Walezi acheni kupeleka watoto bweni kama shule za kutwa zipo karibu. Bweni inaweza kuwa jehanamu kwa mtoto mdogo na kijana anayepitia balehe

Walezi acheni kupeleka watoto bweni kama shule za kutwa zipo karibu. Bweni inaweza kuwa jehanamu kwa mtoto mdogo na kijana anayepitia balehe

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Leo mtoto wangu wa darasa la nne kaniletea barua kutoka shuleni kwao kwamba eti yafaa zaidi awe anabaki huko huko shuleni boarding asiwe anarudi nyumbani. Nikiwa kama mzazi wake hii barua ilinipa hasira sana, hhizi shule za sikuhizi wametanguliza sana pesa kuliko watoto wetu, Kuna kipindi walinilazimisha nilipie school bus yao kwa shule ambayo mtoto aanatembea na wenzake wa shule ya karibu kwa dakika 15 niliakatalia kabisa, na kwenye hili la boarding wala siwezi kujiuliza mara mbili, Huyu mwanangu bado ni mtoto mdogo anahitaji uangalizi wangu, huko boarding mpaka aende labda akifika miaka 17 wakati ambao analau ana akili ya maisha na hata ile miaka ya foolish age ya balehe imeanza kufifia.


kupeleka mtoto huko boarding chekechea , msingi na O-level ni kumuweka hatarini mtoto, kwa form 5 kuna angalau. Boarding tulizosoma enzi hizo na hizi za sasa ni tofauti sana, Dunia imepitia mabadiliko mengi sana,,, Elimu pekee isiwe kigezo cha kumtelekeza mtoto huko boarding, mtoto kuwa chini ya uangalizi wa mlezi ni kitu muhimu sana,,

Huko boarding kusema kwamba umtegemee mwalimu na patron / matron kulea mtoto ni kujidanganya, shule nzima nakuta matron anasimamia wasichana zaidi ya 300 na patron anasimamia wavulana zaidi ya 400, hivi atawezaje kuweka umakini wote kwa mtoto wako? hata ukiwapa zawadi watie umakini kwa mtoto wako unadhani wewe ni mlezi pekee anaefanya hivyo ?

Haya ni baadhi ya mambo hatarishi yanayoweza kumkumba mtoto akiwa boarding bila uangalizi wa makini wa mlezi:

MAPENZI YA JINSIA MOJA - Mambo ya ushoga na usagaji kwa shule za boarding yapo tangu zamani ila yalikuwa kwa uchache sana lakini siku hizi utandawazi umeenea sana na kusambazwa kionekane ni kitu cha kawaida kupitia mitandao ya kijamii, filamu, tamthilia, katuni, games, miziki.. watoto bila uangalizi wa wazazi wanaiga haya mambo kirahisi hasa wakiwa boarding ambako uangalizi wa karibu wa walezi haupo, Tabia hizi zinaweza kuanzia mabafuni, wakiwa mabwenini mida ya usiku, hali inakuwa mbaya zaidi pale wale wanaopenda kuonea wenzao wakianza kutumia ubabe wao kuwalawiti kinguvu wenzao hasa wale wenye sura nzuri za mama zao.

Haya mambo yapo kabisa, Mwaka uliopita kuna mtoto wa rafiki yangu wa kazini alifukuzwa shuleni kwa sababu ya kushawishi wenzake wawe wanamlawiti, hii tabia ilianza alipolazimishwa kinguvu kwa mara ya kwanza ila kwa sasa hawezi kuacha, ameshafundisha wengine huu mchezo ambao nao yawezekana wameanza kuwaingilia kinguvu wanafunzi wenzao na si ajabu moja wao akawa mwanao.

UONEZI - kaika shule za boarding ni kitu cha kawaida sana, na endapo mtoto wako akiwa mwathirika wa hii ishu anakuwa ni muoga anashindwa hata kukwambia. Nimeshuhudia uonezi ukipelekea mpaka wawanafunzi kulawiti na wababe usiku wakati walimu wamerudi makwa na matron anauchapa usingizi, likizo mtoto anarudi wiki 2 au mwezi ila akirudi shuleni anaanza kula vipigo miezi minne mfululizo, anapumzika likizo wiki 2 anarudi tena shuleni jehanamu, mlezi hujui chochote hapo.

HAKUNA MSAADA WA ZIADA WA TUISHENI - hizi hizi tuisheni zinakuwa na wanafunzi wanakua wachache au mwalimu anakuja nyumbani kumfundisha mtoto peke yake, tuisheni hizi zinasaidia sana wanafunzi ambao wakiwa darasa la wanafunzi wengi hawaelewi vizuri, walimu hawawapi umakini, wanaogopa au hawapati nafasi ya kuuliza maswali, walimu hawaingii madarasani, walimu wanafundisha kwa spidi kubwa kuzidi uwezo wao, n.k huku tuishen mwalimu anamfundisha mwanafunzi moja moja kwa umakini, Mwanafunzi anakuwa huru kuuliza maswali, Mwalimu anafundisha kulingana na spidi ya uelewa wa mwanafunzi, mwalimu hakosi vipindi, n.k. Tuisheni zinasaidia sana sio za kuzibeza hata kidogo.

Kuliko kupeleka mtoto boarding ni bora nitafute kijana aliemaliza degree ya ualimu anaetafuta ajira niwe nampa elf 5 kila siku jioni awe anakuja nyumbani kumfundisha mwanangu one on one kwa umakini zaidi kuliko huko boarding ambako wanajisomea bila msaada wa ziada.

USHAWISHI WA MAKUNDI MABOVU - Makundi mabovu nayo hasa kwa vijana wadogo wanaobalehe ni hatari kwenye mindset ya mtoto, kijana akiangukia kundi bovu nae ataanza kuziiga tabia zao kwa dhana ya kuonekana mjanja, tabia hizi ni kama ulevi wa pombe, kuvuta bangi, ngono zembe bila condom, wizi, n.k. hakuna jicho la mlezi hapo, hakuna wa kumuokoa tofauti na day ambako ni rahisi mlezi kujua mtoto kuna mahala anateleza kwa kuchunguza mabadiliko yake ama hata kuzipata habari zake mtaani,, vijana wa form 1 hadi 4 wapo kipindi cha balehe, ni vema uwe nao karibu
 
St. Mary's Morogoro nao wana hii tabia. Mtoto wa darasa la nne mnataka apelekwe boarding kwa ajili gani?

Mtihani wa darasa la nne una ugumu gani mpaka mtoto mdogo wa miaka 8 hadi 10 akakae shuleni?

Wale watoto ni wadogo hawawezi kujitegemea bado wala kuishi mbali na familia. Ebu acheni uroho wa pesa mnaharibu watoto wa watu.
 
True boarding iwe gor high school. Nakumbuka school tuliandaa mgomo ila o level tuliwaambia watulie maana ilikua petition ya wakubwa inasound sana tofauti mkiwa na madogo. Pia hata msisitizo wa roll calls madogo wakiwa likizo haikuzingatiwa kama wao wakiwepo
Naunga mkono hoja, kipindi chote cha 0-16yrs mtoto awe chini ya uangalizi wa mzazi/mlezi.
 
St. Mary's Morogoro nao wana hii tabia. Mtoto wa darasa la nne mnataka apelekwe boarding kwa ajili gani? Mtihani wa darasa la nne una ugumu gani mpaka mtoto mdogo wa miaka 8 hadi 10 akakae shuleni?
Wale watoto ni wadogo hawawezi kujitegemea bado wala kuishi mbali na familia. Ebu acheni uroho wa pesa mnaharibu watoto wa watu.
Wanafanya biashara yaani lengo lao ni biashara, pesa
 
Kwa kifupi Boarding sio salama nyakati hizi, ilikuwa sakama enzi hizo ila sio enzi hizi, oia hizi shule za Sijui English medium wao wakao kibiashara asilimia 100 wanaforce watoto waende Bording kea sababu kuna pesa zaidi mzazi atalipa ili wao wapige pesa.

Mzazi usipo jiongeza inakula kwako ni bora ikishindikana peleka mtoto shule za Serikali kwani hakuna maisha huko?
 
Huu uzi ni muhimu sana. Ungesambazwa kwenye makundi mengi. Inaskitisha sana.Na ndio ukweli huu.Watoto wengi wanaharibika. Hali inatisha, kulikuwa na makabila kuona mtoto au kijana shoga, ilikuwa ni jambo lisilotegemewa kabisa, lakini sasa hivi makabila hayo ni wengi tu,na ni wasomi wazuri.
 
Kuna wakati huwa najiuliza maswali kuhusu baadhi ya wazazi kuwapeleka watoto wadogo boarding sipati majibu


Hivi ni uvivu wa kuwahudumia au tunakwepa usumbufu!? Kama ni hivyo sasa kwanini uwazae?

Pesa imetufanywa watumwa hadi tunasahau thamani ya mtoto.
 
Mtoto kuanzia miaka 0-16 anatakiwa alelewe na wazazi au walezi kwa ukaribu sana ili ajifunze tamaduni na tabia za asili yao. Pia itasaidia mtoto kutengeneza upendo na familia. Wazazi watajua tabia ya mtoto wao kwa haraka na kuweza kuibadilisha mapema. Boarding siyo sehemu salama kwa malezi na makuzi ya mtoto!
 
Mtoto kuanzia miaka 0-16 anatakiwa alelewe na wazazi au walezi kwa ukaribu sana ili ajifunze tamaduni na tabia za asili yao. Pia itasaidia mtoto kutengeneza upendo na familia. Wazazi watajua tabia ya mtoto wao kwa haraka na kuweza kuibadilisha mapema. Boarding siyo sehemu salama kwa malezi na makuzi ya mtoto!

Halafuuuu

Kwa ushauri tuu lakini, mzazi unaona una pesa za kumpeleka mtoto wa miaka 2, 3, 4.... boarding nursery na kwanini usiitumie hiyo pesa kuajiri walimu wamfundishe mwanao nyumbani?

Yaani pesa yangu naitafuta kwa jasho ikamtese mwanangu ati Boarding?!?
Hapana!!

Mimi mwenzenu hata Ile ya kumwamsha mtoto mdogo wa miaka2,3,4 saa11 saa 12 asubuhi ilinishinda!! Ni either niishi karibu walking distance na shule anayosoma mtoto au nifanye mipango ya homeschooling.

Boarding ataenda ukiwa mkubwa hukooo sekondari
 
Ukitaka kufanya mistake kwa wanao wapeleke boarding mapema mtoto kule ataondoka na vitu vitatu kati ya hivi

1. Kutokana na tabia chafu zinazoenea siku izi na kuonekana za kawaida jua kabisa boarding kuna ubabe mwingi yani kama jera kama mtoto wako ana sura ya mama ake mzuri mzuri lazima wampasue linda nakazia apa lazima wamchane tako nakumbuka ilikua miaka ya 90 tupo boarding kuna dogo alichanwa linda na wababe flani kisa deni

2. Apa utatengeneza mtoto mchoyo sana yani mbinafsi kwasababu maisha ya boarding nikuangalia mali zako tu hawafundishwi kitu kinaitwa sharing hii tabia watoto huwa wanarudi nayo nyumbani ndo maana unakuta mtu kasoma kafanikiwa vizuri lakini mgumu sana kweny mambo ya kusaidia watu waliomzunguka hata ndugu zake wa damu kwasababu maisha yake yote ametengenezwa kuwa mchoyo na mali zake kwaiyo ni vizuri umpeleke mtoto atleast A-level apo anajitambua

3. Upendo hupungua kwa wazazi
 
subiria waamke maana wiki hii walikuwa na pilika za kuwapeleka watoto wao Boarding hukohuko
Imekuwa kama fasheni lakini uhalisia wa shule nyingi sikuhizi wameweka malengo ya faida zaidi kuliko elimu. Shule anayosoma mtoto wangu wa darasa la 4 ni dakika 15 kutoka nyumbani waliniambia nilipie school bus nikawapiga chini maana nilijua hio ni biashara tu, Mtoto wangu anaongozana na wenzake wengi tu wanaosoma shule za karibu na shule yao na hajawai patwa tatizo, kwanza kuna stori huwa zinanoga sana njiani na kuyaishi maisha halisi ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom