Wakuu naombeni mnipe muongozo jinsi ya kuingia Zanzibar, Nahitajika kuwa na vitambulisho gani?. Naenda kutafuta kazi.

Passport, ya kusafilia, NIDA,au kadi ya mpiga kura
 
UONGO MTUPU ETI WAZANZIBAR WANA ROHO NZURI
 
Zanzibar pagumu sana kutoboa.
Kwa nini usiingie hapo Dodoma au Dar tu ukapambane?
Kweli Zanzibar kutoboa ni ngumu lakini kama anataka kwenda kutafuta Milioni moja au mbili ili arudi Tanganyika afanye biashara Adobe hapo sawa, Zanzibar mji wa kichawi sana ule Mifumo imeshkwa na watu wawili watatu tofauti na Tanganyika. uku Tanganyika mimi ninaweza kwenda nje ya nchi nikaagiza Sukari na Ngano na Sabuni hakuna shida ila Zanzibar upati hiyo ruhusa kwasababu hiyo biasharaku kuna mfanya biashara mkubwa anaifanya kwa hiyo wewe unazuiliwa. Mfano MO Dewji analeta Mafuta ya kula anakua peke yake tu mtu mwingine akitaka kuagiza ananyimwa Kibali.
 
Tsh 200- mpaka utakapo fika kikomo cha mfuko wako! au umekosea ni mia mbili au elfu 2
 

m pia nataka mwongozo asanteee!
 
Mkuu-nitakupa connection kuanzia trh 3-5 January kuhusu kampuni Fulani kubwa Sana inayojihusisha na Ujenzi utafanya Kazi mpaka ukimbie Nssf na benefits nyingine wanatoa

Hii ni kwako tu Kwa sasa ukiwa tayari utani-Pm
 
Tsh 200- mpaka utakapo fika kikomo cha mfuko wako!
Sijakosea, kuanzia shilingi mia mbili (200) na kuendelea unaanza kupata chochote tumboni. Andazi, kisheti, kachori, katilesi, chai,uji n.k huanzia bei hiyo!
 
Zingatia Zanzibar ni Nchi.
 
Ndoto ya Kila Mtanganyika Kwa hivi Sasa ni kuingia Zanzibar hali hii isipodhibitiwa sijui hali ya Zanzibar itakuwaje baada miaka 10
Wenye dhamana waliangalie hili Kwa jicho la tatu kisiwa kinazama

Kwa sababu kule huduma za kijamii ni nafuu mno kuliko Bara. Huduma kama hospital mke akijifungua ni bure 100%, Umeme wanateleza tu, vifaa vya kielectronic bei sawa na bure. Chamoto kipo Tanganyika!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…