Walimu Busega wachachamaa,wampa notisi ya siku 90 Maiko Kachoma (Mkurugenzi,Busega) wasema lazima Haki ipatikane

Walimu Busega wachachamaa,wampa notisi ya siku 90 Maiko Kachoma (Mkurugenzi,Busega) wasema lazima Haki ipatikane

Samwel90

Member
Joined
Jan 22, 2025
Posts
53
Reaction score
42
Walimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wameamua kugeukia Mahakama ili kudai haki yao baada ya Mkurugenzi wao, Ndugu Maiko Kachoma, kukaidi matakwa ya sheria na kupuuza maombi yao. Walimu hao, zaidi ya 150, wamempa notisi ya siku tisini kuhakikisha kuwa amekamilisha mchakato wa kuwatoa katika Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na kuwaunganisha na Chama cha Walimu Chakuhawata. Notisi hiyo inamtaka Ndugu Kachoma kushughulikia suala hilo mara moja, la sivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake kwa gharama zake mwenyewe.

Inasikitisha kuona baadhi ya wakurugenzi, walioteuliwa kusimamia watumishi wa umma na kufuata sheria za nchi, wanageuka kuwa viongozi wenye kiburi na dharau. Ndugu Maiko Kachoma amejitwalia mamlaka makubwa kiasi cha kuonekana kama "Mungu mtu," akiwataka walimu wamuabudu ili awatekelezee matakwa yao. Hali hii inazua maswali kuhusu vigezo vinavyotumika kuwateua viongozi wa aina hii.

Walimu wamebeba mzigo mkubwa wa kifedha kwa kuchangisha zaidi ya shilingi 5,000 kila mmoja ili kugharamia huduma za kisheria. Fedha hizi, ambazo zingeweza kusaidia familia zao, sasa zimetumika kwa sababu ya ukaidi wa kiongozi mmoja. Ni haki kwamba Ndugu Kachoma atoe fidia kutoka mfukoni mwake kwa
Screenshot_20250311-192501.png
inashangaza jinsi mtu anayekaidi sheria anaweza kutegemewa kutetea maslahi ya wananchi na kusimamia utungaji wa sheria. Tabia yake ya kiburi na ukaidi si tu inakera, bali pia inahatarisha uhusiano kati ya serikali na watumishi wa umma. Hata ofisini kwake, amekuwa kero kwa watumishi huku akijitambulisha kama "Afisa Kipenyo" au "Afisa Usalama."

Kwa mara nyingine, naomba mamlaka za uteuzi zimwangalie kwa makini Ndugu Maiko Kachoma. Kiburi chake kinazidi kuleta mgawanyiko na kuharibu taswira ya serikali mbele ya watumishi wa umma.

Screenshot_20250311-192443.png
 

Attachments

  • Screenshot_20250311-192515.png
    Screenshot_20250311-192515.png
    232.6 KB · Views: 1
Hatari sana,usipokuwa makini unaweza jikuta umejichukulia sheria mkono,huyo Kachoma aache kucheza na mishahara ya watu,akachezee mat **k ya mkewe
 
Mkuu hakuna mtu mpuuzi na mjinga kama bwana Kachoma,tumegoma kumnyenyekea,Haki haiombwi,inadaiwa, tunaendelea kushughulikia Kila sehemu,nasikia anampango wa kwenda kugombea ubunge,huyu jamaa kama wajumbe wananisikia wampige CHINI ,mnafiki sana,hafai
Huyo ni masaburi kama wakurugenzi wengine waliohongwa wawakatalie walimu, umbwa huyo!
 
Hatari sana pale tunapokuwa na viongozi wasiotaka kufuata sheria tulizojiwekea wenyewe na wanabaki kutaka kutunishiana misuri na watu ambao hawako katika nafasi ya kuweza kufanya hivyo,huu ni uonevu na utovu wa nidhamu na ukosefu wa maadili wa bwana Kachoma
Duh aiseee
 
Wakurugenzi wengi ni wajeuri mnoo, kwani hamna chombo cha kwasilisha malalamiko juu yao, wamekua miungu watu, wanakanyaga taratibu na miongozo mbalimbali ya utumishi wa umma. Watumishi wananyanyasika sana, wanamchonganisha mama kwa makusudi na watumishi wa umma wazalendo wanaofanya kazi kubwa katika mazingira magumu. Lazima mamlaka za juu ziunde chombo au kamati ipite nchi nzima kusikiliza kero za watumishi, Hali ni mbaya mnoo katika Halmashauri, wakurugenzi wao wamekua ni miungu watu.
 
Niliona sehemu, Mwalimu Nyerere alishawahi kusema kuwa "Ukiona msomi anatendewa jambo baya bila kuhoji, ujue taifa linatengeneza wasomi wajinga" Kwa hatua hii, hata wanafunzi wanaofundishwa na walimu wa aina hii watakuwa na self-confidence. Ogopa mwl mwoga hawezi kumfundisha mtoto ujasiri na kujiamini.
Walimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wameamua kugeukia Mahakama ili kudai haki yao baada ya Mkurugenzi wao, Ndugu Maiko Kachoma, kukaidi matakwa ya sheria na kupuuza maombi yao. Walimu hao, zaidi ya 150, wamempa notisi ya siku tisini kuhakikisha kuwa amekamilisha mchakato wa kuwatoa katika Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na kuwaunganisha na Chama cha Walimu Chakuhawata. Notisi hiyo inamtaka Ndugu Kachoma kushughulikia suala hilo mara moja, la sivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake kwa gharama zake mwenyewe.

Inasikitisha kuona baadhi ya wakurugenzi, walioteuliwa kusimamia watumishi wa umma na kufuata sheria za nchi, wanageuka kuwa viongozi wenye kiburi na dharau. Ndugu Maiko Kachoma amejitwalia mamlaka makubwa kiasi cha kuonekana kama "Mungu mtu," akiwataka walimu wamuabudu ili awatekelezee matakwa yao. Hali hii inazua maswali kuhusu vigezo vinavyotumika kuwateua viongozi wa aina hii.

Walimu wamebeba mzigo mkubwa wa kifedha kwa kuchangisha zaidi ya shilingi 5,000 kila mmoja ili kugharamia huduma za kisheria. Fedha hizi, ambazo zingeweza kusaidia familia zao, sasa zimetumika kwa sababu ya ukaidi wa kiongozi mmoja. Ni haki kwamba Ndugu Kachoma atoe fidia kutoka mfukoni mwake kwa View attachment 3266963inashangaza jinsi mtu anayekaidi sheria anaweza kutegemewa kutetea maslahi ya wananchi na kusimamia utungaji wa sheria. Tabia yake ya kiburi na ukaidi si tu inakera, bali pia inahatarisha uhusiano kati ya serikali na watumishi wa umma. Hata ofisini kwake, amekuwa kero kwa watumishi huku akijitambulisha kama "Afisa Kipenyo" au "Afisa Usalama."

Kwa mara nyingine, naomba mamlaka za uteuzi zimwangalie kwa makini Ndugu Maiko Kachoma. Kiburi chake kinazidi kuleta mgawanyiko na kuharibu taswira ya serikali mbele ya watumishi wa umma.

View attachment 3266961
 
Back
Top Bottom