal

Yan watu wanaikurupukia hii issue wengine hata hawaelewi kinachoendelea. Hapa kinachozungumzwa ni utaratibu uliotumika.

Sasa mtu anaandika utafikiti anahara. Mbumbumbu utabaki kuwa mbumbumbu tu. Heshima kwako Rage uliyaona mbali hata mambumbumbu
 
Kwanza anapaswa aelewe kuwa Neymar hakuwalipa Barca gharama za pesa walizomsaini bali aliwalipa Barca pesa kulingana na thamani waliyomuwekea endapo kama kuna klabu itamuhitaji(release clause/buyout clause)
Shwaini wengi wanajua pesa aliyorudisha fei ni yake kumbe ni kama anawarudishia Yanga pesa yao (signing fee),Yanga wakiridhia kupokea ile pesa basi itabidi wataje pesa yao kukubali kuvunja mkataba,kama ilivyo kwa wachezaji na makocha tunavyosikiaga fifa imewataka iwalipe kwa kuvunjiwa mikataba na ni hivyo kwa wachezaji,fei akae chini na Yanga wamtajie kiasi wanachotaka awalipe asepe sio aamke tu asubuhi akadeposit pesa kwenye acc ya Yanga eti ndio kavunja mkataba!
 
Kweli huijui sheria, na hata vipengele vya kisheria kwenye mikataba huvijui pia maana yake.

Hapo suala sio lazima mpaka viongozi wa Yanga SC wakae na Azam ndio waongee biashara, muhimu ni kama umeweka kipengele kwenye mkataba wa mchezaji wako kinachomruhusu kuondoka aki deposit kiasi fulani cha pesa, basi hapo umejibana mwenyewe.

Mchezaji ataondoka wakati wowote akiamua, muhimu aweke pesa mliyotaka kwenye akaunti yenu, hapa suala la Yanga SC kuongea na Azam linakuwa halina maana tena, halipo, kwasababu mchezaji ameshavunja mkataba na Yanga SC kwa kuweka mzigo kwenye akaunti, huyu sasa ni sawa na mchezaji huru.
Mkuu unaongea point ila nasikitika kuna vitu bado havijui kwenye mkataba na sheria na taratibu za FIFA na TFF. Hawezi kufanya hivyo unavyoandika ikiwa msimu wa ligi unaendelea.

Azam kama walikua wanamtaka Feisal dirisha dogo ilibidi wafanye mazungumzo na Yanga na sio uhuni waliofanya. Sijui walishauruwa na kiazi gani
 
Hi I unajua kuna tofauti ya signing fee na release clause? Neymar aliwalipa Barca signing fee au release clilikuwa

Mktaba wa Neymar ulikuwa na kipengele cha kulipia 220 million euro kama buyout clause. Na ndo alichokifanya kwa kulipa hiyo hela.. akawa huru. So akaenda PSG kama mchezaji huru.
 
Wakili na mwanamichezo mzoefu nchini, Aloyce Komba ametoa ufafanuzi juu ya dili la Fei Toto kutua Azam akisema:
.
“Yanga wamefanya uzembe wenyewe na wasije wakathubutu kukimbilia Fifa kama walivyofanya kwa Bernard Morrison itakula kwao. Waangalie vizuri mkataba wa mchezaji unaeleza nini, watapoteza muda zaidi.”
.
“Ninachokiona Yanga walimpa mkataba Fei ambao hauna faida kwao. Unawekaje kiasi hicho cha pesa kuvunja mkataba wake wakati unaona kabisa kiwango cha mchezaji kilivyo. mchezaji hawezi kuacha pesa hasa kama mkataba wake unaruhusu kuununua ama kuuvunja.”
.
“Sioni kama Azam wamekosea na ni timu ambayo inazingatia sana masuala ya kisheria katika kuvunja mikataba ya wachezaji wao ama wanaposajili mchezaji. Azam siyo wajinga kiasi hicho wakurupuke tu kumsajili Fei Toto pasipo kuzingatia taratibu za kimkataba.
.
“Wanachotakiwa kukifanya Yanga ni kuulezea umma ama wanachama na mashabiki juu ya hilo, lakini mengine ni kuleta siasa tu kwenye mpira.”

My Take
Nawakumbusha tu Yanga kuitwa Utopolo ni maono ya ndani sana. Hii ndio maana halisi ya Utopolo
Wakili msomi fikiri vizuri hakuna mkataba unavunjwa na pande mmoja, kwani wewe ukiingia mkataba na mteja wako yeye ghafla tu anaweza kuvunja mkataba bila kijadiliana na wewe?

Pia mkataba uusome wewe kwanza kabla ya kutoa maoni, haya mitandaoni kuwa mkataba ukikuwa hivi ama vile sio sahihi.
 
Ukisoma comments nyingi humu mashabiki wengi wa Simba wanamikurupuko na misharuko kuhusiana na hii issue ya Feitoto lakini wengi kwa comments tu unajua kichwa maji
 
Feisal yuko sahihi kwa 100% kisheria.
Ameamua kuvunja mkataba na Yanga kwa kulipa gharama yote inayotamkwa na mkataba wake. Hakuna tena suala la kukaa mezani, kukubaliana au kupatana. Mkataba wa Feisal imetamka yote na wote umefuatwa. Feisal kwa sasa ni mchezaji huru, ana uhuru wote wa kwenda klabu yoyote hata bure. Na Yanga kwa sasa hawahusiki chochote na Feisal.
 
Issue sio kuvunja mkataba, swala ni utaratibu wa kuvunja watu wana twist story mimi mwanzo nlikua upande wa Feisal ila nmefatilia nmegundua kuna sehemu haipo sawa
Kuna kipengele cha kuvunja makataba (bila sababu) endapo tu mchezaji ataweka mezani (kununua mkataba) tsh. 100m za usajili na mshahara wa miezi mitatu 12m. Fei na washauri wake wameona huo mwanya na wameutunia, mengine ni kujifariji tu.
 
Hapo sijui Sheria is kuna raia ni vilaza sana kwenye soka,umeona wapi mchezaji mwenye mkataba na timu anasajiliwa na timu nyingine bila hizo timu kukubaliana? Yaani Leo Jude Bellingham apokee pesa kutoka Man City akailipe Dortmund then awe mchezaji wa Man City bila City na Dortmund kukubaliana?
Basi wachezaji wengi sana wangesepa Kwa namna hiyo.
Utopolo akili zenu ni robo kijiko! Fei hajasajiliwa na team yoyote akiwa ndani ya mkataba, amevunja mkataba kwanza then usajili utafata. Kwasasa ni mchezaji huru, atakuwa huru kujiunga na club yoyote wakati nyinyi mkipoteza muda kukata rufaa!!!!
 
Feisal yuko sahihi kwa 100% kisheria.
Ameamua kuvunja mkataba na Yanga kwa kulipa gharama yote inayotamkwa na mkataba wake. Hakuna tena suala la kukaa mezani, kukubaliana au kupatana. Mkataba wa Feisal imetamka yote na wote umefuatwa. Feisal kwa sasa ni mchezaji huru, ana uhuru wote wa kwenda klabu yoyote hata bure. Na Yanga kwa sasa hawahusiki chochote na Feisal.
Mikataba ya football haipo hivyo inafuata msimu hauvunji tu kama taraka ya ndoa
 
Kuna kipengele cha kuvunja makataba (bila sababu) endapo tu mchezaji ataweka mezani (kununua mkataba) tsh. 100m za usajili na mshahara wa miezi mitatu 12m. Fei na washauri wake wameona huo mwanya na wameutunia, mengine ni kujifariji tu.
Leta huo mkataba hapa tuone
 
Shwaini wengi wanajua pesa aliyorudisha fei ni yake kumbe ni kama anawarudishia Yanga pesa yao (signing fee),Yanga wakiridhia kupokea ile pesa basi itabidi wataje pesa yao kukubali kuvunja mkataba,kama ilivyo kwa wachezaji na makocha tunavyosikiaga fifa imewataka iwalipe kwa kuvunjiwa mikataba na ni hivyo kwa wachezaji,fei akae chini na Yanga wamtajie kiasi wanachotaka awalipe asepe sio aamke tu asubuhi akadeposit pesa kwenye acc ya Yanga eti ndio kavunja mkataba!
Ndugu yangu bado uko nyuma.
Haihitaji Yanga wakae wakubali au wakatae kupokea Pesa ya Feisal, suala ni mkataba umefuatwa, basi. Hakuna tena suala la kujadili ikiwa sheria (mkataba) imefuatwa. Baada ya Feisal kutimiza hilo takwa la kuwarejesha Yanga Pesa zao, maana yake Feisal yuko huru kwa 100%. Hakuna tena pesa ya kumdai wala kufuatilia wapi atakwenda.
 
Mkataba wa football sio kama chumba cha kupanga kwamba unavunja tu sheria za FIFA zipo wazi sababu mna mihemuko endeleeni kujifariji
Rejea ya Neymar utanielewa, mlijichanganya kuweka kipengele cha kuvunja mkataba endapo mchezaji ataweka dau (kununua mkataba wake) Fei kaweka mzigo now yuko free.
 
Back
Top Bottom