Wale tuliomaliza darasa la 7 mwaka 2000 kurudi nyuma tujikumbushe ilivyokua siku matokeo ya la 7 yanatangazwa

Wale tuliomaliza darasa la 7 mwaka 2000 kurudi nyuma tujikumbushe ilivyokua siku matokeo ya la 7 yanatangazwa

Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.
Aisee......
 
Elimu ya 2000 kurudi nyuma ilikuwa tough sana. Yani darasa lenye wanafunzi 45 wanachaguliwa wawili au watatu tu na hapo umekaza ile ile.
Siku hizi shule za CCM, mtu mpaka anamaliza std 7 hata jina lake kulisoma ni shida lakini nae anafaulu.
Wanapigwa kijiko siku ya paper.
 
😲😲😲😲 ivi humu kumbe kuna wengine wanajitoaga ufahamu afu Ni watu wazimaaa🙆🙆🙆🙆,huo mwaka hata shule ya msingi sijaanza.
 
Ilikua heshima sana kufaulu kipindi hicho...Wilaya nzima shule ya sekondari ni moja tu,ukifaulu unafahamika...mitihani ilikua 3 tu na inafanyika siku 1.
 
Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.
Hakika mkuu mie nilihitimu la 7 mwaka 1995 Hali ilikuwa mbaya Sana.
 
Hakika mkuu mie nilihitimu la 7 mwaka 1995 Hali ilikuwa mbaya Sana.
Nchi ilikuwa maskini kinoma ndugu yangu. Hizo ndo enzi kwenda Mwanza kutokea Arusha mnalala njiani. Dar - Mtwara ni safari ya wiki nyakati za mvua. Umaskini ulikuwa umekithiri.
 
Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.
Kilikua kipindi cha hovyo sana, tushukuru sana utandawazi
 
Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.
Kipindi hicho kulikuwa na kufaulu na kutofaulu. Miaka hii kuna kuchaguliwa na kutochaguliwa!
 
Nimemaliza STD Seven mwaka 1997 kwenye shule mojawapo wilaya ya Kinondoni. Siku matokeo yametoka tumekwenda wilayani na marafiki zangu tumekuta watu wameshajaa kwenye ubao wa matangazo hata nafasi hakuna.
Kuna dogo mmoja namfahamu alitangulia ile kuniona tu akaniambia "Mwamba umepasua Azaboy umekwenda" akimaanisha Azania Sekondari. Aisee sikuamini nilipambana kwenye ule umati hadi nikaona jina langu, nilifurahi sana.
Kuna mwenzetu mmoja tulikuwa nae ametafuta jina halioni na alikuwa kipanga darasani, alitafuta jina lake hadi alikata tamaa. Kumbe kachaguliwa Mzumbe vipaji pekee kiakili, kuja kuona jina alishangilia kama Mwehu.
Kipinid kila Dar es salaam ilikuwa na shule za sekondari za serikali chache sana.
1. Azania- wavulana tupu
2. Jangwani- wasichana tupu
3. Kisutu- wasichana tupu
4. Zanaki- wasichana tupu
5. Forodhani- Mchanganyiko
6. Kibasira- Mchanganyiko
7. Kambangwa- Mchanganyiko.
8. Pugu
NB! Tambaza ilikuwa ni A-level tu (kuanzia mwaka 1994)
Pata picha Dar nzima wanafunzi wanagombania nafasi kwenye hizo shule ushindani wake ulikuwaje.
Asilimia kubwa tulitegemea Tuition ili kufaulu bila hivyo ni ngumu kutoboa.
Tuition maarufu za wanafunzi wa shule ya msingi wilaya ya kinondoni kipindi kile zilikuwa;
1. MT Zungu- Sinza,
2. Dani - Mburahati,
3. Boniface Ibunga- Mabibo.
Sahihisho, Tambaza ilikuwa A level tu kuanzia mwaka 1996.
 
1998 dah asubuhi naamka taarifa matokeo yametoka [emoji15] baada ya chai mbio magomeni wilayani watu kama wote tafuta tafuta na Wewe hadi saa 7 hola mtu nyomi. Tetesi gazeti la Dar Leo na Alasiri wametoa majina ya waliochaguliwa. dah mbio kkoo shule ya uhuru kulisaka gazeti. Pekua hola. Nikarudi home kinyongeee sana. Wamefaulu watu 16 mimi siko na nakuwaga top 10. Hata chakula sikula siku hiyo.
Kumbe bana Mungu ana mipango yake bana. Nikaja kusoma shule iliyobadilisha mengi sana maishani mwangu na watu niliokutana nao. The rest is history.
Wale walioenda Azania Forodhani Kibasila sijui Kambangwa Jangwani Kisutu waliotoboa hadi huku juu hata watatu hawafiki.
Nyakati ngumu sana miaka hiyo,mock unapasua vibaya National unapigwa chini nadhani ndo kipindi cha biashara ya majina waliofaulu inaangaliwa status ya familia ikoje nani aende nani asiende,ile ilikua sio kufaulu bali uchaguliwe unafaulu na hauchaguliwi
 
Shule za vijijin alikuwa anafaulu moja au wawili
Sio kufaulu ni kuchaguliwa,unafaulu kufika wastani lakini hauchaguliwi kulingana na mahitaji ya shule ni chache wanaangalia waliozidi wastani zaidi,ndomana class seven wa miaka hiyo ana compete na four wa miaka hii
 
1994 tulichaguliwa wawili shule yetu. ila ckwenda kusoma nikatorokea Nairobi.
 
Nakumbuka siku hii kaka yangu alikuwa anasoma Form VI Azania ile anarudi kitaa na furaha tele, ananiambia, dogo umetokea gazetini top 10 ya jiji la Daslam.

Kesho yake kabla ya kufika ubao wa manispaa pale Taifa, nikawa nawaza na mimi naenda kuwa Aza boy tuu, mara paap Kibaha hii hapa. The rest is history….
Hongera Alumni mwenzangu.
 
Back
Top Bottom