Waliopigania uhuru wa Tanganyika Walipigana na nani?

Waliopigania uhuru wa Tanganyika Walipigana na nani?

Hi Great thinkers.

Nafikiri kuna jambo haliko sawa hasa tunaposema tulipigania uhuru. Tulipigana na nani.?

Mi navojua ule ulikuwa ni mchakato wa kupata uhuru wa Tanganyika, Na hakuna mtu aliyegoma kutupatia uhuru eti hadi tuanze kupigania.

Ni bora isemwe tu kwamba walioongoza harakati za kupata uhuru wa Tanganyika na siyo kupigana .

Labda kama ni sielewo kiwahili vizuri kati ya harakati/Kupigana.
Wapigania Uhuru wa nchi yetu walianza harakati za kupigania Uhuru wa nchi yetu mara tu baada ya uvamizi wa kikoloni barani Afrika

Baadhi ya wapigania Uhuru kabla ya vita ya pili ya dunia ni kama Kijenkitile Ngwale,Mkwawa,Mtemi Isike,Abushiri na wengineo

Baada ya vita ya pili ya dunia wapigania Uhuru wengine walijitokeza akina Nyerere ambaye alihamasisha watanganyika kuungana na kudai uhuru wa kweli ili waafrika tujitawale moja kwa moja na kujitegemea

Nyerere alipigania uhuru wa Tanganyika kwa kuwaunganisha watanganyika kuwa kitu kimoja na kupinga janja janja za wakoloni kutaka kukabidhi Uhuru kwa vibaraka wao akina Zuberi Mtemvu

Kupigania siyo lazima uchukue mtutu,hata kwa kelele au hamasa ni kupigania Uhuru pia na shukuru vita ya kwanza ya dunia ikawepo sidhani kama mjerumani angekabidhi Uhuru kwa amani
 
Hi Great thinkers.

Nafikiri kuna jambo haliko sawa hasa tunaposema tulipigania uhuru. Tulipigana na nani.?

Mi navojua ule ulikuwa ni mchakato wa kupata uhuru wa Tanganyika, Na hakuna mtu aliyegoma kutupatia uhuru eti hadi tuanze kupigania.

Ni bora isemwe tu kwamba walioongoza harakati za kupata uhuru wa Tanganyika na siyo kupigana .

Labda kama ni sielewo kiwahili vizuri kati ya harakati/Kupigana.
nakuona unavyopambana kuelewa.....

Jana yanga walipigana kiume sana aisee....
 
Naona hata heshima kwa jeshi letu pendwa ipo chini, hakuna mission yoyote kali ambayo unaeza simulia mtu, kina mayunga wangepaswa wawe hata 100 lakini matokeo yake tuna kanali anauawa kwa visu na dereva bajaji 😂😂

Uhuru wa kupewa, hakuna uhuru wapiganiwa kama china na Japan, India na England

Jeshi letu limebakia kwenda Zanzibar kutishia raia kipindi Cha uchaguzi mkuu basi. Hawana la maana.
 
Kuna kitu kinaitwa maana kutokana na muktadha (contextual meaning) Kuna watu wanapigania uhai wodini, Kuna watu wanapigania ndoa zao Kuna watu wanapigania mapenzi na wengine Wana pigania familia zao na wewe upo hapa unapigania ujinga
 
Kuna kitu kinaitwa maana kutokana na muktadha (contextual meaning) Kuna watu wanapigania uhai wodini, Kuna watu wanapigania ndoa zao Kuna watu wanapigania mapenzi na wengine Wana pigania familia zao na wewe upo hapa unapigania ujinga

Vijana wa siku hizi usipoteze muda wako kuwaelezea jambo.

Huko shuleni walisoma Vita Baridi na hapakuwa na mapigano ya silaha. Wao wanachojua kupigana lazima ngumi, silaha na damu zihusike
 
Imagine miaka 60 sasa tuna taifa la majoga ....hakuna elimu wala kujitambua...hatuwezi kusimamia haki yetu kama Taifa....sembuse miaka hiyo.....walijitahidi sana wale wazee sasa tuna key boardworriors
Kabisa mkuu, alafu kuna jamaa anawadharau hapa.
 
Mi mwenyewe hii kitu hua siielewi ni bora hata zanzibar walitegea mwarabu amefunga ana swaum kali akakianzisha wakafanya mapinduzi sasa sisi hamna hata mzungu mmoja alipigwa hata ngumi moja ya pua atleast tuone damu eti tunajisifu tulipigania uhuru.
 
Back
Top Bottom