Wale tuliomaliza darasa la 7 mwaka 2000 kurudi nyuma tujikumbushe ilivyokua siku matokeo ya la 7 yanatangazwa

Wale tuliomaliza darasa la 7 mwaka 2000 kurudi nyuma tujikumbushe ilivyokua siku matokeo ya la 7 yanatangazwa

Nyakati ngumu sana miaka hiyo,mock unapasua vibaya National unapigwa chini nadhani ndo kipindi cha biashara ya majina waliofaulu inaangaliwa status ya familia ikoje nani aende nani asiende,ile ilikua sio kufaulu bali uchaguliwe unafaulu na hauchaguliwi
Kuna mtu matokeo yalitoka akaona jina lake limetoka wilayani ila kesho yake majina yamekuja kubandikwa kwenye kata yao halipo. Ilikuwa kilio. Bahati nzuri mjomba wake akamfadhili kwenda private school.
 
Hivi matokeo ya miaka ya nyuma yanaweza patikana online kweli . Maana page za necta kuna miaka hakuna
 
Nakumbuka siku hii kaka yangu alikuwa anasoma Form VI Azania ile anarudi kitaa na furaha tele, ananiambia, dogo umetokea gazetini top 10 ya jiji la Daslam.

Kesho yake kabla ya kufika ubao wa manispaa pale Taifa, nikawa nawaza na mimi naenda kuwa Aza boy tuu, mara paap Kibaha hii hapa. The rest is history….
We ni Getman Mwandemele nini?!!!!
Uliwakuta kina Kunambi, Kachingwe Kaselenge (r.i.p), Kadelya na Mwampaja?!!!!!
 
Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.
Sisi wa early 80s tuna comment wapi?
 
Second Selection iliniokoa .2000-Kahama .Wilaya nzima shule ya Sekondari ya serikali ilikuwa moja na mbili za private.Vijana wawili tu darasa letu ndio walienda shule za bweni nje ya mkoa .Mmoja marehemu ,mwingine anazurula tu Ulaya.Si haba na mimi nakula sahani moja na mashehe huku mkoani.
 
Second Selection iliniokoa .2000-Kahama .Wilaya nzima shule ya Sekondari ya serikali ilikuwa moja na mbili za private.Vijana wawili tu darasa letu ndio walienda shule za bweni nje ya mkoa .Mmoja marehemu ,mwingine anazurula tu Ulaya.Si haba na mimi nakula sahani moja na mashehe huku mkoani.
Ulimalia 99?
 
Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.

Daah mkuu hali ilikuwa inatisha. Mimi kti ya darasa lote tulichaguliwa wanne tuu. Alafu matokeo yanatolewa wilayani na sisi kijijini ni umbali wa 20 kms. Tuliletewa matokeo na mwalimu alioyeenda mjini. Kipindi hicho nikikatiza pale kijini nilikuwa naheshimiwa na kila mtu yaani ilikuwa vibe fulani mtaani ilikuwa gumzo. Nakumbuka siku ya kwenda form 1 wenzangu tuliokuwa darasa moja ambao ni majirani walikuja kuniaga siku naenda shule wakaniletea zawadi kila mmoja alinipa penseli kalamu na daftari. Kati yetu wanne wawili waliiishia form 2 wakaacha shule. tukabaki wawili. form four mwenzangu akafeli alikuwa mtu wa mishe mishe flani hivi wazazi wake walikuwa watumishi so dogo akawa anajiona matawi ya juu hajali sana kusoma. Mimi nikapata div 1, nikasonga form 5 na hatimaye chuo.
 
Daah mkuu hali ilikuwa inatisha. Mimi kti ya darasa lote tulichaguliwa wanne tuu. Alafu matokeo yanatolewa wilayani na sisi kijijini ni umbali wa 20 kms. Tuliletewa matokeo na mwalimu alioyeenda mjini. Kipindi hicho nikikatiza pale kijini nilikuwa naheshimiwa na kila mtu yaani ilikuwa vibe fulani mtaani ilikuwa gumzo. Nakumbuka siku ya kwenda form 1 wenzangu tuliokuwa darasa moja ambao ni majirani walikuja kuniaga siku naenda shule wakaniletea zawadi kila mmoja alinipa penseli kalamu na daftari. Kati yetu wanne wawili waliiishia form 2 wakaacha shule. tukabaki wawili. form four mwenzangu akafeli alikuwa mtu wa mishe mishe flani hivi wazazi wake walikuwa watumishi so dogo akawa anajiona matawi ya juu hajali sana kusoma. Mimi nikapata div 1, nikasonga form 5 na hatimaye chuo.
Hongera sana. Kiukweli ilikuwa ni huzuni kubwa sana kwa wale wanaokuwa hawajachaguliwa... mimi ninaamini kuna watu wangepata nafasi ya kuendelea wangekuwa wasomi wakubwa nchini. Ndo maana huwa nakwepa sana mambo ya kukutana kwenye party za watu mliowahi kusoma pamoja kwa sababu kwa wale ambao hawakuweza kuendelea mbele na bahati mbaya maisha pia yamewapiga inakuwa kama mnawanyanyapaa.
 
Back
Top Bottom