Wale Graduate mlioweza kujiajiri mlitumia mbinu (njia) kuweza kujiajiri?

Wale Graduate mlioweza kujiajiri mlitumia mbinu (njia) kuweza kujiajiri?

Mzee mimi niliajiriwa na private company nimefanya kazi kama miaka 3 hivi ila hali ikazidi kuwa mbaya, baadaye nikapiga kazi chini nikaanza biashara ya mazao nilipiga root moja kisha wahindi wakashusha bei nikaachana nayo nikaanzisha biashara nyingine nilisota kama miezi 9 hivi mambo yakaanza kujiset yenyewe ila changamoto kuu ilikuwa capital.
Mjomba unapitia Njia ,ninazopitia Mimi .Naomba tupeane ushauri DM plz
 
Kutokana hili Tatizo la Ajira kuzidi kuongeza hapa Nchi nakuacha baadhi ya Graduate wakizagaa tu mtaani ,kuzulula mtaani , kukaa nyumbani tu naomba mtusaidie kutupa njia au mbinu mlizotumia kuweza kujiajiri

Graduate wengi sana wapo mtaani kwa sasa hawajaweza kujiajiri , wengine bado wanasumbuliwa na mawazo (stress) zaidi ya mwaka wa tatu sasa hivi je nyie mlioweza kujiajiri mlianzaje hadi mkafanyikiwa kujiajiri ?

Ni njia (mbinu) gani mlitumia hadi mkaweza kujiajiri?
++Kama vile kupata mtaji(mlianza na mtaji wa shingapi?)
++Biashara mlizo anzanazo
+++Changamoto
+++ kukwepa aibu na mengineyoo


Naomba mtuambie jinsi mlivyo fanya hili litasaidia sana graduate waweze kupata fikira mpya na waweze kujiajiri huku wanatafuta ajira wengine wajiajiri kabisa kuliko kukaa tu nyumbani , kuzulula mtaani, kushinda kwenye mitandaoni.

Mtaji ni changamoto
Utapitia kipindi cha madeni mpaka utakimbia mji ila baada ya muda mambo yakikaa sawa utaenjoy
Kikubwa chora ramani yako vizuri kisha komaa nayo mpaka kieleweke
 
Kutokana hili Tatizo la Ajira kuzidi kuongeza hapa Nchi nakuacha baadhi ya Graduate wakizagaa tu mtaani ,kuzulula mtaani , kukaa nyumbani tu naomba mtusaidie kutupa njia au mbinu mlizotumia kuweza kujiajiri

Graduate wengi sana wapo mtaani kwa sasa hawajaweza kujiajiri , wengine bado wanasumbuliwa na mawazo (stress) zaidi ya mwaka wa tatu sasa hivi je nyie mlioweza kujiajiri mlianzaje hadi mkafanyikiwa kujiajiri ?

Ni njia (mbinu) gani mlitumia hadi mkaweza kujiajiri?
++Kama vile kupata mtaji(mlianza na mtaji wa shingapi?)
++Biashara mlizo anzanazo
+++Changamoto
+++ kukwepa aibu na mengineyoo


Naomba mtuambie jinsi mlivyo fanya hili litasaidia sana graduate waweze kupata fikira mpya na waweze kujiajiri huku wanatafuta ajira wengine wajiajiri kabisa kuliko kukaa tu nyumbani , kuzulula mtaani, kushinda kwenye mitandaoni.

Mtaji ni changamoto
Utapitia kipindi cha madeni mpaka utakimbia mji ila baada ya muda mambo yakikaa sawa utaenjoy
Kikubwa chora ramani yako vizuri kisha komaa nayo mpaka kieleweke
 
Welll doneee[emoji106][emoji106][emoji106][emoji106]
Nilipomaliza chuo sikua na mishe ya kufanya home..nikawaza nifanye Nini ili nitoke na kudanga siwezi.

Nikakumbuka Nina accnt ya insta yenye followers 2000 ..nikafikiria changamoto inayowasumbua wanawake hasa kwenye ngozi zao nikapata jibu (strechmark).

Nikakngia Google nikagoogle picha ya mtu mwenye michirizi (before&after) nikaipost ile picha na tumaelezo tudogo..namshukuru Mungu nilipata wateja Kama watano hivi wawili wa dar watatu wa mikoani

Wale wa mikoani wakanitumia pesa na pesa hiyo ndio ilikua mtaji wa kununulia chupa na malighafi.

Nikatengeneza bidhaa nikawatumia wa mkoani na dar nikawepelekea walipo..Safari yangu ya ujasiriamali ilianzia hapo na hadi Sasa naendelea nayo hata nimesahau Kama nilisomaga chuo.
 
Nikuulize swali dogo tu msotaji, baada ya msoto wa myda mrefu na elimu yako mtaani je unaweza kwenda kuuza mifuko sokoni?
 
mkiwa vyuoni mnabetua sana watu kwa kujiona nyie ndo nyie ndo maana mnaona aibu kujimix.
Kweli kabisa. Huwezi kujiajiri ghafla tu. Nakumbuka mtaji wangu ulianzia Kariakoo. Likizo nilikuwa siendi nyumbani, naingia kariakoo enzi hizo wakipanga viatu vya plastiki na raba za kichina za konfu barazani. Nikawa nafanya udalali hasa kwa wazungu na wachina. Wenye viatu hawajui umombo, kariakoo nzima wakipata wazungu waniniita mimi. Hivyo nikajichanganya nao hadi week end nikawa nashinda kariakoo.Wakaniita msomi. Tulipofukuzwa chuo sababu ya mgomo mimi ndio ikawa fursa. Unaweza ku imagine baada ya kugraduate nilikuwa na pesa kiasi gani.Usidhani nilifeli, kwanza sikuwahi kupata hata sup. Japo nilikuja kuajiriwa lakini nikawa nafanya biashara pia kwa ule mtaji nilioupata kariakoo.

Biashara ilikuwa kubwa nikaacha kazi bila woga. Sasa hivi ndio hao na bahasha zao nawaajiri japo ni mapasua kichwa. Hawakuwa na kazi, nimewapa kazi halafu wananiibia eti wasukume Range kama mimi. Nyambaf. LEO MTAWEZA KUJISHUSHA HIVI ENYI WA MILEGEZO?
 
Mimi nilianza na mtaji nguvu zangu, nilikwenda Kigoma, nikafyatua tofali za kuchoma, nikauza kwa shule moja ilikyokua ikijengwa nikapata pesa, nikaamua kurudi town, nikatafta frame maeneo ya chuo kikuu nifungua stationery ambayo nimeitumikia kwa muda wa miaka mitatu ndipo nikapata ajira. Changamoto kubwa niliyoipata ilikuwa ni kufanya maamuzi ya kuanza.
 
Mtaji ni changamoto
Utapitia kipindi cha madeni mpaka utakimbia mji ila baada ya muda mambo yakikaa sawa utaenjoy
Kikubwa chora ramani yako vizuri kisha komaa nayo mpaka kieleweke
Mtaji siyo sababu. Capital ni universal problem ukiweza kutatua tatizo la mtaji then wewe ndiyo mjasiliamali.
 
Mimi nilianza na mtaji nguvu zangu, nilikwenda Kigoma, nikafyatua tofali za kuchoma, nikauza kwa shule moja ilikyokua ikijengwa nikapata pesa, nikaamua kurudi town, nikatafta frame maeneo ya chuo kikuu nifungua stationery ambayo nimeitumikia kwa muda wa miaka mitatu ndipo nikapata ajira. Changamoto kubwa niliyoipata ilikuwa ni kufanya maamuzi ya kuanza.
Mkuu,

Nami nataka kufanya hiyo biashara Chuo Kikuu,
Taratibu za upatikanaji wa fremu zipoje huko?
 
Nilipomaliza chuo sikua na mishe ya kufanya home..nikawaza nifanye Nini ili nitoke na kudanga siwezi.

Nikakumbuka Nina accnt ya insta yenye followers 2000 ..nikafikiria changamoto inayowasumbua wanawake hasa kwenye ngozi zao nikapata jibu (strechmark).

Nikakngia Google nikagoogle picha ya mtu mwenye michirizi (before&after) nikaipost ile picha na tumaelezo tudogo..namshukuru Mungu nilipata wateja Kama watano hivi wawili wa dar watatu wa mikoani

Wale wa mikoani wakanitumia pesa na pesa hiyo ndio ilikua mtaji wa kununulia chupa na malighafi.

Nikatengeneza bidhaa nikawatumia wa mkoani na dar nikawepelekea walipo..Safari yangu ya ujasiriamali ilianzia hapo na hadi Sasa naendelea nayo hata nimesahau Kama nilisomaga chuo.
well done
 
Mimi nilianza na mtaji nguvu zangu, nilikwenda Kigoma, nikafyatua tofali za kuchoma, nikauza kwa shule moja ilikyokua ikijengwa nikapata pesa, nikaamua kurudi town, nikatafta frame maeneo ya chuo kikuu nifungua stationery ambayo nimeitumikia kwa muda wa miaka mitatu ndipo nikapata ajira. Changamoto kubwa niliyoipata ilikuwa ni kufanya maamuzi ya kuanza.
Unafyatuaje tu tofari bila kuwa napesa, inamaana ukiwa na nguvu tu una hata shingi 10 unaweza fyatua tofari.
 
Nilipomaliza chuo sikua na mishe ya kufanya home..nikawaza nifanye Nini ili nitoke na kudanga siwezi.

Nikakumbuka Nina accnt ya insta yenye followers 2000 ..nikafikiria changamoto inayowasumbua wanawake hasa kwenye ngozi zao nikapata jibu (strechmark).

Nikakngia Google nikagoogle picha ya mtu mwenye michirizi (before&after) nikaipost ile picha na tumaelezo tudogo..namshukuru Mungu nilipata wateja Kama watano hivi wawili wa dar watatu wa mikoani

Wale wa mikoani wakanitumia pesa na pesa hiyo ndio ilikua mtaji wa kununulia chupa na malighafi.

Nikatengeneza bidhaa nikawatumia wa mkoani na dar nikawepelekea walipo..Safari yangu ya ujasiriamali ilianzia hapo na hadi Sasa naendelea nayo hata nimesahau Kama nilisomaga chuo.
Ebu jazia maelezo kidogo mkuu, nami niweze kuanza
 
Tatizo ni kwamba Most of graduates tunashindwa kuwa wabunifu,katika kipindi hiki ambacho hata wafanyabiashara hali sio nzuri sana, ni lazima nasisi graduates tutumie akili nyingi pia kwenye kutafuta kazI hasa kama hauna connection. Tunalalamika kwamba kazi zinatolewa kindugu au kirafiki lakini ukijiuliza tu mwenyewe Mfano wewe ndo boss na unatafuta mfanyakazi,anatokea graduate wa kwanza anatafuta kazi lakini humfahamu kabisa,upande wa pili anatokea rafiki yako unaemwamini anakwambia anamfahamu graduate ambae anachapa kazi,muaminifu na pia anawafahamu mpaka wazazi wake,kama wewe ndo boss utamchukua mfanyakazi yupi katika position hiyo ya kazi? DIRECTLY wengi watamchagua huyu wa pili maana hata kama ataleta uharibifu wowote inakuwa rahisi kumpata maana vijana wa sasa hivi nao hatueleweki,Kwa hiyo kwa sisi ambao hatuna connection ni lazima kuwa na vitu vya ziada na pia kuwa ubunifu ili kupata kazi.
NJIA RAHISI NINAYO IONA ILI KUPATA KAZI HASA KWA KIPINDI HIKI.
Unajua katika hiki kipindi kila boss anapokutana na graduate anaetafuta kazi wengi wanakuwa na wasiwasi kwamba huyu mtu nikimwajiri nitamlipa kiasi gani na degree,masters au P.h.d yake.mtihani mkubwa uko hapa na maboss wengi wanashindwa kutuajiri sababu kwanza anajua kwamba hatuna experience,pili hajui tabia yako na tatu hali ya biashara pia sio nzuri sana hivyo ana wasi wasi atakulipa kiasi gani uridhike na masters yako au P.h.d yako.Njia rahisi ya kuli ruka hili kweli kama wewe ni graduate unaetafuta kazi kweli na ni mchapa kazi ni kwa kwa kujitofautisha na graduates wengine wanaohangaika na mabahasha mjini kutafuta kazi,WAKATI wao wanatafuta kazi wewe tafuta kitu unachokipenda hasa vitu ambavyo vitakupatia UJUZI na itapendeza zaidi kama ujuzi huo utakuwa katika field ambayo umeisomea.MFANO kama umesomea mambo ya Computer science na unapenda labda mambo ya kudesign Website,graphics design au software development Tafuta Kampuni zako kama tano ambazo kweli zinadeal na hizo kazi za designing,badala ya kuomba kazi wewe OMBA kujitolea katika moja ya kampuni utakayo pata kati ya hizo tano,Kuwa mbunifu pia kwenye kuomba nafasi hizi za kujitolea,Mfano unaweza ukatafuta hata watu watatu wakajifanya ni wateja labda wanataka huduma ya kutengenezewa website ukaenda na mmoja siku ya kwanza kwenye kampuni ya kwanza ukajieleza wewe ndo umemtafuta na umemleta kama mteja,baada ya siku mbili ukampeleka mteja wako wa pili anajifanya anataka kudesigniwa logo, baada ya siku nne ukampeleka mteja wa tatu alafu siku hiyo hiyo ukaacha na barua yako ya kuomba kujitolea,Haki ukifanya hivyo kwa kampuni zote tano huwezi kukosa hata moja.
WORKING PRINCIPLE
Hapa ninavyosema uombe kujitolea haitakuwa kujitolea kweli kweli kama kweli wewe una nia na ni mchapa kazi kweli kweli,kama kweli unachapa kazi haita pita hata mwezi mmoja asilimia kubwa za makampuni wataanza kukulipa japokuwa haitakuwa sawa na degree,masters au p.h.d yako.Kuomba kwa kujitolea itaifanya kampuni kuwa free kukulipa kutokana na uwezo wake maana sio kla kampuni zinauwezo wa kumlipa mfanya kazi kutokana na elimu aliyo nayo.Hata kama wasipokupa kitu komaa maana UJUZI utakaoupata ndio muhimu kuliko hata mshahara ambao wangekulipa kwa elimu uliyo nayo.Njia pekee ya kutukomboa sisi kama graduates sio kupata KAZI bali kuwa na UJUZI,Baada ya muda ukiona umeiva vizuri na pesa wanayokulipa hauridhishwi nayo YOU CAN MOVE ON na kuanza kufanya hizo shuguli mwenyewe.KIUKWELI biashara unayoweza kuianza bila ya kuwa na mtaji kabisa ni kwa kuwa na ujuzi maana EVEN if utapewa mamilioni ya fedha uanzishe biashara labda ya kuuza products,huwezi kuwa na uhakika 100 percent maana biashara pia zinaweza kufa muda wowote,cha kujiuliza utafanya nini baaada ya biashara kufa?UJUZI ni security yako milele na hakuna yeyote anaeweza kuuchukua au kuku nyang'anya,LET US BE CREATIVE.
Umeeleza uhalisia asante kwa mchango mzuri
 
Graduates nendeni mkajiajiri kwenye kilimo, acheni ubwege.

Mtaji wako mkubwa ni nguvu zako na elimu yako. Mashamba yapo ya bure kabisa ktk mikoa ya Katavi, Tanga, na Tabora. Yaani sijui mnataka nn tena?


Sijui km uko serious..labda wakalimie kenya..kilimo cha Tanzania kina changamoto nyingi sana pia inataka mtaji mnene...mnasemaga tu mapori yamejzana manyara atalimia nn??kuandaa shamba lazima uwe na walu 1m..labda ukute shamba halin visiki...kulimisha tu ni 50000\...hizo hela za vibarua wanapata wpi??
Mbegu je bora wanasidiwa na nan.....hap mie nasemea kilimo biashara
 
Back
Top Bottom