Wakili Mwabukusi, Emmanuel Masonga na Mdude Nyagali wakamatwa na Polisi Mikumi wakiwa safarini kuelekea Dar es Salaam

Usifananishe Watanzania na kenya mzee.

Watanzania ni Waoga , hata usijipe moyo mkuu.
 
Tawala za Kiafrika hazijawahi kukombolewa...
 
Wana celo za kuwahifadhi Watanganyika wote tunaopinga bandari zetu kuporwa?

Viwango hivyo vya HOFU tulishavivuka.

Tusubiri.
Si ajabu unaandika huku unasubiri ugali wa shikamoo hapo.
 
Miye nawalaumu tuu kujipakiza gari moja, hapo mwingine angekwea mwewe, mwingine treni, na mwingine angepanda basi hadi iringa akatokea Dodoma zen akarudi Dar. Umafya umafya tuu maisha kuwindani km nyati na simba porini.
Hapo ndio mwisho wa akili yako?
 
Hawawezi hao.
Siasa za CDM za kizamani sana.
Hapo nyuma CDM niliipenda sana , ila tabia zao za undumilakuwili hapana kwakweli.
Kabisa mkuu,zamani CDM ilikuwa moto.,enzi zile za miaka ya 2008-2011 chini ya DK Slaa. Alikuwa mstari wa mbele kudai haki.
 
Endeleani kumshika sharubu Simba.Siku akiwapa mnachotaka msilalamike.Hawa wengi wana hamu ya kurudi kwa Nyapara,wapewe mambo yao.
 
Siyo "yakiri", yatangaza.

Kwani walificha wapi na walitangaza mapema kuwa watu wanaochochea na kutaka kufanya uhaini watakamatwa, na wanatutangazia kuwa wawili tayari na wengine wapo njiani kukamatwa. Huko siyo kukiri, huko ni kutangaza.

Usicheze na maneno. Sababu za kushikwa kwao zinajulikana. Kauli za kishenzi walizokuwa wanatowa haziashirii amani hata kidogo.

Tena bahati yao, kama ni USA wanafinywa tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…