Walioteuliwa na SSH wote wamemshukuru kupitia mitandao ya kijamii, Makonda pekee ndiye kama amegoma kushukuru kwa uteuzi

Walioteuliwa na SSH wote wamemshukuru kupitia mitandao ya kijamii, Makonda pekee ndiye kama amegoma kushukuru kwa uteuzi

Nimepitia mitandao ya kijamii ya walioteliwa wote, wameonyesha furaha na shukrani.

Makonda ni kama kichwa gia zinaruka, mpaka sasa haamini kama hayupo jikoni, kapelekwa akakusanye kuni, hajatoa neno la shukrani.
Matarajio yanapopishana na matokeo
 
Nakuona namna unavyoweweseka na kuhangaika sana katika kujaribu kumchafua Mheshimiwa Makonda. Hata hivyo hutafanikiwa kwa namna na njia ya aina yoyote ile.Makonda ni mwamba na kila mtu anafahamu uchapakazi wake na uzalendo wake kwa Taifa letu. Anafahamu upendo mkubwa na heshima kubwa aliyonayo kwa Mheshimiwa Rais na namna ambavyo amekuwa tayari kufanya na kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais . Nakukumbusha tu ya kuwa Mheshimiwa Makonda ndio mtu pekee aliyemtabiliaga Mheshimiwa Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan kuwa Makamu wa Rais na na mwanamke wa kwanza kushika nafasi hiyo katika Taifa letu na kweli ikaja kutokea hivyo. Kwa hiyo huwezi kutuambia wala kutupandikiza chuki kwa Mheshimiwa Makonda maana tunamfahamu sana uzalendo wake.
Bado hujasema.....
 
Nimepitia mitandao ya kijamii ya walioteliwa wote, wameonyesha furaha na shukrani.

Makonda ni kama kichwa gia zinaruka, mpaka sasa haamini kama hayupo jikoni, kapelekwa akakusanye kuni, hajatoa neno la shukrani.
nadhani ile muhimu zaid,
ni kijana Comrade Paul Makonda kwenda kufanya kazi maalum alopangiwa na kuelekezwa, kwa umakini sana, umahiri na weledi wa kiwango cha juu sana ili mambo yasonge kama yalivyokusudiwa 🐒
 
Endelea kuweweseka na kuhangaika na mheshimiwa Makonda wakati akiendelea kuchanja mbuga katika mioyo ya watanzania
Kuchanja mbuga tu, bado, atachanja mpaka kuni, CCM hatutaki majitu mahuni mahuni
 
Ma-mafia wa A-town wamesogezewa mpira miguuni. Kazi kwao sasa kufunga goli kimafia.
 
Kushukuri rais ni utumwa na ulofa wa kiwango Cha PhD.anayeshukuriwa ni Mungu pekee
 
Nimepitia mitandao ya kijamii ya walioteliwa wote, wameonyesha furaha na shukrani.

Makonda ni kama kichwa gia zinaruka, mpaka sasa haamini kama hayupo jikoni, kapelekwa akakusanye kuni, hajatoa neno la shukrani.
Usihangaike na makonda, yeye tayar ameshachora ramani ya ushindi . Utajua 2025. He is coming very strong
 
WanaArusha wapo tayari kufichua madudu yote mbele ya makonda

Nashukuru mama Kwa teuzi hii iliyotukuka
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Unaumia sana kwa Makonda!?

Unapiga majungu ila yeye anazidi kupaaa!

Ni kama mamako anakupuuza tu
Kupata vyeo vya hisani nayo ni kupaa?! Nimecheka vibaya.😂
 
Nimepitia mitandao ya kijamii ya walioteliwa wote, wameonyesha furaha na shukrani.

Makonda ni kama kichwa gia zinaruka, mpaka sasa haamini kama hayupo jikoni, kapelekwa akakusanye kuni, hajatoa neno la shukrani.

Kwa hiyo shukran zinapitia kwenye mitandao ya kijamii?
 
Mlima umegeuzwa kichuguu daadeq. Na Bado!

Mama anaendelea kuupiga mwingi....
Nakumbuka toka anafariki jiwe ulikuwa unakataa viuno eti sukuma gang inakomeshwa!
.
Ila matokeo yake ni tofauti kabisa! Sabaya soon anakuja kuwapelekea moto tena.
 
Back
Top Bottom