Wakoloni walituletea dini kama kinga kwao ili watutawale

Wakoloni walituletea dini kama kinga kwao ili watutawale

Mkuu ukiulizwa A unajibu C.

Sijaona maana ya kujakueleza tafsri yako ya neno imani,jamaa una majibu mepesi kwenye maswali magumu.
sina hakika km tunaweza kuelewana aiseee yaani dini imekuingia sana tatizo ndio sababu tunashindwa kuelewana
nishakwambia mara kadhaa dini sio Mungu,
 
watu hali mbaya mpaka wanaanza kukufuru, Muombe Mungu japo huna imani hiyo akusaidie , daaaaa ugumu wa maisha ni kipimo cha akili
mkuu kufuru ndio nini? na nanni anayekufuriwa kwenye huu uzi?
hivi ndivyo wakoloni walivyowaagiza wa missionary wawaambie kuwa msihoji jambo lolote linahusu dini, mkihoji mnakufuru, ujinga wa hali ya juu huu
 
Huwa naumia sana pale ninapozungumza na marafiki zangu ambao ni walokole nikawataka wawafanye viongozi wa makanisa yao wawe countable kwa sadaka na zaka wanazotoa, huwa wepesi sana wa kukasirika wakidai hayo wanamwachia Mungu wanachoangalia wao ni kuwa maombi yao kwa kupitia hao viongozi wao yanajibiwa bila shida yeyote. Halafu bahati mbaya viongozi wengi wa dini hawawafundishi waumini wao namna ya kutengeneza pesa zaidi ya kuwakamua tu hasa kwa kile kidogo walicho nacho, kiukweli huwa inaniumiza sana. Pia unakuta mtu anashinda kanisani siku tano za wiki bila kufanya kazi na ukimuuliza kama kanisa linamlipa anasema hapana anafanya kazi ya Mungu, mtu kama huyu ataachaje kuwa maskini mnadhani.

mkuu hebu nisaidie na wewe maana kuna watu hapo juu hawataki kunielewa sijui ni kwa makusudi au la, dini ndio chanzo cha umasikini huo ndo ukweli, kwa sababu zinawafundisha watu kuwa wasihangaike na vya duniani bali wahangaike na vilivyo juu, kutothamini mali zilizo chini ya ardhi yaani madini na vingine na kuwa utajiri wote uliopo duniani hauhusiani na Mungu, tena mafundisho haya huwa yanakaziwa kweli kuthamini mali au utajiri ulioko duniani ni chukizo kwa Mungu. (lkn wao wana magari ya kifahari, nyumba, maisha mazuri, watoto wao wanasoma nje, wana ndege nk)

mafundisho ya aina hii ndio yameharibu watu, wengine wao ni wavivu wa kujishughulisha wakisubir siku wakifa wataenda kuishi maisha ya milele ambako huko ni kusifu na kuabudu tu, wengine hawataki kusoma wanadai dunia imeisha YESU yuko karibu kurudi kwa hiyo hataki kujisumbua kwa neno lolote, isipokuwa anataka kusali na kuomba tu akimsubiri YESU (ndo hao wanolala makanisani hawafanyi kazi)

binadamu anatakiwa elewe na kuamini moyoni mwake kuwa Mungu yupo, roho yake ni mali ya Mungu, isipokuwa mwili ni mavumbi ya ardhi, watoke wafanye kazi, waache kulala makanisani na misikitini Mungu hatumikiwi hivyo, watafute pesa wawasaidie wanohitaji msaada pale wanapojiweza, wahakikishe wanatenda mema maishani mwao, watende haki na waitetee haki, ahakikishe ana chukia na kuachana na mabaya yote, awapende binadamu wote bila ya kuwabagua nk, huko ndiko kumtumikia Mungu.
 
nadhani hujamuelewa huyo ndugu, ni kweli kuwa dini na Mungu ni vitu viwili tofauti ila dini ni njia ambayo wanadamu tumejiwekea ya kumfikia huyo Mungu ingawa sio lazima sana kwani kuna watu wanawasiliana na Mungu moja kwa moja bila kupitia dini
Nimemuuliza ni ujumbe gani ambao hao akina Musa Yesu na Muhammad walikuja nao? hajanitajia huo ujumbe.

Wala hajanitajia ni kipi cha kututhibitishia kuwa huo ujumbe ni kutoka kwa mungu,ajabu bado mnaendelea kuniambia kuwa kuna bado wanaendelea kupokea au kuwasiliana na mungu.

Ukiangalia dini zinaelekeza mfumo gani wa kuishi hapa duniani vile ambavyo mungu ameelekeza tuishi hivyo na huo ujumbe wa mungu unapitia njia hiyo, sasa mnachotaka kukieleza nyie mnashindwa kukiweka katika kuendana na uhalisia ili kilete maana.
 
mkuu Eiyer kabla ya afrika kuvamiwa na wakoloni afrika chini ya uongozi wa Mafarao, lilikuwa bara linoongoza kwa tekenolojia na maendeleo duniani, miili ya mafarao waliokufa miaka 3,000 iliyopita ilipakwa dawa ikazikwa haijaoza mpaka leo, maarifa haya leo hayakupo duniani na afrika wakati huo ilikuwa ikiongoza kwa sayansi na utawala bora ikiwa na taasisi nyingi za utafiti wa kisayansi ambazo dini za kigeni mujibu wa dini za kigeni wanaziita Mungu, afrika imewahi kutawala dunia kwa miaka isiyopungua 18,000 au zaidi, tangu hapo afrika lilikuwa bara tulivu kutokana na asili ya watu wake kuwa waungwana na watulivu, (watu weusi)Tawala za afrika zilikuwa tawala za kidemokrasia waatu wake walikuwa na uhuru wa kutoa mawazo yao mradi havunji sheria za nchi, waaafrika wana asili ya utu wema, upole, ni waungwana, wakarimu, hawana asili ya ubaguzi, kama wangelikuwa ni watu wabaguzi, Yusufu wasingempa kazi ya uwaziri mkuu wa nchi yao.

Mambo yalianza kubadilika baada ya Warumi kuchukua dola kutoka mikononi mwa wagiriki waarumi walianzisha utawala wa sheria, mfumo uliowafanya wawe maarufu na kupendwa sana duniani, kwawa bahati mbaya,watawala hawa walijisahau, wakajiingiza katika starehe naufisadi hapo ndipo sayansi, utawala bora na democrasia vikatoweka, badala yake starehe na ufisadi ikawa ndio dira ya watawala, watanashati, wakaasisi siku kuu nyingi za mapumziko kitaifa, siku kuu hizo zilisherehekewa kwa ngono na ufisadi, Moja wapo ya siku kuu za aina hiyo ilikuwa siku ya tarehe 25 Desemba, siku kuu hizo, nyingine zilipigwa marufuku nyingine kubadilishwa kama ile ya Tarehe 25 December ambayo ilibadilishwa ikawa siku kuu ya Chrismas siku ya kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu,

kupitia dini walitukandamiza wa afrika wakapanua dola yao kwa kisingizio kuwa wametumwa na Mungu, wazungu walikuwa watu wa kwanza kufika afrika kuleta dini, walitumia ulaghai mwingi kulaghai watu kuzisadikisha dini zao, waarabu nao walipoleta dini, walitumia ulaghai ule ule uliotumiwa na wazungu kusadikisha dini zao, pamoja na kutumia ulaghai mwingi, pia waarabu walitumia mabavu kusadikisha dini yao, yaani jihad, walifanya mauaji ya kikatili ya hali ya juu, mfano mzuri ni pale walipovamia afrika kaskazini, walichinja watu kama watu wanavyochinja kuku, waliwaona watu weusi kuwa nimashetani makafri hawatokani na Mungu, wakidai kuwa wao wametumwa na Mungu kuleta dini, huu ni ushenzi wa hali ya juu waliotufanyia hawa watu na dini zao,

Mkuu,

Tusaidie kidogo,
Tukitaja Afrika tunamaanisha nini na waafrika ni watu gani?
 
sina hakika km tunaweza kuelewana aiseee yaani dini imekuingia sana tatizo ndio sababu tunashindwa kuelewana
nishakwambia mara kadhaa dini sio Mungu,
Na nyie wengi mna tatizo la kuona mnaelewa sana,na huwa mnashindwa kuwaelewesha kuelewa hicho mnachoelwa matokeo yake mnaona watu sio waelewa kumbe tatizo ni nyie mnashindwa kuelewesha.

Kwa maelezo gani ya kina uliyoyaeleza ambao ulitaka mie nifikie kukubaliana na unachokieleza? au wewe unataka nikubali tu unachokieleza bila kukuhoji ili nielewe?
 
'Ukiijua kweli, nayo kweli itakuweka huru'. Entry point ya wazungu/waarabu kwa Afrika ilisaidiwa na kufanikishwa kupitia dini. tulipumbazwa na tunaendelea kupumbazwa kupitia dini tulizoletewa na kudharau na tunaendelea kudharau mila na tamaduni zetu ambapo tunatoa fursa kwa wageni kuendelea kunyonya mali zetu mpaka damu zetu. Afrika ndio asili ya ubinadamu (Binadamu wa kwanza aliishi Afrika). Ustaarabu na elimu vilianzia Afrika (falme za songai na mwanamtapa na uwepo wa piramids) ambapo kwa wakati huo nchi za ulaya hazikuwanavyo. Siraha (physical) haina madhara makubwa sana ukilinganisha na madhara yaletwayo na 'deception'(upotoshwaji wa kifkra). Kwa miaka zaidi 300,000 Afrika na waafrika tumelishwa uongo na tunaendelea kulishwa uongo na kuuamini na tunaelekea kupoteza mwelekeo ukilinganisha na jamiii zingine duniani na hii pamoja na mambo mengine inachangiwa na namna tunavyo practice dini tulizoletewa na wala sisemi eti Mungu hayupo Mungu yupo kwani waafrika walimjua hata kabla ya ukoloni.

Leo hii tunaaminishwa kwamba wayahudi waliopo pale Israel (akina Natanyahu) eti ndio wale wanaosemwa kwenye Biblia na kwamba eti Yesu alikuwa mzungu this is deception. Tufikirie kwa makini ni watu gani walipelekwa utumwani kwa miaka kede kede? na huko walikopelekwa wakafanyishwa kazi na nchi hizo zikainuka na kuwa mataifa makubwa je, ni wayahudi wa leo au ni waafrika?? Je, wakati wa utumwa pale misiri ni watu gani walikuwa watumwa???? wayahudi wa leo au waafrika"". Anwal Sadat raisi wa zamani wa misiri aliwakataa wayahudi wa leo kuikalia palestina akidai kwamba hawawezi kukaa pale kwani waliondoka misiri wakiwa watu 'weusi' na wamerudi wakiwa weupe (wazungu). Hitler wakati akitekeleza maangamizi kwa wayahudi alisema wao sio wale waliotamkwa ndani ya biblia bali waliotamkwa ni 'Niggroes'. Biblia inasema ' watachukuliwa utumwani na watatawanyika pande zote za dunia na itafika wakati watadai kurudi kwenye nchi ya ahadi na hapo watakaporudi amani itatamaraki. Swali la kujiuliza watu gani walichukuliwa utumwani na kutawanyika pande zote za dunia?? wayahudi au watu weusi?? kwa watu weusi angalia nchi kama marekeani, uingereza, ubeligiji, visiwa vya carribeani na baadhi ya visiwa vya asia na asia yenyewe. Je wayahudi wa leo baada ya kurudi kwenye nchi yao ya ahadi amani imetamaraki???? Leo tunaaminishwa kupitia dini zetu kwamba wayahudi wa leo wamebarikiwa na hakuna taifa lolote linaloweza kuwasumbua na kumbe tunasahau ukweli kwamba wale ni vipandikizi vya marekani na uwezo wao wote wanaitegemea marekani na marekani aliwapandikiza pale kupunguza threats kutoka nchi za kiaarabu. Wakristo kila siku tunaenda kuhiji kwa Natanyahu tukiamini kwamba ndio wateule kumbe tumelishwa uongo kwa miaka kede kede na uongo huo umegeuka kuwa ukweli.
fact[emoji106]
 
tatizo lililokuwepo watu wengi badala ya kuijadili dini yenyewe yaani kujadili maandiko wengi hujadili watu ya mzungu na mwanarabu,kwa mfano ndani ya qur an inasema msikubali kudhurumu wala kudhurumiwa,lipeni kisasi mtu akiuwa mke na nyinyi ueni mke wao,jicho kwa jicho na jino kwa jino,tuchukulie mzungu kaja kuchukua heka 1000 za wanakijiji kwa njia kwamba atajenga shule lakini eneo lililobaki akafanyia mambo yake mengine binafsi wanakijiji wakiamua kukataa na kuwatayari kwa lolote huyuhuyu mtu atawalaumu wanakijiji kwa kupinga maendeleo,watu wanafiki hivi hawa wanaopora madini yetu,tembo,na mambo mengine wamekuja na dini gani.richmond,escro,rada,ndege,vichwa vibovu vya treni walikuja na dini ipi?wacha unafiki na upotoshaji usio na msingi
hachana na hawa waliokuja jana au juzi,,sisi tunazungumzia wale waliokuja enzi za ukoloni na kuleta dini iliyowafanya babu zetu kuwa inferior/wanyonge mbele yao ili wawatawale na kuwanyonya kiraisi,,,kamwa huwezi nibadilisha mawazo kama"THE TRUE AND GENUINE WAY OF WORSHIP GOD IS ONLY THE TRADITIONAL WAY OF OUR ANCESTORS" ila hizi zingine zimeletwa na wapigaji tuu!!!
 
Nimemuuliza ni ujumbe gani ambao hao akina Musa Yesu na Muhammad walikuja nao? hajanitajia huo ujumbe.

Wala hajanitajia ni kipi cha kututhibitishia kuwa huo ujumbe ni kutoka kwa mungu,ajabu bado mnaendelea kuniambia kuwa kuna bado wanaendelea kupokea au kuwasiliana na mungu.

Ukiangalia dini zinaelekeza mfumo gani wa kuishi hapa duniani vile ambavyo mungu ameelekeza tuishi hivyo na huo ujumbe wa mungu unapitia njia hiyo, sasa mnachotaka kukieleza nyie mnashindwa kukiweka katika kuendana na uhalisia ili kilete maana.
Musa, Yesu na Mohamed ni watu, ni binadamu km ulivyo wewe, kila mmoja aliwakilisha mtazamo wa Mungu km anavyoufikiria yeye, ndio maana kunatofauti sana kati ya hawa watu,
uKRISTO unasema Yesu ndiye mwanzo na mwisho
Uisilamu unasema Msujudie Mungu na Mtume wake (Mohamed)
Musa msimamo wake ni wa Mungu mmoja na wala si Miungu mitatu,
mitazamo hii ya kibidamu si ya Ki Mungu

Mfumo wa maisha ya mwanadamu wa ki Mungu ni kupitia Sayansi, maana Science hushughulika na maendeleo ya watu walio hai, isipokuwa dini inahangaika na watu walio wafu,

katika kazi zote za ki sayansi, wana sayansi huwa wanaafikia na kuwa na msimamo mmoja katika mambo yao yote, lkn wana dini hawajawahi kukubaliana na wala haitakuja kutoa kukubalia ktk jambo lolote lile wanalodai kuwa ni la ki Mungu
 
Mkuu,

Tusaidie kidogo,
Tukitaja Afrika tunamaanisha nini na waafrika ni watu gani?
Afrika ni neno la Kilatini, lenye maana ya mtu alyeungua MWEUSI, hivyo inapotamkwa/kutajwa Waafrika ina maanisha ni mtu/watu weusi
 
Musa, Yesu na Mohamed ni watu, ni binadamu km ulivyo wewe, kila mmoja aliwakilisha mtazamo wa Mungu km anavyoufikiria yeye, ndio maana kunatofauti sana kati ya hawa watu,
uKRISTO unasema Yesu ndiye mwanzo na mwisho
Uisilamu unasema Msujudie Mungu na Mtume wake (Mohamed)
Musa msimamo wake ni wa Mungu mmoja na wala si Miungu mitatu,
mitazamo hii ya kibidamu si ya Ki Mungu

Mfumo wa maisha ya mwanadamu wa ki Mungu ni kupitia Sayansi, maana Science hushughulika na maendeleo ya watu walio hai, isipokuwa dini inahangaika na watu walio wafu,

katika kazi zote za ki sayansi, wana sayansi huwa wanaafikia na kuwa na msimamo mmoja katika mambo yao yote, lkn wana dini hawajawahi kukubaliana na wala haitakuja kutoa kukubalia ktk jambo lolote lile wanalodai kuwa ni la ki Mungu
Duh! haya twende hivyo hivyo.

Ulisema mwenyewe kuwa akina Musa Yesu na Muhammad walikuwa wanaleta ujumbe kutoka kwa mungu na walipewa karma na ukawataja hadi akina Nyerere. Sasa ndiyo maana nikauliza huo ujumbe ni upi waliyokuja nao kutoka kwa mungu? Unakataa tena kwa kusema waliyokuwa wakiyafundisha ni mitizamo yao haikuwa ya mungu,ina maana Musa Yesu na Muhammad hawakuwa na ujumbe kutoka kwa mungu.

Mkuu kwa contradictions hizi bado tu naonekana mie ndiyo sio muelewa?
 
Wale walishakuwa addicted na dini.
Hawaoni wala kusikia lolote pindi dini inapozungumzwa.
Dini ni kama opium vile.

Such kind of people might have been through hell n the church could have been their only support and so they decide to stand firm even if under manipulation
 
habari ya hapa,

Ni lini mtu mweusi alipata kiongozi anayeitwa faraoh?
Farao kilikuwa ni cheo cha watawala wa Afrika na Afrika imepata kutawaliwa na watawala wengi (Mafarao)
wewe wamtaka Farao gani? maana Mafarao wote walikuwa ni watu weusi
 
Duh! haya twende hivyo hivyo.

Ulisema mwenyewe kuwa akina Musa Yesu na Muhammad walikuwa wanaleta ujumbe kutoka kwa mungu na walipewa karma na ukawataja hadi akina Nyerere. Sasa ndiyo maana nikauliza huo ujumbe ni upi waliyokuja nao kutoka kwa mungu? Unakataa tena kwa kusema waliyokuwa wakiyafundisha ni mitizamo yao haikuwa ya mungu,ina maana Musa Yesu na Muhammad hawakuwa na ujumbe kutoka kwa mungu.

Mkuu kwa contradictions hizi bado tu naonekana mie ndiyo sio muelewa?
Mawazo ya kutenda Mema hutokana na Mungu, kupitia Ubongo wa Binadamu, kwa maana hiyo mtenda mema yeyote hutokana na Mungu Si Nyerere, Yesu, Muhamed, Musa nk, wako wengi tu
 
Dini alianza mashariki ya kati na kuhubiriwa Ulaya. halafu Africa na latin America zimekuja kwa njia ya ukokoloni. Sasa ubaya wake ni nini?wakoloni hawakuleta dini tuu, bali walileta elimu na hospitali ili kukusaidia wewe na mimi kupata maarifa. dini imepunguza sana imani za kichawi na watu kuchukizana kwa sababu ya imani za uchawi. elimu imetuletea wajenzi wa nchi na hospitali zimerefusha maisha yetu. sasa huo ubaya wa mkoloni upo wapi? wewe unajua kabla kuja mwa mkoloni adha ya kung'oa jino ilivyokuwa?Heshima kwenu mabibi na mabwana ni imani yangu kuwa hamjambo, poleni na heka heka za maisha

Km kichwa cha habari kinachojieleza hapo juu, nimeona leo nitoe dukuduku langu kuhusiana na hizi dini zilivyo tushika, na kweli tumeshikika na wametuweza na wamefanikiwa sana katika hili, na sisi pasi na kujiuliza tulikubali kuzipokea tukapumbazika, tukawaacha wakawekeza dini zao km vitega uchumi, haikutosha ili kutumaliza kabisa wakadai kuwa, dini zote za watu weusi, zikiwapo mila, desturi na tamaduni zao zote ni zamashetani.

Ndio maana adui wa maradhi, ujinga na umasikini ametuganda kwa sababu akili zetu zimedumaa, tunaendeshwa km gari bovu, hii ni kwasababu tumekubali kuwa vibaraka wa kupigania dini za watu, kupitia dini wametugawa vipande vipande, hawa watu waliotuletea dini wanadai kuwa wao ni mitume na manabii wa Mungu, shetani kwa mujibu wadini zao wanadai kuwa ana sura na maumbile mabaya eti ana mikia mingi mwenye rangi nyeusi km mwaafrika, huu ni upuuzi kabisa.

Tupo hivi tulivyo kwa sababu tuliacha mila, desturi na tamaduni zetu badala yake tukaamua kukumbatia mila na desturi za wengine. Kupitia tamaduni zao wanatudharau sasa kwa kusema kuwa mila, tamaduni na desturi zetu nitatokana na mashetani. Kwa mujibu wa dini hizi wanadai kuwa hapajawahi wala kupata kutokea kwa malaika mweusi tangu kuwapo kwa dunia,


Binafsi huwa nasema na nasema tena dini ni ujinga, tufundishwa ujinga na tumeamini ujinga na huenda waliamua kuletea dini kwa sababu kuna kifo na pengine kifo kisingekuwepo kusingekuwa na kitu dini, hebu tuache kudharauliana na kutengana sisi kwa sisi kwa sababu tu wewe wazijua mila za kiarabu na wewe wazijua mila za kizungu, turudi kwenye asili yetu, hizi dini za kiyahudi na kiarabu hazitatufikisha popote zaidi ya kuendelea kutufanya wajinga.
 
Mawazo ya kutenda Mema hutokana na Mungu, kupitia Ubongo wa Binadamu, kwa maana hiyo mtenda mema yeyote hutokana na Mungu Si Nyerere, Yesu, Muhamed, Musa nk, wako wengi tu
Musa Yesu na Muhammad ujumbe wao kutoka kwa mungu ulikuwa ni upi?
 
Back
Top Bottom