Wale mliokimbilia kujenga Dodoma poleni sana

Wale mliokimbilia kujenga Dodoma poleni sana

Nakukumbusha tu hakuna mji duniani serikari imewekeza pekee ikaishinda majiji ya biashara. Mfano Beijing haijaishinda Shanghai, Abuja hajaishinda Lagos, Cape town na Johansburg hivyo hio ni ndoto ya alinacha.
Hapo hatushindanishi, bali tunaweza distribution angalau... sio kila mshamba wa nchii hii lazima akaishi Dsm, acha na washamba wengine wakaishi majiji yanayoifuatia Dsm.
 
Njia rahisi ya kujua kama dodma kuna mzunguko kwanza ni kuangalia idadi ya abiria wanaoingia kwa siku kutokea sehem kama dar na mikoa mingine. Kwa mtu ambaye alipita dodoma miaka ya nyuma anaweza dhani pamelala, ni wajinga wachache sana wamebaki na hiyo misemo kuwa dodoma hakuna movement. Kuna lodge zilizopo hazitoshi kulingana na idadi ya wageni wanaongia na kutoka . Nyumba ni chache sana kadri siku zinavyozidi kwenda mbele zinakuwa adimu sana sababu watu wanazidi ongezeka. Benki zinazidiwa. Ni dodoma tu ambako utakutana na tawi la crdb ambalo yamepishana mitaa na yote foleni lake la kufa mtu.
Mpaka equity wanafoleni dodoma.
Ni dodoma pekee ambako abiria hawaangalii bei ila huduma, dodoma happy nation ni ngalangala lakini mwanza ni luxury. Dodoma bila basi la choo ndani unafunga biashara.
Sasa fursa zilizopo dom
Kuna uhaba wa nursery shule za private ni chache wakat mahitaji ni mengi, mleta mada hujaiona hiyo fursa? Au unataka fursa za kutembeza vyombo.
Ujenzi upo kwa spind anzisha kabiashsra katofari kama una hela, sisi tunajua huna
Mahindi mengi sana kibaigwa sagisha unga safirisha kwenda dar utawapiga gepu wale wasongea ambao kusafirisha kwa tani wanalipa 120000 wakati dom ni 30000 na utofauti bei ni 100. Yaan dom mahind sasa hivi ni 60000 wakat songea ni 50000 ila kusafirisha mahind toka songea dar utahitaji 3600000 kwa tani 30 wakat dom utalipia 900000. Utofauti wa 1.7mil.

Tafuta hela we bwege uache kuishi kwenye nyumba za uridhi
Achana nae huyu msukuma wa sangamwalugeshi kaja mjini kwa lift ya treni!Dodoma aliiona pale relini tu
 
Tatizo mmeingia dar juzi ndo mnapiga kelele. Hivyo viwanja unavyonunua kwa square meter kibada wenzio tulinunua kama mashamba tena kwa kubembelezwa miaka ya 2003. Tembeni muelimike. Nyie kaeni na dar yenu mtakuja shtuka wenzenu washakuwa mabilionea
[emoji2962][emoji2962][emoji849][emoji849]
 
Nyie endeleeni kupoteza muda na dodoma, mkija dar hakuna plot mtakayo weza ishika.. sqm 1 ni elfu 45 hadi elfu 50. Kiwanja cha sqm buku uwe na kuanzia milioni 45 na kuendelea, hiyo dodoma haiwez kukua kama ilivyo pewa promo
Wa kuja mna taabu![emoji23][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]daah!mnashoboka na Dar wakati watu wazawa hatuna habarii!pole sana
 
Tatizo mmeingia dar juzi ndo mnapiga kelele. Hivyo viwanja unavyonunua kwa square meter kibada wenzio tulinunua kama mashamba tena kwa kubembelezwa miaka ya 2003. Tembeni muelimike. Nyie kaeni na dar yenu mtakuja shtuka wenzenu washakuwa mabilionea
Tena mapori hata lami hawana!!wanajionaa wajaanja!!!
 
Dodoma ya sasa sio ya zamani, nimepita last week nikakaa siku 2 aisee imebadilika sana, Dodoma imejengeka kwa kiasi kikubwa.. JPM alifanya kazi sana kuiboresha Dom

Siku hizi mpaka kuna Shopping Mall 😂😂😂

Ila tatizo la Dom ikifika saa 4 usiku unaweza kusema ni saa 8 usiku, gari za kuhesabu 😂😂 sio kama Daslamu au Mwanza.

Dodoma imepanuka sana ukilinganisha na zamani.

Promo za Serikali ya 4 imeisadia Dodoma kupanuka na watu kuhamia huko.
 
Kipindi Serikali au mtu mmoja aliyeamua katangaza Dodoma kama makao makuu kwa maslai yake, watu wa Mikoani wakakurupuka kutoka huko kwenda kuwekeza Dodoma, sasa mambo yamekuwa magumu wanalalamika [emoji3] biashara zimekuwa ngumu na ni za msimu.

Nyumba walizojenga hazina wapangaji yaani mambo ni tafrani apeche alolo
Watu waliokimbilia huko wanalia wanapauka kwa vumbi na jua, Maji yamejaa chumvi hata kuyanywa ni shida
Ndo mkome kukurupuka kama chafya bila kufikiria.

Hizo nyumba zibebeni mzilete huku kigamboni [emoji4]

Unakimbia Dar unaenda kuwekeza Dodoma sehemu ngumu vile una akili kweli bora ungeenda kuwekeza Arusha, Mwanza, Moshi, Mbeya, Dar

Unadanganya watu. Haya unayosema umetunga asilimia 100
 
Dodoma ya sasa sio ya zamani, nimepita last week nikakaa siku 2 aisee imebadilika sana, Dodoma imejengeka kwa kiasi kikubwa.. JPM alifanya kazi sana kuiboresha Dom

Siku hizi mpaka kuna Shopping Mall [emoji23][emoji23][emoji23]

Ila tatizo la Dom ikifika saa 4 usiku unaweza kusema ni saa 8 usiku, gari za kuhesabu [emoji23][emoji23] sio kama Daslamu au Mwanza.

Dodoma imepanuka sana ukilinganisha na zamani.

Promo za Serikali ya 4 imeisadia Dodoma kupanuka na watu kuhamia huko.
Watu wamejenga wenyewe then unasema mwendazake ndo kaboresha acha ujinga wewe n jitihada za watu binafsi wala sio yeye
 
elewa swali kwanza
Naona unalikimbia swali...Jibu ni kuwa; mwekezaji mkubwa wa majengo makubwa hapo Dar es Salaam alikuwa ni serikali; na mashirika makubwa ambayo yanamilikwa na serikali (NHC, PPF, NSSF(PSSSF) etc). Hao wote sasa hawatofanya tena uwekezaji hapo Dar; na badala yake wanawekeza Dodoma. Hivyo ni kuwa Dar es Salaam ya leo, itaendelea kubaki hivyo hivyo kwa miaka 5-10 ijayo. Labda kama nyinyi watu mmoja mmoja kama wewe; mtawekeza kwa vijumba vyenu vya chumba kimoja na choo nje; kule MBAGALA MAJI MATITU na BUZA KWA MPALANGE. Sasa sijui kama hizo nyumba za chumba kimoja na choo nje zitaibadili hii sura ya Dar es Salaam ya sasa?? Hapo utajijibu mwenyewe. Kwa Dodoma mambo yatakuwa ni tofauti, maana uwekezaji mkubwa wa serikali umepelekwa kwa makusudi huko (strategically). Hivyo muonekano wa Dodoma utakuwa tofauti kabisa. Hahihitaji PhD ya UDOM kujua hayo; jaribu tu ku-visualize kwa akili ya kawaida, utaona ukweli.
 
Back
Top Bottom