Wakristo mjitafakari kwenye suala la mahari, mnawakosea sana binti zenu. Kilichotokea hivi karibuni kwa jamaa yangu kina funzo

Wakristo mjitafakari kwenye suala la mahari, mnawakosea sana binti zenu. Kilichotokea hivi karibuni kwa jamaa yangu kina funzo

Rafiki yangu(37) ni single father with 3 kids, ana mchumba wake mganda ambaye naye ni single mother(37 yrs) with one kid. Alikuwa rafiki yake wakati wakisoma chuo, wakaja kukutana tena miaka kadhaa baada ya ku graduate, jamaa anaishi Dar, mrembo anaishi Kampala wakaanzisha uhusiano.

Muda wa kwenda kutoa mahari ulikuwa mwezi uliopita. Nilikuwa mmoja katika ujumbe uliyoongozana na rafiki yangu na matchmaker(mshenga) wake. Wakati wa kunegotiate mahari wazazi wakaanza na 15 million Ugandan ambayo ni kama milioni 9 ya Tanzania(walitaja idadi ya ng'ombe then ikawa converted to cash).

Tukakomaa wakashusha mpaka milioni kumi ya Uganda. Tutakomaa tana wakashusha mpaka milioni tano ya Uganda. Mwisho kabisa wakakomea shilingi milioni nne na point kadhaa ya Uganda ambayo ni sawa na milioni tatu ya Tanzania.

Hapo wakasema haipungui hata mia. Tukaomba tupewe muda tukatafakari kisha tutatoa taarifa ni lini tutarejea tena ukweni kukamilisha hiyo mahari. Kumbuka hapo tumefikia hotelini. Basi tulipoenda kujadiliana tukamuuliza muoaji kama bajeti yake ina mruhusu kulipa milioni tatu cash akasema no way out hawezi kulipa mahari yote hiyo.

Akasema alitegemea wangesema milioni moja halafu yeye angetoa laki tano au saba huku akitoa ahadi ya kumalizia mahari iliyo baki(waganda hakunaga kubakiza mahari). Wakati hapa Tz kutokumalizia mahari ni heshima kubwa sana kwa wakwe, kwasababu kwanza, inaonyesha kwamba bibi harusi sio bidhaa unayo weza kuinunua dukani na kwamba wazazi wa bibi harusi wamekutunuku binti yao ukaanzishe nae familia. Lakini pili Inaonyesha kwamba wewe muoaji unampenda sana mkeo kiasi kwamba haupo tayari kusubiri mpaka upate mahari kamili.

Mshenga akamuuliza bwana harusi. Hauna alternative mahali kwingine, yaani hauna mchumba mwingine?
Jamaa akajibu nina mchumba mwingine yupo Tanzania ila yeye ni muislamu na kwao wanataka tufunge ndoa ya kiislamu(mshenga akajibu nilitaka kushangaa unakosaje alternative?!).

Kisha akamuuliza. Upo tayari kufunga ndoa ya kiislamu? Jamaa akajibu yupo tayari. Mshenga akajibu tunasubiri nini? Mshenga akaenda kutoa taarifa ukweni kwamba tunarudi Dar kujipanga na tutarejea tutakapo kuwa tayari.

Jamaa karudi Dar ndani ya hizo wiki mbili kavuta jiko na harusi ikafanyika kwa gharama ya kawaida sana, na mtoto mwenyewe mbichi kabisa ndiyo kwanza kamaliza form four(anaweza kuwa bado hajawa dis flowered).

Baada ya kuoa jamaa kamjulisha mchumba wake wa uganda kwamba hayupo tena interested na ndoa kwa sababu hizo gharama haziwezi na kwamba ameamua kuoa sehemu nyingine. Mwanamke wa kiganda kachanganyikiwa sasa hivi anawalaumu wazazi wake tu.

Wakristo hizo zama za wanaume kutoa mahari za mamilioni hazipo tena. Jifunzeni kwa waislamu, mnawakosesha binti zenu ndoa kwa sababu ambazo hazina msingi. Kwanza karne hii ukiona mtu "amepandwa na kichaa " cha kutaka kuoa unapaswa kumpa mke haraka kabla kichaa hakija toweka, ili kichaa kiondoke tayari akiwa na mke ndani ndiyo akumbuke 'kumbe mimi fala hivi'.

NB: Kwa sababu ya complications zake, familia nyingi za kikristo huwa zina experience ndoa chache sana ikilinganishwa na familia za kiislamu. Dini ya kiislamu imerahisisha sana suala la ndoa. Matokeo yake familia nyingi za kikristo huwa hazifahamu saikolojia siasa za waoaji.

Ni hivi muoaji anapo kuja kwenye familia yako, usifikiri hajaona mwanamke mwingine au hana option nyingine. Most of the time muoaji anapofikia hatua ya kuja kujitambulisha nyumbani kwenu tayari anakuwa na option zingine kama mbili, tatu au hata nne.

Nikija kwenye familia yako kuchumbia, halafu ukaniletea complications ngumu, mimi nitakacho kifanya nita kuachia binti yako nitaenda kwenye familia ambayo haitaniwekea complications ngumu.

Ninapokuja kwenye familia yako usinichukulie kwanza kama mtu ambae ninataka kumuoa binti yako, nichukulie kama mtu ambae nimekuja kutazama kama familia yako ina complications au la!
Maongezi yako yote mie Nina jicho moja kuwa una nia ya ku impart fear kwa watu hao uliowaongelea.

Yaani fear ndio inayo tufanya tuishi maisha yetu na Wala sio lingine huwa tunachagua the safest way and not unfamiliar way to pass through.


So don't impart fear mkuu
 
Kwanza karne hii ukiona mtu "amepandwa na kichaa " cha kutaka kuoa unapaswa kumpa mke haraka kabla kichaa hakija toweka, ili kichaa kiondoke tayari akiwa na mke ndani ndiyo akumbuke 'kumbe mimi fala hivi'.
Nakaziaa hapa mkuu naona km palikua pamelegea hivi 🤫
 
Ninapokuja kwenye familia yako usinichukulie kwanza kama mtu ambae ninataka kumuoa binti yako, nichukulie kama mtu ambae nimekuja kutazama kama familia yako ina complications au la!
Nakazia mkuu 😊
 
Mkuu mfano wewe umeenda kuoa wazazi wa Binti wakataja mahari utafanya nini?
Utaanza kuwapiga darasa au ili wasikutoze sababu ni iumdunisha mwanamke?
Issue ya mahari ipo kitamaduni zaidi sidhani kama inahusiana na kuuzwa au kudunishwa kwa mwanamke.
Mimi siendi kuoa kwa wajima.

Mahari inaondoa utu wa mwanamke na kumfanya awe bidhaa inayonunuliwa kwa bei fulani.
 
Mimi siendi kuoa kwa wajima.
Wajima tena mkuu?
Nilidhani utajibu hata kwa imagination kwamba umefika kwa wakwe wanataka mpunga ungefanyeje? Jibu usaidie hata watakaokutwa na kadhia za hao wajima.
 
Ni mtazamo tu

Hamuoni kama humu watu mna double standards. Kwa mfano; kuna watu mnalalamikia dini ya Kikristo kuhusu mambo ya mahari, au eti ukristo una mambo mengi...ok sawa. Lakini ni ukristo (neno la Mungu) unaosema mwanamke amtii mumewe...mwanamke asipotii kutwa mnafoka hakuna mfano kwamba haheshimu maandiko. Hamuoni mnakuwa mna double standard??

Afu ukute hata kupenda mlikoagizwa hampendi..tena ni biblia hiyohiyo ilioagiza wanaume kumpa mke heshima kama chombo kisicho na nguvu ili kuomba kusizuiliwe haya haya hamyatimizi lakini mnashadadiaga utii utii utii na mengine hamyashiki. Kama vipi tushike yote...ni Kristo aliekataza uzinzi kwaiyo michepuko ni kuzini tu vilevile. Wewe unazini afu mke asipomutii au kukuheshimu unasimamia maandiko kiaje yani??
 
Wajima tena mkuu?
Nilidhani utajibu hata kwa imagination kwamba umefika kwa wakwe wanataka mpunga ungefanyeje? Jibu usaidie hata watakaokutwa na kadhia za hao wajima.
Mtu anayeshindwa kulipa mahari, au anayelalamika kupangiwa mahari kubwa baada ya kufika kwa wazazi ni mjinga.

Kwa sababu, hizi habari zote alitakiwa kuweza kuzipata kabla ya kwenda huko, kwa upelelezi wake.

Na mimi nakwambia, kabla ya kwenda huko nitajua kama wataweza kuelewa msimamo wangu wa kupinga mahari ama vipi.

Kama wanaendekeza tamaduni za kijima zinazomdhalilisha mwanamke kama mahari, hata hiyo ndoa haiwezi kufana na kudumu.

Kwa sababu ndoa itaunganisha familia, na mimi sitaki kuendeleza ujima kwenye familia yangu.

Ndiyo maana nikakwambia siwezi kuoa kijima.

Lakini watu tupo tofauti sana, inawezekana kabisa usinielewe.

Nikawa kama ngamia ninayemuandikia samaki habari za jangwa lisilo na maji, samaki akasoma akawa haelewi inawezekana vipi kukawa na sehemu haina maji kabisa.
 
Ila hapa nimejifunza jambo moja, lazima kidume uwe na backup plan all the time. Kutegemea mwanamke mmoja itakula kwako.

Kelsea na sophy27 nawashauri pamoja na hao matajiri wenu mliokuwa nao ni vyema mkamuweka mzabzab kama backup plan 🤣🤣🤣🤣🤣
😂😂😂Ilo ndo uliloliona pekee Uzi wote huu 😂
 
Hivi wakristo mahali wanapanga wazazi au anaeolewa ndo anataja mahari??
 
😂😂😂Ilo ndo uliloliona pekee Uzi wote huu 😂
Wee kiwa nanbackup plan ndugu yangu, hawa wanaume ni mashetani kama mlivyo mashetani nyie wanawake. Unabwagwa siku yoyote🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kuna wengine mtadai tamaduni ok fine. Tamaduni za kiafrica labda zinaruhusu wanawake wengi. Lakini tamaduni zinataka wanawake watolewe mahari hakuna kuolewa bure. Kama unaenda na tamaduni all the way fanya kama zinavyodai. Kama una a lot of wives wahudumie sawa.

Huku ukitoa gari na huku toa gari. Huku wakila kuku na huku wale kuku. Mnasema tamaduni na hata wengne hamzijui. Tamaduni na mila za Africa zinakutaka ukalime wake watulie ndani wapendeze si wanakulelea watoto bwana.

Tamaduni hazitaki mtoto wa kike asome we kwanini unawasomesha?? Why waste your money. Ukishikilia jambo lielewe ili ulishike kwelikweli.

Ni mtazamo tu
 
Na kuachana ni cheap sana kwenye uislamu

Ukristo expensive na kuachana hakupo
Wanaachana sana tu na sikuhiz wanaoa km kawaida na nishahudia watu wamefunga ndoa kanisani zaidi ya maramoja na Bado wenzawao wapo hai
 
Rafiki yangu(37) ni single father with 3 kids, ana mchumba wake mganda ambaye naye ni single mother(37 yrs) with one kid. Alikuwa rafiki yake wakati wakisoma chuo, wakaja kukutana tena miaka kadhaa baada ya ku graduate, jamaa anaishi Dar, mrembo anaishi Kampala wakaanzisha uhusiano.

Muda wa kwenda kutoa mahari ulikuwa mwezi uliopita. Nilikuwa mmoja katika ujumbe uliyoongozana na rafiki yangu na matchmaker(mshenga) wake. Wakati wa kunegotiate mahari wazazi wakaanza na 15 million Ugandan ambayo ni kama milioni 9 ya Tanzania(walitaja idadi ya ng'ombe then ikawa converted to cash).

Tukakomaa wakashusha mpaka milioni kumi ya Uganda. Tutakomaa tana wakashusha mpaka milioni tano ya Uganda. Mwisho kabisa wakakomea shilingi milioni nne na point kadhaa ya Uganda ambayo ni sawa na milioni tatu ya Tanzania.

Hapo wakasema haipungui hata mia. Tukaomba tupewe muda tukatafakari kisha tutatoa taarifa ni lini tutarejea tena ukweni kukamilisha hiyo mahari. Kumbuka hapo tumefikia hotelini. Basi tulipoenda kujadiliana tukamuuliza muoaji kama bajeti yake ina mruhusu kulipa milioni tatu cash akasema no way out hawezi kulipa mahari yote hiyo.

Akasema alitegemea wangesema milioni moja halafu yeye angetoa laki tano au saba huku akitoa ahadi ya kumalizia mahari iliyo baki(waganda hakunaga kubakiza mahari). Wakati hapa Tz kutokumalizia mahari ni heshima kubwa sana kwa wakwe, kwasababu kwanza, inaonyesha kwamba bibi harusi sio bidhaa unayo weza kuinunua dukani na kwamba wazazi wa bibi harusi wamekutunuku binti yao ukaanzishe nae familia. Lakini pili Inaonyesha kwamba wewe muoaji unampenda sana mkeo kiasi kwamba haupo tayari kusubiri mpaka upate mahari kamili.

Mshenga akamuuliza bwana harusi. Hauna alternative mahali kwingine, yaani hauna mchumba mwingine?
Jamaa akajibu nina mchumba mwingine yupo Tanzania ila yeye ni muislamu na kwao wanataka tufunge ndoa ya kiislamu(mshenga akajibu nilitaka kushangaa unakosaje alternative?!).

Kisha akamuuliza. Upo tayari kufunga ndoa ya kiislamu? Jamaa akajibu yupo tayari. Mshenga akajibu tunasubiri nini? Mshenga akaenda kutoa taarifa ukweni kwamba tunarudi Dar kujipanga na tutarejea tutakapo kuwa tayari.

Jamaa karudi Dar ndani ya hizo wiki mbili kavuta jiko na harusi ikafanyika kwa gharama ya kawaida sana, na mtoto mwenyewe mbichi kabisa ndiyo kwanza kamaliza form four(anaweza kuwa bado hajawa dis flowered).

Baada ya kuoa jamaa kamjulisha mchumba wake wa uganda kwamba hayupo tena interested na ndoa kwa sababu hizo gharama haziwezi na kwamba ameamua kuoa sehemu nyingine. Mwanamke wa kiganda kachanganyikiwa sasa hivi anawalaumu wazazi wake tu.

Wakristo hizo zama za wanaume kutoa mahari za mamilioni hazipo tena. Jifunzeni kwa waislamu, mnawakosesha binti zenu ndoa kwa sababu ambazo hazina msingi. Kwanza karne hii ukiona mtu "amepandwa na kichaa " cha kutaka kuoa unapaswa kumpa mke haraka kabla kichaa hakija toweka, ili kichaa kiondoke tayari akiwa na mke ndani ndiyo akumbuke 'kumbe mimi fala hivi'.

NB: Kwa sababu ya complications zake, familia nyingi za kikristo huwa zina experience ndoa chache sana ikilinganishwa na familia za kiislamu. Dini ya kiislamu imerahisisha sana suala la ndoa. Matokeo yake familia nyingi za kikristo huwa hazifahamu saikolojia siasa za waoaji.

Ni hivi muoaji anapo kuja kwenye familia yako, usifikiri hajaona mwanamke mwingine au hana option nyingine. Most of the time muoaji anapofikia hatua ya kuja kujitambulisha nyumbani kwenu tayari anakuwa na option zingine kama mbili, tatu au hata nne.

Nikija kwenye familia yako kuchumbia, halafu ukaniletea complications ngumu, mimi nitakacho kifanya nita kuachia binti yako nitaenda kwenye familia ambayo haitaniwekea complications ngumu.

Ninapokuja kwenye familia yako usinichukulie kwanza kama mtu ambae ninataka kumuoa binti yako, nichukulie kama mtu ambae nimekuja kutazama kama familia yako ina complications au la!
Zee lote hilo linashindwa mil.3? 😬😬
 
Kirahisi hakidumu
Kutokudumu ni kuchagua kwako asiekufaa pia binadamu hatuwez kuwa sawa never watu mmekutana ukubwani kilamtu kalelewa kwao kumatch sio rahis Inahitaji uvumilivu mkishindwa kuvumiliana achaneni Kwa amani
Talaka ipo na japo ni Sheria ila haifurahishi ila Tulivoumbwa hatufanani na hatuendani 💯
 
Wee kiwa nanbackup plan ndugu yangu, hawa wanaume ni mashetani kama mlivyo mashetani nyie wanawake. Unabwagwa siku yoyote🤣🤣🤣🤣🤣
Always unachaoamin maranying ndo kinatokea ukiamini utapata mwanaume 😂 shetani unapewa tu shetani lako kama mm nikipewa wew lazima nipate kichaa🤣🤣🤣
 
Mtu anayeshindwa kulipa mahari, au anayelalamika kupangiwa mahari kubwa baada ya kufika kwa wazazi ni mjinga.

Kwa sababu, hizi habari zote alitakiwa kuweza kuzipata kabla ya kwenda huko, kwa upelelezi wake.

Na mimi nakwambia, kabla ya kwenda huko nitajua kama wataweza kuelewa msimamo wangu wa kupinga mahari ama vipi.

Kama wanaendekeza tamaduni za kijima zinazomdhalilisha mwanamke kama mahari, hata hiyo ndoa haiwezi kufana na kudumu.

Kwa sababu ndoa itaunganisha familia, na mimi sitaki kuendeleza ujima kwenye familia yangu.

Ndiyo maana nikakwambia siwezi kuoa kijima.

Lakini watu tupo tofauti sana, inawezekana kabisa usinielewe.

Nikawa kama ngamia ninayemuandikia samaki habari za jangwa lisilo na maji, samaki akasoma akawa haelewi inawezekana vipi kukawa na sehemu haina maji kabisa.
Sawa mkuu japo sijui kwa nini umeweka shaka kwamba sitakuelewa.
Hapo kwenye upelelezi sawa ila pia kama umeshafanya upelelezi ukajua wazazi lazima watataka pesa na unamhitaji Binti nini utafanya?
Mimi sichukulii mahari Kama mila mbaya miongoni mwa Mila zetu na sijui ni kwa nini tunainasibisha na kudhalilishwa kwa wanawake.
Kwani hakuna siku utajisikia kuwapelekea wakwe zako zawadi ? Kwa nini tusiichukulie kama zawadi japo baadhi ya wakwe nao wanataka kama wanakomoa.
 
Anayeolewa ni Nani?
Dhana nzima ya kuolewa ni ya tamaduni fulani.

Utaliona hili vizuri katika lugha.

Katika Kiswahili kuna anayeoa na kuolewa.

Katika Kiingereza, hakuna anayeoa wala kuolewa. Watu wanaoana. They get married.

Sasa wewe umejifunga katika utamaduni, utamaduni uliopitwa na wakati.
 
Back
Top Bottom