Wakina mama hujisikia vibaya watoto wao wa kiume wasiposhughulika na wanawake

Wakina mama hujisikia vibaya watoto wao wa kiume wasiposhughulika na wanawake

UZZIMMA

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
414
Reaction score
481
Siku moja mama aliniita alikuwa amekaa na baba ukumbini. Kilikuwa kama kikao cha dharura hivi. Mama akafunguka maswali yafuatayo.

Hivi mwanangu mbona sijawahi kuona, wala kusikia hata kidogo kama una mwanamke? Una tatizo gani mwanangu?

Mwenzako fulani analetewa hadi kesi kwa kutembea na watoto wa watu, wewe mbona sisikii lolote?

Na jambo kama hili lilitokea kwa ndugu yangu mwingine mtoto wa mama mdogo. Na rafiki yangu mwingine aliwekewa kikao kama hiki.

Mara ya mwisho rafiki yangu mwingine licha ya hao niliowataja alinihadithia tukio hili,
"mama yake alikuwa anatazama majina katika phonebook ya huyo rafiki yangu. Hakuona jina la kike hata moja. Mama yake hakujisikia vizuri akamuuliza. Mwanangu mbona sioni jina la kike hata moja? Una matatizo gani?

Kwa maelezo hayo nikagundua ya kuwa, wamama wanajisikia vibaya sana watoto wao wa kiume kutokuwa na mademu, tofauti na wababa. Na hii sijajua ni kwa nini. Kwa maana kwa upande wangu, baba hakuwa na wasiwasi ila ni mama. Na hao wote niliowataja wana baba ila wasiwasi ulikuwa ni kwa mama zao.

Hivi wadau hii imekaaje jamani?
 
Moja ya hofu kuu ambayo huwaandama wazazi wa kiafrika ni ile inayohusu kuzaa mtoto wa kiume halafu aje kuwa shoga au hanithi.

Ndio maana wamama huwa wanakikisha kile kikamba cha kitovu cha mtoto mchanga wa kiume, hakidondokei maeneo jirani na uume wake wakihofia imani potofu inayohusu masuala ya uhanithi.

Kwa mantiki hiyo inawezekana ulipokuwa mchanga kitovu chako kilidondokea kwenye eneo nililotaja hapo juu. So anachofanya bi mkubwa ni kukuuliza ili apate uhakika kama yaliyomo yamo. Bi mkubwa wako yupo sahihi.
 
Mbwa asiyewinda/ kulinda ni mzigo kwa mfugaji. Lazima awe na wasiwasi maana wanawake ndio hutambishiana sana wajukuu. So hamu ya kupata wakamwana na wajukuu itamlazimu akuje kukuhimiza.

Kuna mama alinunua godoro jipya akampa kijana wake wa 25 years. Kila siku usiku anaenda kusikilizia kama atasikia sauti ya kwanza.

Baada ya mwaka alimwita mwanae na kusema " Asheri mwanangu naomba unirudishie godoro langu, yaani wewe unaita marafiki zako mnapiga story tu mpaka usiku. Sijawahi kusikia sauti ya mwanamke hata siku moja, siwezi kukuvumilia zaidi".

Jamaa alifariki akiwa na 33 years akiwa hana mtoto wala mchumba.
 
Ulikuwa na umri gani? Kama ulikuwa umemeliza masomo na una miaka kuanzia 20 mama yako kukuambia hivyo sio ajabu

Ila kama ndio ulikuwa shule ya msingi ama sekondar kisha mama anakushinikiza ukatafute wanawake, huyo mama yako alikuwa ni shangingi, stori kama hizo mnaongea na watu wa rika lako sio mama yako
Halafu atakutoleaje mfano wa rafiki yako kufunguliwa kesi kisa wanawake? anataka umuige? mbona ameoza sana kimaadili?
sorry kwa kum judge
 
Nimewahi kusikia wamama wakiongea stendi huyo mmoja alikua anamuhadithia mwenzie kuwa hamuelewi mtoto wake wa kiume kwamba hata akipita mdada mwenye tako jamaa hageuki [emoji23][emoji23][emoji23] sasa anashangaa jamaa anashida gani, hatamani au sio riziki. Jamani msiwape wazazi wenu stress.
 
Nimewahi kusikia wamama wakiongea stendi huyo mmoja alikua anamuhadithia mwenzie kuwa hamuelewi mtoto wake wa kiume kwamba hata akipita mdada mwenye tako jamaa hageuki [emoji23][emoji23][emoji23] sasa anashangaa jamaa anashida gani, hatamani au sio riziki. Jamani msiwape wazazi wenu stress.
Haha huyo maza anafikiri kila kijana wa kiume anapendelea mwanamke mwenye bonge la kalio!? Wengine huwa wanakufa na kuoza kwa wenye flat kama bappa ya upanga.
 
Back
Top Bottom