Rafiki yangu(37) ni single father with 3 kids, ana mchumba wake mganda ambaye naye ni single mother(37 yrs) with one kid. Alikuwa rafiki yake wakati wakisoma chuo, wakaja kukutana tena miaka kadhaa baada ya ku graduate, jamaa anaishi Dar, mrembo anaishi Kampala wakaanzisha uhusiano.
Umekusudia kuutukana ukristo? Ona hoja zako mfu hapa ambazo zinaonyesha jinsi gani unaleta hadithi za kutunga zisizo na mashiko:
1. Rafiki yako single father watoto watatu. Mama wa watoto hao watatu yuko wapi?
2. Single mother mtoto mmoja, baba wa mtoto yuko wapi?
3. Walikuwa marafiki chuoni (wapenzi)? Wapi Ukristo unaruhusu uchafu huo?
Muda wa kwenda kutoa mahari ulikuwa mwezi uliopita. Nilikuwa mmoja katika ujumbe uliyoongozana na rafiki yangu na matchmaker(mshenga) wake. Wakati wa kunegotiate mahari wazazi wakaanza na 15 million Ugandan ambayo ni kama milioni 9 ya Tanzania(walitaja idadi ya ng'ombe then ikawa converted to cash).
Tukakomaa wakashusha mpaka milioni kumi ya Uganda. Tutakomaa tana wakashusha mpaka milioni tano ya Uganda. Mwisho kabisa wakakomea shilingi milioni nne na point kadhaa ya Uganda ambayo ni sawa na milioni tatu ya Tanzania.
Hapo wakasema haipungui hata mia. Tukaomba tupewe muda tukatafakari kisha tutatoa taarifa ni lini tutarejea tena ukweni kukamilisha hiyo mahari. Kumbuka hapo tumefikia hotelini. Basi tulipoenda kujadiliana tukamuuliza muoaji kama bajeti yake ina mruhusu kulipa milioni tatu cash akasema no way out hawezi kulipa mahari yote hiyo.
4. Hilo suala la mahari ya waganda lina uhusiano gani na Ukristo? Ni wapi kuna maelekezo ya kudai kiwango fulani cha mahari? Hoja za kipuuzi kweli kweli.
5. Huyo muoaji alitakiwa kusikitikia bajeti yake, kwamba amevamia mila za watu bila mwongozo sahihi. Muache kukurupuka, mambo haya hufanywa kwa utaratibu.
Akasema alitegemea wangesema milioni moja halafu yeye angetoa laki tano au saba huku akitoa ahadi ya kumalizia mahari iliyo baki(waganda hakunaga kubakiza mahari).
6. Akasema alitegemea watasema.... Kwani mlikwenda kupeleka posa mpangiwe mahari au mlikwenda kuwaeleza kile mlichokuwa tayari kulipa? After all mahari ya MWANAMKE tena mwenye mtoto haiwezi kuwa hicho ulichosema, ni uongo dhahiri. Mengine tuwaachie waganda na mila zao, sasa Ukristo unaingiaje hapo ewe usiye ufahamu?
Wakati hapa Tz kutokumalizia mahari ni heshima kubwa sana kwa wakwe, kwasababu kwanza, inaonyesha kwamba bibi harusi sio bidhaa unayo weza kuinunua dukani na kwamba wazazi wa bibi harusi wamekutunuku binti yao ukaanzishe nae familia. Lakini pili Inaonyesha kwamba wewe muoaji unampenda sana mkeo kiasi kwamba haupo tayari kusubiri mpaka upate mahari kamili.
7. Nilitegemea utasema "WAKATI KATIKA UISLAMU KUTOMALIZA MAHARI NI HESHIMA KUBWA.... " Kumbe umejichanganya mwenyewe, unadai Tanzania ni heshima kutomaliza mahari, kwani Tanzania ni ya Waislamu na Uganda ni ya Wakristo? Una matatizo ya logic kwenye hoja zako.
Mshenga akamuuliza bwana harusi. Hauna alternative mahali kwingine, yaani hauna mchumba mwingine?
Jamaa akajibu nina mchumba mwingine yupo Tanzania ila yeye ni muislamu na kwao wanataka tufunge ndoa ya kiislamu(mshenga akajibu nilitaka kushangaa unakosaje alternative?!).
8. Sasa huyo mtu wenu alikuwa muoaji kweli au ni mhuni tu? Pia ninyi wasindikizaji feki ni genge la malaya tu, eti mngeshangaa kama hana alternative!? You're fake!!
9. Ok, kwa akili yako ukaona ni wakati sahihi kutuingizia character wako muislamu kwenye utunzi wako. Eti kwao wanataka ndoa ya Kiislamu, hapa unamaanisha ndoa za Kiislamu hazina mahari?
Kisha akamuuliza. Upo tayari kufunga ndoa ya kiislamu? Jamaa akajibu yupo tayari. Mshenga akajibu tunasubiri nini? Mshenga akaenda kutoa taarifa ukweni kwamba tunarudi Dar kujipanga na tutarejea tutakapo kuwa tayari.
10. Mwanamume aliye tayari kwa ndoa, amekwisha kujichagulia mchumba hawezi kamwe kubadili gia angani sekunde moja baadaye kutaka mwanamke mwingine. Hii ni dhahiri huyu hakuwa muoaji, ama utunzi umepwaya.
Jamaa karudi Dar ndani ya hizo wiki mbili kavuta jiko na harusi ikafanyika kwa gharama ya kawaida sana, na mtoto mwenyewe mbichi kabisa ndiyo kwanza kamaliza form four(anaweza kuwa bado hajawa dis flowered).
11. Form four, anaweza kuwa bikira. Kamaliza shule gani huyo? Huyu jamaa yako alidai anaye mchumba mwingine, alimposa lini? Kwa hiyo alikuwa na wanawake wawili akisubiri mwenye unafuu wa mahari? Baada ya kufeli kwa mwanamke wa kwanza akahamia kwa wa pili, huyu jamaa hakuwa na mpango wa kuoa licha ya sifa feki ulizommwagia. Genge la wahuni tu.
Baada ya kuoa jamaa kamjulisha mchumba wake wa uganda kwamba hayupo tena interested na ndoa kwa sababu hizo gharama haziwezi na kwamba ameamua kuoa sehemu nyingine. Mwanamke wa kiganda kachanganyikiwa sasa hivi anawalaumu wazazi wake tu.
12. Mwanamke wa Kiganda ama wa kikristo aliyechanganyikiwa? Umeshutumu ukristo kwa mila za Kiganda?
Wakristo hizo zama za wanaume kutoa mahari za mamilioni hazipo tena. Jifunzeni kwa waislamu, mnawakosesha binti zenu ndoa kwa sababu ambazo hazina msingi. Kwanza karne hii ukiona mtu "amepandwa na kichaa " cha kutaka kuoa unapaswa kumpa mke haraka kabla kichaa hakija toweka, ili kichaa kiondoke tayari akiwa na mke ndani ndiyo akumbuke 'kumbe mimi fala hivi'.
12. Sasa hapo kwenye hitimisho la upuuzi huu unajazia "ukristo" wakati kwenye andiko lako umebainisha utofauti wa ndoa za Kiganda na za Kitanzania, hivi kichwa chako kinawaza sawa sawa? Hakuna hata sehemu moja umeonyesha uhusika wa viongozi wa kikristo kwenye mchakato wa mahari. Sasa ukristo ujifunze nini kwenye Uislamu?
13. Tofauti ya ndoa za kikristo na nyinginezo ni mchana na usiku. Kwa mfano ndoa nyinginezo (ikiwemo uislamu) ni mikataba ambayo yaweza kuvunjwa wakati wowote lakini ndoa za kikristo ni AGANO LA MAISHA. Hili huvunjika pale tu upande mmoja unapokufa.
14. Mahari ni utamaduni wa kibiblia ambao huashiria nia njema ya muoaji. Pia ni shukrani kwa mzazi kwa malezi bora kwa binti yake. Maandiko hayaweki kiwango cha mahari stahiki, hilo limeachwa kwa jamii husika. Kuutuhumu ukristo kisa mlishindwa kulipa mahari ya Kiganda ni upotofu wa fikra. Yakobo alitumika miaka 14 ili kumpata mkewe aliyempenda sana, sasa huyo jamaa yako safari moja tu ya Uganda imeanzisha mada 'JF. Badala ya kurudi na kupanga hoja ili mwishowe ampate yule ampendaye eti akaona aoe muislamu! Kizazi cha hovyo kweli kweli.
NB: Kwa sababu ya complications zake, familia nyingi za kikristo huwa zina experience ndoa chache sana ikilinganishwa na familia za kiislamu. Dini ya kiislamu imerahisisha sana suala la ndoa. Matokeo yake familia nyingi za kikristo huwa hazifahamu saikolojia siasa za waoaji.
15. Ukusudia wanawake wengi wasio na ndoa duniani ni Wakristo? Kwa utafiti upi? Huu nao ni upuuzi mkubwa. Unataka kumaanisha hata wanaume wa kikristo hupendelea kuoa wanawake wa Kiislamu? Hello, jaribu tena. Wewe si mtunzi mzuri.
Ni hivi muoaji anapo kuja kwenye familia yako, usifikiri hajaona mwanamke mwingine au hana option nyingine. Most of the time muoaji anapofikia hatua ya kuja kujitambulisha nyumbani kwenu tayari anakuwa na option zingine kama mbili, tatu au hata nne.
Kama hujaoa nakushauri usithubutu kwani hujajua ndoa ni nini. Huo ushauri wako ni wa kijinga kabisa, kama sababu za binti kukubali kuolewa ndio hizi, basi hakuna haja ya kuolewa!! Mtu anayekuja akiwa na 'option' mbili au tatu sio mwoaji, ni malaya kama malaya wengine tu. Tofauti ni kwamba huyu ameamua kuhalalisha umalaya wake kwa kumweka ndani binti wa watu huku moyo wake ukitangatanga hovyo.
Nikija kwenye familia yako kuchumbia, halafu ukaniletea complications ngumu, mimi nitakacho kifanya nita kuachia binti yako nitaenda kwenye familia ambayo haitaniwekea complications ngumu.
Ninapokuja kwenye familia yako usinichukulie kwanza kama mtu ambae ninataka kumuoa binti yako, nichukulie kama mtu ambae nimekuja kutazama kama familia yako ina complications au la!
Mwanamume anapohangaika kumpata mke ni dalili ya upendo kwake na mara nyingi ndoa za aina hiyo hudumu. Kwa familia yenye maadili kuoa sio hisani kwamba unaisaidia familia. Wewe na huyo jamaa yako bado mna safari ndefu ya kujifunza maana na maisha ya ndoa. Pole sana.