UZZIMMA
JF-Expert Member
- Nov 20, 2014
- 414
- 481
Siku moja mama aliniita alikuwa amekaa na baba ukumbini. Kilikuwa kama kikao cha dharura hivi. Mama akafunguka maswali yafuatayo.
Hivi mwanangu mbona sijawahi kuona, wala kusikia hata kidogo kama una mwanamke? Una tatizo gani mwanangu?
Mwenzako fulani analetewa hadi kesi kwa kutembea na watoto wa watu, wewe mbona sisikii lolote?
Na jambo kama hili lilitokea kwa ndugu yangu mwingine mtoto wa mama mdogo. Na rafiki yangu mwingine aliwekewa kikao kama hiki.
Mara ya mwisho rafiki yangu mwingine licha ya hao niliowataja alinihadithia tukio hili,
"mama yake alikuwa anatazama majina katika phonebook ya huyo rafiki yangu. Hakuona jina la kike hata moja. Mama yake hakujisikia vizuri akamuuliza. Mwanangu mbona sioni jina la kike hata moja? Una matatizo gani?
Kwa maelezo hayo nikagundua ya kuwa, wamama wanajisikia vibaya sana watoto wao wa kiume kutokuwa na mademu, tofauti na wababa. Na hii sijajua ni kwa nini. Kwa maana kwa upande wangu, baba hakuwa na wasiwasi ila ni mama. Na hao wote niliowataja wana baba ila wasiwasi ulikuwa ni kwa mama zao.
Hivi wadau hii imekaaje jamani?
Hivi mwanangu mbona sijawahi kuona, wala kusikia hata kidogo kama una mwanamke? Una tatizo gani mwanangu?
Mwenzako fulani analetewa hadi kesi kwa kutembea na watoto wa watu, wewe mbona sisikii lolote?
Na jambo kama hili lilitokea kwa ndugu yangu mwingine mtoto wa mama mdogo. Na rafiki yangu mwingine aliwekewa kikao kama hiki.
Mara ya mwisho rafiki yangu mwingine licha ya hao niliowataja alinihadithia tukio hili,
"mama yake alikuwa anatazama majina katika phonebook ya huyo rafiki yangu. Hakuona jina la kike hata moja. Mama yake hakujisikia vizuri akamuuliza. Mwanangu mbona sioni jina la kike hata moja? Una matatizo gani?
Kwa maelezo hayo nikagundua ya kuwa, wamama wanajisikia vibaya sana watoto wao wa kiume kutokuwa na mademu, tofauti na wababa. Na hii sijajua ni kwa nini. Kwa maana kwa upande wangu, baba hakuwa na wasiwasi ila ni mama. Na hao wote niliowataja wana baba ila wasiwasi ulikuwa ni kwa mama zao.
Hivi wadau hii imekaaje jamani?