Wakristo, Hivi andiko gani limesema maiti azikwe akiwa kwenye Jeneza?

Wakristo, Hivi andiko gani limesema maiti azikwe akiwa kwenye Jeneza?

Mazishi ya Kikristo yanavyokuwa.
Wakristo wote tunafahamu kuwa muongozo wetu ni Biblia,Hivyo kila tunalolifanya linatakiwa kuongozwa na Biblia neno la Mungu,Imani yetu imejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii naye Kristo ni jiwe kuu la Pembeni (Efeso 2;20). Hivyo tunajifunza kutoka kwao Maandiko hayatufundishi popote kuwa Walipokufa mitume walikamuliwa kama wafanyavyo waislamu mfano Ibrahimu alipokufa hatusomi kuwa alikamuliwa(Mwanzo 25;7),Isaka na yakobo pia walikufa na kuzikwa bila kukamuliwa (Mwanzo 49;32,50;1-6). Ni muhimu waislamu kutuambia kuwa maswala ya kukamuana wanajifunza kwa nani? Maana quran imeagiza wajifunze kutoka kwa Wakristo na wayahudi kama wana shaka katika jambo lolote {Surat Yunusi (Yona) 10;94)}
Kwa nini Wakristo tunazika na Sanduku?

Swala la kuzika na sanduku limekuwa likiwakera sana na kuwachanganya waislamu wamekuwa wakihoji kuwa wakristo wamejifunza wapi Tabia ya kuzika na sanduku?wakati mwingine wanafikiri tunaigiza utamaduni wa kizungu,kwa kawaida Wakristo hatufanyi mambo kinyume na maandiko yanavyo tufundisha soma (Mwanzo 50;24).

“..Yusufu akawaambia nduguze,Mimi nitakufa,Mungu atawajia ninyi bila shaka atawapandisha kutoka nchi hii mpaka nchi aliyowaapia Ibrahimu;na Isaka na Yakobo,Yusufu akawaapisha wana wa Israel akasema bila shaka Mungu atawajia ninyi nanyi mtapandisha huko mifupa yangu.Basi Yusufu akafa,mwenye miaka mia na kumi,WAKAMPAKA DAWA WAKAMTIA KATIKA SANDUKU HUKO MISRI.”
 
Naomba muongozo.... kwanini maiti mnawaweka kwenye Jeneza ... ?View attachment 2595171
Huu ni ustaarabu tu. Binadamu ni mnyama mwenye ustaarabu na pia tunatumia vilivyotuzunguka katika kutekeleza ustaarabu huo. Miili yetu baada ya kufa bado huitaji ustaarabu wa kuzika na ndio maana utaona maiti inaoshwa na kuvishwa vizuri. Kuna wanaozika kwa kufukia kujengea kuna wanaokausha na kuiifadhi ndani kwa muda.
 
Mungu ametupa utashi sio kila jambo limeandikwa, maana yake ni kwamba tuzike kwenye jeneza au sanda tu haitamake any difference.
Ukisema utumie utashi wako maana Yale dini yako haijakamilika kwny unaiongezea nyama .Hiyo ndio huwa tunaiita bagosha Bangladesh!
 
Mimi ni mfuasi wa Kristo kama alivyosema Mtume Paulo kwenye 1Wakorintho 11: 1

Suala la kuzika kwa jeneza tumerithi kutoka kwa Warumi ambao waliliokota kutoka kwa Misri ya kale.

Kimsingi halipo kwenye maandiko


24 Yusufu akawaambia nduguze, Mimi ninakufa, lakini Mungu atawajia ninyi bila shaka, atawapandisha toka nchi hii, mpaka nchi aliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.
Mwanzo 50:24

25 Yusufu akawaapisha wana wa Israeli, akasema, Bila shaka Mungu atawajia ninyi, nanyi mtaipandisha huko mifupa yangu.
Mwanzo 50:25

26 Basi Yusufu akafa, mwenye miaka mia na kumi; wakampaka dawa, wakamtia katika sanduku, huko Misri.
Mwanzo 50:26
 
sawa. Jeneza ni biashara hakuna cha utaratibu kaka
Waza umemvika mpendwa wako nguo ya gharama kisha unamfukia na tope lenye majimaji. Utajisikiaje? Hapo ndio suala la jeneza linapokuja. Halafu uchumi mzuri huchochea yote hayo uwezi ishi jangwani ukawaza jeneza 😂😂😂
 
Back
Top Bottom