Waliogundua hesabu ngumu walikuwa wanatafuta nini na walizigunduaje?

Waliogundua hesabu ngumu walikuwa wanatafuta nini na walizigunduaje?

Sisi tunaumiza vichwa namna ya kupata mahitaji muhimu kama chakula , mavazi na nyumba hayo mengine ni kazi ya wachache walio jaaliwa
Mkuu; Hiyo kuumiza kichwa namna ya kupata mahitaji muhimu.... ndo Hesabu zenyewe! Kila kitu ni Hesabu - hata kulala ni hesabu e.g. Utalala saa ngapi na utaamka saa ngapi ili uweze kutekeleza majukumu yako 1,2,3 n.k. Usipoweka mahesabu yako vizuri utajikuta unakimbia-kimbia tu siku nzima na umri unaenda. Time and Tide waits for no man. Hesabu hutumika mpaka kaburini😲 - huwezi kuacha kutumia Hesabu alimradi upo na unaishi. Hebu fikiria kwa case ya COVID-19 Je, wasingetumia hesabu kwamba mgonjwa apewe oxygen kiasi gani si wangekubugiza hewa hiyo tuu na matokeo yangekuwa mabaya kuliko COVID yenyewe? Hesabu/Mathematics ni somo TAKATIFU na linatawala masomo mengine yote- yooote kabisa( na fani zote hata Uchungaji). Ndo maana kila course yoyote/ combinations zote Arts or Science kunakuwapo na somo la Hesabu(Additional or Applied) - Tuipende tu Hesabu aisee hata kama inasumbua kichwa.
 
Ni kwa sababu hujataka kujua... kuna mashine nyingi sana zinafanya kazi kwa hayo mahesabu.
Mkuu; Ile Midude inayotumika katika ujenzi (Cranes) inatumia trigs, Ufanisi wa matumizi ya RPG na Artillery jeshini hutumia sana hizo hesabu mkuu. Sema tu kwamba sisi tunafaidika na matokeo ya matumizi yake lakini hatujishughulishi kutaka kujua imekuwaje hata ikatokea hivyo.
 
Hesabu (Mathematics) ni kitu endelevu. Usiseme ni Mihesabu migumumigumu kwani hakuna kilicho kirahisi-rahisi. Hebu mfikirie naye mkulima wa jembe la mkono anavohangaika - suluba anazopitia- jualake, mvua yake, hatimaye hupata mavuno baada ya miezi mitatu (3 months)au zaidi. Sasa wewe unasolve page nne tu mjomba halafu unataka kukimbia? Acha bhana. Ukifuatilia kwa karibu zaidi utakuta hesabu mpya zipo na zitaendelea kuja kila uchao. Nakutakia kila la kheri Mkuu.
 
Kivipi hebu fafanua mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu; Probability of an Event inahusika. Je, katika tukio hili uwezekano wa kujirudia matokeo yanayolingana au ni mara ngapi jambo hili litatokea au kuonekana kati ya mengine yatakayotokea? mfano mrahisi ukiulizwa: hebu tabiri kwamba; ukienda Ulaya unadhani kati ya Watu utakaokutana nao; Mtu mweusi au Mzungu ni kipi kitatokea zaidi kati ya watu utakaokutana nao kwa siku hiyo moja? Si utasema ni Mzungu? Kwa nini au Umejuaje? Samahani lakini kama nime ku-mislead au sikujibu swali lako kama ulivyotarajia- nayo ni probability!
 
Back
Top Bottom