Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Hata Mimi ningekuwa me ningeoa mwanamke mwenye mtoto tayari walau mmoja! Kwanza mwanamke alozaa anakuwa amepevuka tayari. Anajua maana nzima ya Raha ya mapenzi[emoji39]! Lock zote zinakuwa zimetoka![emoji2960]!( Hii ni kwa wale wajuzi tu)
Hakuna kitu kama hicho mkuu!,nimeshawahi kuwa kwenye mahusiano na mwanamke mwenye mtt nikiamini ups and downs alizopitia kwenye mahusiano yaliyopita atakuwa amekomaa kiakili lkn kilichokuja kutokea Mungu ndio anajua
 
kuna watu wanajitoa mhanga vibaya sana hakyamungu😱
 
Habari ya mda huu wanajanvi!

Kama mada inavyojieleza hapo juu:

Hebu leo tujadiliane kwa pamoja juu ya swala hili linalo onekana kumea kwa kasi katika maisha ya sasa.

Je? Ni sababu zipi zinapelekea jambo hili lionekane ni "common" katika maisha ya
Sasa.

Binafsi naweza kulizungumzia swala la kuongezeka ma "single mother"
Kwa kulinganisha na sababu zifuatazo:-


Mtego wa mimba:
Asilimia kubwa ya mabinti/wanawake ambao hawajaolewa hivi sasa wamejenga tabia ya kujilaisisha kwa wanaume amabao wanaona kuwa wana vipato/ajira.

Jambo hili lime pelekea wengi wao(mabinti/wanawake) ambao wanatafuta uolewaji kudhani kuwa hiyo itakuwa sababu ya mwanaume huyo kumuowa na hatapia kubeba majukumu ya malezi kwa mtoto kama mzazi.


Malezi na Makuzi:

Hii pia ni sababu inayo changia kwa kiasi kikubwa.

Kutokana na mabinti wengi kukuwa na kulelewa katika familia zisizo fuata misingi ya maadili, imepelekea mabinti wengi kujiingiza katika vitendo vya uasherati.

Hebu tujadiliane mbali na saba tajwa hapo juu, ni sababu zipi nyingine zinazo pelekeà kuongezeka kwa ma"single mother ".

Nakalibisha maoni yenu.
 
Kibongo bongo sababu kubwa ni ujinga.

Wanawake wengi wamekua wakijihusinga na vitendo vya ngono bila kujua njia za kujikinga kupata ujauzito.
Unakuta binti hajui siku hatari za kushika mimba na siku salama ni zipi.
Na kutokujua matumizi ya condom

Matokeo yake ni kubemba mimba za wanaume wasio na malengo ya kuolewa nao.
 
Hizo ni sababu lakini sababu iliyokuu ni BAADA TU YA WANAWAKE WENGI KUPATA ELIMU YA JUU (CHUO KIKUU ) ndo tatizo lilianzia hapo,wengi wao sio watiifu tena kwasababu wanaelimu,hawako romantic kwasababu ya ubize na majukumu ya kutafuta hela,wanapenda haki sawa na kituma sana vijakazi wao,n.k kwahiyo hiyo sifa ya kupata elimu ya magharibi ndo imeambana na hayo yote ambapo matokeo yake hakuna mwanaume anaependa kuishi na mwanamke wa type hiyo na hatimaye kujikuta wanapigwa mimba tu na kuachwa,kwa wale ma single mother ambao hawajapata western education ni kiherehere chao na tamaa zao za kupata urahisi wa maisha kupitia mwanaume na hatimaye kushindwa kuplay part yao kwenye mapenzi.mwanamke mwenye maslahi hata romance zake ni za kuigiza. Naishia hapo kwa leo
 

Kweli kabisa
 
Wazo la kuolewa linawatesa Dada zetu...wakishakuona kwako wakarizika kiasi plus peer pressure wanayokutana nayo, anaanza kuwaza anaweza kuwa mkeo hapa atajiachia kama mke mwishowe mimba..hapa akijua kipato chako anajua kabisa huyu anaweza kuja kwetu kutoa mahali kumbe naye boy anawaza mipango àjenge kwanza au anunue gari...mimba ikishatokea na baba hakuwa tayari kuwa baba muda huo ugomvi unatokea then binti anazidi kupanic anapoona anazalia nyumban (anahisi watu wameanza kumdharau) na wengi hapa wanatumia mtoto kama fimbo ya kumuadhibu mwanaume kuombwa hela kwingi mwishome me nae anaona huu ni ufala liwalo na liwe. hapo hao wawili ndoa inakuwa ishaota mbawa.
 
tatizo lingine ni kuwa mabinti wengi wanataka wawe.wana maamuzi na mashuri kwa.mabwana zao.
Hiii dhana huwa inazaa laana kubwa ya kuachana
 
Mimi mwenyewe naona tu niongeze idadi ya singo maza mmoja maana nimejaribu kuishi na pisi week moja tu ndani ya siku mbili nimeshachoka.
 
Naombeni muwaache hawa wamama waishi kwa amani mwaka huu, maan kila kona singo mama, singo mama dah ebu muwaache.
 
Kwa kuongezea tu mabinti wameasi imani zao na kutokua na hofu ya MUNGU kitu kinachozalisha ujinga ,upumbavu kujiona n.k n.k hali inawapelekea kuzalishwa na kuachwa pekee yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…