Wakimbizi wa Kiafrika wapigwa mpaka kifo huko nchini Hispania

Ardhi ngum sana hii, Inahitaj angalau Rangi nyingine ikalie kiti, Hii Green/Yellow unafiki sana.
 
Wakimbiz ni case special kabisa huwez kuwafananisha na mzigo wa wahindi na wachina wanaotuovertake huku mitaani.
Wale ni watu wanapewa hifadhi ya Muda chini ya uangaliz wa Sheria za kimataifa.
Hawa koko wao wamegeuza bongo goli lao la upigaji.
 

Sasa hizo chuki huwa zinatoka wapi?
Kwanini mtu atukane dini ya mwenzie kama sio mafundisho
Watoto wanakuwa na kucheza pamoja bila kujua udini wa ukabila na huchangia kila kitu
Sasa Kwanini wanabadilika kama sio kuambiwa na wakubwa?

Mtu ana marafiki wa dini nyingine lakini hawezi kuweka hisia zake mbaya live ila huku nyuma ya keyboard ndio anakuwa kama sio yeye

Mimi sio wale wale kama unavyowaza wewe ila sipendi ushari una jambo mwambie mtu moja kwa moja ana kwa ana na muache woga
 

Tanzania ina uhusiano mzuri na nchi zote ila wakimbizi waafrika wenzetu waliokumbwa na machafuko na ndugu zao kuuwawa na nyumba zao kupigwa mabomu na ndugu zao
Pindi wanapokuja kwetu unaona wanavyodhalilishwa na hao hao unaowaita marafiki na ndugu moja?

Wanawekwa jela wakimbizi na kuporwa kila kitu walichonacho Halafu wanaitwa waandishi wa habari na kupiga picha kama wamekamata majambazi

Naona hufuatilii kabisa habari za dunia hata ndani ya nchi yako au unajitoa ufahamu tu

Tangu lini nchi za africa zikasaidiana hao unaosema wasiende Ulaya ila wabaki kwa ndugu zetu
Unajua xenophobia maana yake?

South Africa walivyowauwa waafrika walioenda kutafuta ajira hata ukiuza maandazi wanakuuwa Sasa wao wameshindwa kuuza maandazi

Fuatilia hali halisi ya maisha sio unaandika tu
Hakuna wabaguzi kama waafrika wenyewe kwa wenyewe

Ukishuka airport unaona mtu ana kazi yake ya heshima ila akumuona mzungu mpaka begi atambebea

Watu wanakuja ulaya kwa sababu sheria ni nzuri na kuna ajira kibao
Huwezi kukaa bila kazi Labda utake mwenyewe
Kama [emoji636] kuna ajira 220,000 kila siku mitandaoni ni wewe na nguvu zako

Kama ni biashara zina zaliwa kila siku zinasajiliwa zaidi ya 2000
Na rekodi iliyovunjwa walisajili 2095 siku moja

Sasa hapo Afrika Kuna ajira gani za kumuweka mtu akae hapo? Kama ni transit waacheni wakatafute maisha wewe inakuuma nini
 
Mimi hainiumi ila inakuuma wewe kwakua wanauliwa kama kuku ilhali wana nchi zao.

Hivi umeelewa nilichoandika au umekurupuka kujibu na mahisia yako hayo!??

Unaingia kinyemela nchi za watu utegemee kuachwa kipuuzi tu, hao wanaotangazwa ujue haikufaa wao kua hapa, hawakuingia kihalali.

Hivi unajua hapa nchini kuna makambi ya wakambizi?? Na hayo makambi si kuna wakimbizi!! Sasa hao wanaokamatwa nje ya kambi wanafanya nini?

Acha upuuzi wa kutaka uonewe huruma hapa na kuhalalisha uhalifu kwa kigezo cha huruma.

Hizo ajira ni kwa ajili ya wanaUSA na wale wanaoingia kihalali nchini kwao na sio watu kama wewe mnaoingia kinyemela kama majambazi na acha mpigwe shaba,rungu na mfie majini kila siku.
 
Mkuu hivi hufuatiliagi hayo mabishano kati ya ukristo na uislam kua wote hujibizana.

Labda wewe ni muislam kwahiyo unaona mapungufu kwa wenzio ila kwako huoni!!

Wanoongoza kwa kutenga/kushusha hadhi na kudharau watu wa dini nyingine ni waislam.
Katika kundi la kiislam mkristo unaonekan ni najisi, mnafundishwa kutoshirikiana na wakristo(makafir).

Nimeshangaa sana haya malalamiko yako, tulioishi sehemu zenye waislam wengi tumeona hii kitu.
 
Wakimbiz ni case special kabisa huwez kuwafananisha na mzigo wa wahindi na wachina wanaotuovertake huku mitaani.
Wale ni watu wanapewa hifadhi ya Muda chini ya uangaliz wa Sheria za kimataifa.
Hawa koko wao wamegeuza bongo goli lao la upigaji.
Ndio wakimbizi ni special case lakini unachokimbia kwako ni nini??

Ujue kuna mkimbizi na wahamiaji haramu. Hao wanaozamia huko wengi ni wahamiaji haramu na sio wakimbizi.
Ni sawa tu na mbongo/mkenya akutwe huko halafu auawe uje useme eti hao jamaa wana makosa!!.

Kwanimi basi msifate utaratibu mkaingia kama wakimbizi kweli badala yake mnaingia kinyemela tu.
 
wafuasi wa mudy ndo viherehere wa kuvunja utaratibu
 

Unajua wanaongia kihalali [emoji631] ni wangapi?
2017 walipewa visa watu 700,000 na ni laki tu ndio walirudi makwao na 600k walizamia na hawakutoka compare na 300,000 walioingia kinyemela

Usiongee kama mtoto kwani hoja inajibiwa na hoja hunijui sikujui Kwa hiyo nijibu kwa kutetea hoja zako bila jazba

Wahamiaji hawajaanza Leo hata wewe sio mtanzania kwani utakuta babu yako wa nne au wa 3 au wa 5 alitoka Malawi au bibi yako wa Burundi Kwa hiyo kuhama na kuingia katika nchi zingine ni kawaida kama kuna vita

Hata leo Ukraine wameamua kusema tunarudi kwetu
Wapi kwao? Israël wanaiita kwao wakati miaka yote walikuwa wanajiita Ukranians

Kuna lingine kwani huwezi kuzuia watu kutembea na kuamua wapi kwenda kuishi
You are nothing and you can’t do anything about it
 
Wewe ndie unaejibu kwa jazba, huko kujuana wala usingeandika hilo linafamika.

Na nahisi kuna kitu wewe hunielewi, na sijui ni hoja gani hasa unazotaka.

Hakuna mahali nimesema watu wasihame, unahama kihalali??
Msingi wangu ndo upo hapo, sawa unahama je unahamaje sasa!? .

Hao waliouawa nchi zao zilikua na changamoto gani!? Walifuata taratibu ili kuingia huko?

Ingekua ni raia wa nchi moja ama kweli hao waliowapiga kweli wengelikua na roho ya kinyama, wanajua changamoto za nchini kwao halafu wanawadunda tena badala ya kuwapa afueni.

Lakini hao sasa ni kutoka nchi mbalimbali, wanaingia kiwizi tu. Na hapo wakiingia wala hawajipeleki serikalini kupata vibali ila wanaishi kiharamia tu.

Hakuna huruma, hujafata taratibu DUNDWA, urudi kwenu.
 

Sio Kweli Mkuu hilo la kuwaita najisi ni uongo na sio uislam
Hatukufundishwa hivyo
Believe me tunakaa na Kula na wakristo kila leo na tunachangia mpaka vikombe

Kama unataka kuona chuki za wakristo angalia uzi mkristo anaanza kuuliza maswali kuhusu Uislam ambao haumhusu halafu kuna wapambe wataanza kutukana na kukashifu
Halafu angalia uzi mwingine aanzishe mkristo kuhusu ukristo hutaona muislam anadhihaki kwani hajui ni nini na hawezi kuchangia

Tunajua na tunaona kashfa na matusi kuhusu dini hizi lakini je inasaidia nini hata kama mtu kutwa atatukana ?
Does it make any good
Najua inaleta hasira na watu wanaamua kutukana kila aina ya matusi na kejeli

Mbona mitaani hatuoni mtu anaongea wazi bali upendo tu maana wa humu ndio hao hao wa mitaani
Uwe na siku njema
 
Ndgu yangu hizi dini 2 hakuna yenye uafadhali kweny kukashfiana kwa kila aina kashfa na dhihaka.

Mimi nachokishauri puuza, soma yanayokufaa kwa kuongeza maarifa tu ila sio kuichosha akili na moyo wako juu ya kashfa za watu humu.

Wengine huenda ni waislam wenzio ila wanaukashfu uislam basi tu ye anafurah na nafsi yake.

Na kuhusu mafundisho hata wakristo hatufunzwi kuchukia watu.
Sidhani kama kuna dini ya hivyo labda tu utofauti wa wafundishaji.
 

Mkuu mimi najua sana hali halisi ya ukimbizi
Nilikuwa vitani tena tatu
Ya mwisho ilikuwa uvamizi wa Iraq huko Kuwait

Nilikuwa Iraq ikabidi nikimbie niingie Jordan
Pindi vita inapotokea mahali huwa kuna immunity katika nchi husika
Tuliingia na magari yetu na kuelekezwa pa kwenda
Tulikaribishwa bila bughudha na wasiokuwa na passport zao waliambiwa wakaombe katika balozi zao kama huna balozi hapo kuna wawakilishi wa nchi

Nilikaa miezi miwili bila kuulizwa chochote natulipewa nyumba ya gorofa 16

Maisha yakikubana utaenda na kukimbilia popote utapopata uhifadhi Mkuu

Hapo nilipambana nikatoka na kuendelea na safari za kutafuta maisha
Huwezi kujua baada ya miaka kadhaa utakuwa wapi Kwa hiyo maisha hayana formula wala huwezi kupanga bali yanakuja tu

Sikutegemea kama ningemiliki uraia wa nchi nne

Ila leo nimazo mbili tu
Binadamu hawezi kuzuia mtu mwingine kufanya kitu
Mmoja atakataa uingie na mwingine anakupa shavu upande mwingine

Nimekuelewa sana unachoongea ya kuwa watu wafuate sheria waombe sheria za kuishi

Sasa mkimbizi utaomba viza ya Ulaya nani atakupa kwa kwenda ubalozini?
Ubalozi hautoi viza za wakimbizi Kwa hiyo watu wanaingia huko na kujilipua na baadae wanapewa sheria

Nchi za Ulaya western wanahitaji labour kila mwaka ndio maana wanawapokea ukiacha nchi njaa kama Greece
 

Asante kwa hilo na nashukuru kwa maoni yako
Siwezi kukashifu mtu ila huwa najaribu kuwaomba watu waache chuki that’s all

Nimekuelewa
 
Sawa kabisa lakini je hayo matokeo ya kujilipua nani alaumiwe??

Hatuwezo jua huenda hata mm nikajilipua siku moja lakini je nikijilipua na nikalipuka kweli nitalaumu nchi iliyonitendea ubaya?

Ila nimekuelewa mkuu baadhi yao huenda wangesikilizwa wangehurumiwa.
 
Waafrika wengi hawana akili. Wao ndiyo huwapa sababu mtu mweupe atuite nyani na atufanyie mambo kama hayo.
Africa is waste.
Hakuna anayemjali mwafrika popote.

Kuna mtu alisema baada ya miaka 25 kuna hatari Africa ikatawaliwa tena. Na hii inawezekana kabisaa. Wakati wengi wa mababu zetu walikataa kuuzwa utumwani au kuishi na mzungu leo tunamkimbilia Mzungu kama suluhisho la ajira, elimu, fedha, maendeleo na kutafuta maisha. Maana yake hata babu zetu wakiamka leo watatushangaa hata tunavyoiga utamaduni wao. Wakati sababu kubwa ya Nandi, Asante, Oba, Chief Songea, Kinjektile, na Kikuyu iilkuwa kupinga utamaduni wao.

Sasa hivi akifa mzungu ndo inaonekana kafa mwafrika si mtu. Hapo hakuna atakayetangaza genocide, mass killngs wala atrocities. Ni kama hakuna kilichotokea.

Halafu atakuja mtu kuleta story za kueaonea huruma Ukraine[emoji45][emoji3525]. Waacheni wauane tena kama vipi hata Nuke zipigwe tuuuu....kama inaisha na iiisheeee turudi mavumbini...kwa sh ngapi?
 

Mkuu njoo ujilipuwe tuwe wote
Maisha popote

Pia tuko pamoja sana
 
Duuuu!! Wasalimie wa hapo maeneo ya Chicago.

Sent from my CPH2127 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…