Walinzi wa kampuni ya SUMA JKT GUARD wana matatizo ya kisaikolojia

Walinzi wa kampuni ya SUMA JKT GUARD wana matatizo ya kisaikolojia

Waliwahi niweka mtu kati kuanzia sa8 usiku Hadi sa3 asubuhi!! Utawala wa College of Education kisa chenyewe hakina kichwa Wala miguu, Mbaya zaidi mmoja wao akanipa namba yake aseeeh, Nilimtukana sijawahi tukana Wala kudharau kazi ya mtu Kama nilivyofanya kwa huyo, SUMAJKT
Pole sana mkuu. Nadhani pia mazingira yao ya kazi hayawaruhusu kufikiri sana.

Wanasema ukifikiri sana unampa mhalifu nafasi.
Kuna siku unaweza kutana na mwingine na akakusaidia sana mpaka ukabadili mawazo yako juu yao.
Mimi kuwekwa muda wote huo chini ya uangalizi sijui ningefanyaje dah!

Again, pole sana.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Wengine wapo bandarini pale wanapigishwa vibarua halafu wanalipwa buku sita tu kwa shift.......wakati vibarua wenzao ambao si watu wa suma wanalipwa zaidi ya iyo yani full unyonyaji kutoka kwa mabosi zao....wenyewe wanadai wao hulipwa 50 elfu tu kwa mwezi walitarajia pale bandari wangepata posho sawa na wenzao ili hata wajiendeleze kumbe wakubwa zao wamewageuza kitega uchumi cha kupiga ela za bandari.....
nchi ina mikasa kweli hii
 
Sawa poti
Huwezi kuamini. Suma jkt guard kuna vijana wasomi wazuri tu.
Suma ya miezi hii sio ile Suma ya wakati wanaanza kuchukua tenda za malindo ya kwenye taasisi. Wale wa mwanzo walikua ni wakali sana halafu uelewa wa mambo ulikua ni mdogo sana.

Vijana wenzangu wa Suma JKT guard msikate tamaa ya maisha. Wote hamuwezi kuwa polisi, magereza au JW. Tumieni kipato kidogo mnachopata kujiendeleza kwa fani mbalimbali za stadi za maisha lakini kupata mitaji.

Wengi wenu bado ni vijana wadogo. Nawasihi muache umalaya sio mzuri, kuna ukimwi na homa ya ini. Kuweni makini sana vinginevyo mtakwisha.
 
Umeandika ukweli mtupu chief, hawa vijana walimezeshwa ndoto zenye mafanikio makubwa sana. Hivyo ilipelekea wakawekeza nguvu na akili zote kwenye kujitolea, then leo wamerudi kitaa wakiwa hawana mitaji, hawana ajira na wametoka mikono mitupu.

Wakiangalia wenzao waliokuanao mitaani, shuleni na JKT wamepiga hatua kubwa kimaendeleo....

Lazima wachanganyikiee
Hilo la kwanza, la pili ni namna walivyojiunga!

Wengi kwenye mchakato wa kujiunga walitozwa rushwa kubwa kubwa za kisiri, wakihamasishwa miujiza ya mafanikio pamoja na mambo yote uliyoyaeleza.

Tuseme nyakati zimebadilika pakubwa, enzi za utawala wa awamu ya4, vijana wengi walifanikisha ajira za vyombo mbali mbali vya ulinzi kwa njia hiyo, lakini leo ni tofauti.

Kama mtoa mada alivyosema, vijana hawa wanastahili kuangaliwa kwa jicho la 3, ama mfumo uliopo sasa ubadilishwe, iwe asipoajiriwa apewe kianzio.

Pia muda wote wakaapo chuoni wapewe angalao mshahara wa kiwango cha chini cha mfanyakazi wa serikali kuliko ilivyo sasa posho ya 50,000 wapewayo haitoshi hata kununulia suruali ya cadet.
 
Kwa upande Wangu Mimi naona wakome tu maana watanzania hawataki kujielewa Yani Alie Soma na ambae ajasoma wote no wale wale hamna utofauti

Kwanza nimeamua kua na roho mbaya mbele ya watu wasio jielewa hata kutoa msaada mpaka nikuhoji vyakutosha sio kirahisi rais na kuhusu hao vijana watachanganyikiwa Sana wakimalza hao kuchanganyikiwa

Watafata WAHITIMU wa vyuo mbali mbali maana hawana hata maarifa unakuta WAHITIMU kumi wa engineering wameshndwa hata kubuni kiwanda Cha vikombe vya plastic sasa hapo huruma ya nini

Tena chamsing kila MTU apambane na familia yake tu hawa watu wengne ni kuwakazia tu hakuna ujamaa jamaaa mwsho wake no kurudishana nyuma tu. [emoji41][emoji41][emoji41]
 
yaani wanapopita kusoma nyuzi kama hizi ndio mnazidi kuwatoa kwenye reli.

lakini jamani kwenye hizi kampuni za ulinzi kuna wizi nyiee!!!acheni kabisa.

mtu anaingia tenda ya kulindwa na askari anapigiwa hesabu ya laki 900k kila mlinzi.mlinzi anakuja kukabidhiwa 180k!!kweli!!!!wapo vijana nilikuwa nawahoji wa Guardaworld,wanakatwa mifuko ya hifadhi pesa hazipelekwi huko.

mawaziri mizigo wapo,manaibu mizigo wapo,wakurugenzi wapo,wakuu wa idara gani sijui wapo kazi ni kufuga matumbo na kuvaa miwani tu.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Waliwahi niweka mtu kati kuanzia sa8 usiku Hadi sa3 asubuhi!! Utawala wa College of Education kisa chenyewe hakina kichwa Wala miguu, Mbaya zaidi mmoja wao akanipa namba yake aseeeh, Nilimtukana sijawahi tukana Wala kudharau kazi ya mtu Kama nilivyofanya kwa huyo, SUMAJKT
Siku hizi udom mnalindwa na suma jkt?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SITOSAHAU JKT MKATABA ULIVYOISHA NA TUKALUDISHWA NYUMBANI-- "OP MAGUFULI"

ilikuwa ni mwaka 2016 naelekea kikosi cha mafunzo ya jkt kwenye gali unapiga mwimbo wa darasa -muziki... kozi ikaanza na hatimaye ikamalizika miezi 6 baadaye nkawa service man kikosi furani nyanda za kaskazini kuishi kwa taabu na mawazo ya lini ntapata ajira nkijitazama sina kitu chochote wala home sikuacha chochote ata kuku m1 wa kienyeji....

Miaka mitatu inakata tunasikia tetesi za tarehe furani tunaludi home wenzangu wakawa wanatoloka wanaludi makwao kupambana na vitu.vingine kabla kipenga rasmi hakijaliaa mimi npo nacheki mambo mpaka tone la mwisho hatimaye tukaambiwa tukusanye kila mali ya jeshi haraka iwezekanavyo hapa ni kombati,sahani,kikombe ,kofia na mkanda kama unao

Wasichana wakaanza kulia vilio c vya nchi hiii wanaenda wapi kukaa warudi tena home kukaa wengi hawakurudi mimi nkasema narudi kupambana kitaani kwetu na ntakaa home mpaka nipate mtaji hapa ndo MOVIE inapoanzaa.
mkuu , huu ujumbe kama hujaumalzia asee
 
Kuna kituko hapo Dodoma kwenye stendi zote mbili za mabasi, stendi kuu na pale kwenye soko kuu la Job, wapo hao vijana yaani ni tatizo kwa mustakabali wake!.
 
Habari!

Ukichukua matukio machache yaliyofanywa na hawa vijana wa SUMA JKT GUARD utagundua kuna kitu hakiko sawa. Kuna upepo umepunguza akili zao.

Majuzi Jangwani walimpiga yule jamaa wa African sports na kupelekea kifo chake, tena tunapokea taarifa kuwa wamemuua mwananchi asiye na hatia aliyekuwa akilima shambani kwake karibu na msitu wanaoulinda.

Juzi jioni wakati natoka kazini narudi nyumbani njiani nikakutana na kijana wa suma kabeba Kirungu, manati, pingu na vikorokoro vingine anatembea akiekekea lindoni. Jinsi alivyojifanyia camouflage utadhani yupo vitani kumbe anakwenda kulinda kaeneo kadogo tu.

Wale vijana wa SUMA wengi wao ni vijana wa JKT waliomaliza mikataba yao na kurudi nyumbani bila mitaji. Marafiki zao wengi ni vijana waliokuwa nao JKT ambao sasa ni watumishi wa JWTZ, TISS, ZIMAMOTO , UHAMIAJI, MAGEREZA na POLISI.

Wenzao wanakopa wanajenga, wananunua magari na kusaidia ndugu huku wao vijana wa SUMA wakilipwa kitapeli na kampuni yao ya ulinzi. Take home yao haifiki hata 250k, hawakopesheki benki, ajira yao kufukuzwa ni rahisi, hawana uhakika wa maisha ya uzeeni.
Muda wa kazi ni mwingi.

Hawa vijana wa SUMA wasaidiwe .

Ni vijana waliokosa dira, sasa wamebaki kujitutumua tu ili nao wahesabike kama wanajeshi.

Unajua JKT mtiti wake ni mzito sana, miezi 6 unakula kozi ngumu huku ukiendelea kulima kwa bidii, then umemaliza unaendelea kulimishwa zaidi kila siku. Unavumilia ukijua utafanikiwa mwisho wa siku unapewa nauli tu urudi kwenu, lazima uchanganyikiwe.

Hakuna anayekwenda JKT eti akajitolee tu kisha arudi nyumbani. Basi serikali itoe mitaji kwa vijana wanaotoka JKT bila ajira ya uhakika ili wakaendeleze fani walizojifunza huko makambini. Wa kufuga samaki au kuku akafuge, wa kujenga akajenge n.k
Mkuu umeongea ukweli mtupu kiukweli inasikitisha sana.
Wale watu mshahara wao ni laki 2 na take home ni laki 1 na 80.
Mtu ana mke na mtoto, amepanga room.
Nyuma ya pazia kampuni ya SUMA inavuta mkwanja sio chini ya 500K na baadae inatoa gawio ili isifiwe na watu.

Mwafrika ni kiumbe wa kipekee sana, yaani vijana wananyonnywa ili watu wakatoe gawio wasifiwe tu.

Hivi karibuni serikali ilitangaza kima cha chini cha mshahara ni 270K lakini serikali hiyo hiyo iko kimya watu wanalipwa 180K
 
Back
Top Bottom