Wale ambao hatuna Mpango wa kuoa tuendelee kupeana Mbinu za Maisha

Mleta uzi ulisahau wapi kunitag?
 
hatuwezi acha iga wazungu, maana bila wao hata hii JF using ijua.. wala isingekuwepo.. Kana una good management ya maisha na afya uzeeni huwezi pata shida..
 
Watu wanaangalia uzee kwa matatizo yani wameisha jiandaa kisaikolojia kuzeeka na matatizo..
 
Kwahiyo kabla ya kuoa uliishi ukiwa hujui maana halisi ya kuwa mwanaume?

Ni kweli siwezi kukupangia maisha ila usiwe attached na mwanamke kiasi hicho.
Nimeoa na nina mke mmoja tu, ila nilishamuambia kama tutajaliwa kuishi, mie nikifika miaka 55+ , tutaachana sitokuwa tayari kuishi na mwanamke zaidi ya hiyo age. na uzee wangu kama ikatokea nikazeeka sijawai waza waza uzee wa Majanga.. huenda uzee ukanikuta nikiwa mwalimu katika ngazi ya vyuo hata kama part time.. nikiisha zangu kwenye nyumba yangu shambani huko nakula wine, zoezi mala moja moja naosha rungu mahala nitapojisikia kuosha, kazoezi safi kabisa.. maswala ya kuchambana kwangu hayapo nitakufa na nguvu zangu ..
 
Mkuu

Pole Sana,najua unachoogopa ni kile cheti cha ndoa kinachofililisi sana!

Nakushauri ishi na nwanamke zaa nae WATOTO halafu hata kile cheti kisiwe muhimu kwenye Maisha yenu!

Halafu fanya KWA ajili ya WATOTO wako tu vile vya msingi kama nyumba na Biashara YEYOTE ile ya kipato halafu ukichoka mwachie aviendeleze wewe endelea na mambo YAKO tu! Huku ukija kuwacheki wanaendeleaje mara KWA mara Ili usikose Mtoto wa kukupikia hata uji ukitepeta!!

Najua alieharibu ndoa ni mrumi na Tabia zake za vyeti kwenye matukio! Muhimu kwenye Maisha MATOKEO yake kizungumkuti!!
 
"Utakufa na nguvu ZAKO"

Utajipiga Risasi au Autanasia ya kunywa sumu FULANI lakini slow killing process!!?
 
"Utakufa na nguvu ZAKO"

Utajipiga Risasi au Autanasia ya kunywa sumu FULANI lakini slow killing process!!?
Watu wengi wanakufa na nguvu zao, kufa sio lazima hadi upatwe na malazi ya kukuudhofisha mwili. Watu wanakufa na uzee mwema kabisa. Unakuta hata jioni alikuwa anapalilia kashamba kake ka maua, anamaliza anaoga, anaenda lala ndio inakuwa mazima na ndio kifo ambacho nina imagination nacho, sio kufa hadi uharishe ujinyenyee mie sijiwazii hivyoo.. wakati mwingine Mwenyezi Mungu hutupa kile tunacho imagine na kukiwaza
 
Kuna mmoja hapa analala kwenye gesti ashafukuzwa kila kona anazunguka na mkoba na tv na pasi hana hata pa kulala
Narudia tena kusema hili jambo mnachanganya mambo,mada ni mbinu zipi tuende nazo katika ishu ya kuhakikisha tunabaki katika ubachela wakati wote wa maisha yetu,hapa hatujaongelea mambo ya watoto au ndugu.
Punguzeni jazba wakuu wa pinga pinga.
 
mda wa ndoa ni upi ? Ndoa inaweza pia kukuvunjia heshima
Mda wa kuingia ndoani ni very debatable, kila mtu ana umri wake anaoona ni sahihi kuishi na mwenza, mwingine 25, mwingine 40 nk.

Hatusemi ndoa ndio kila kitu, hata vitabu vinasema;

Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA.

Lakini sio lazima mtu kuingia kwa ndoa as Paulo alisema;

Na sasa kuhusu mambo mliyoniandikia. Ni vizuri mtu asioe. Lakini kwa kuwa dhambi ya zinaa imeenea, kila mwanamume awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.
 
😁😁😁 naona umeshusha andiko. Amen
 
Nilicho kiona kwenye huu uzi wengi wana hofu ya maisha na wanajiwazia ukuda tu uzeeni kwao.. wacha wajiandae kuchambwaa maana huenda ndio kiu yao kubwaa
Mmh asa na ww rafiki angu li uzi la zamaani we ndo unaliona leo afu tusshasahau hata tulicomment manini

Lesson: haya ni mawazo ya mtu na sio kwamba ndivo alivo bhana sawa mzee mubaba
 
Nataka tuache(!) uzinzi mkuu🀣🀣🀣
😁😁😁 mie mbona sio mzinzi na hapa nipo na mke wangu, sema kalala mie kuna ka documents nilikuwa namalizia kukaandaa tu. Ukweli napiga humu story ila nina ndoa yangu na nina iheshimu sana aisee.. naelekea hata kuacha masihara humu nacho andika sikiishigi hadi watu wameanza nichukulia hivyo ..
 
Hii ni sehemu ya kupiga story na kumaliza vistress vidogo na zile stress kubwa, chukulia hivyo na uishi mkuu. Nikizini, akiiba, mwingine akiua...nk wote tunahesabika wadhambi tu na tunahitajo toba ili tusamehewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…