Walipoanzisha Mpango wa biashara ya saa 24 Kariakoo walidhani nani atakesha na atamuuzia nani?

umejichokea sikuhizi hunahata mvuto wacha jiji lifunguke kibiashara wewe nenda kamshauri lissu jinsi ya kueneza no reform no election kitu kilicho feli toka kimeanzishwa
 
Ishu sio kuzoea, tuache kujipa moyo kizembe kuwa huu ni mwanzo tu na watu watazoea.

Kinachotakiwa ni kuboresha mazingira, wangeona na kujifunza kutoka kwa nchi ambazo watu wanafanya biashara masaa 24 waone jinsi mazingira yalivyo.
 
Pingapinga Fc at work.
 
Wanafanya tu maamuzi ya kukurupuka bila kushirikisha ubongo ili wapate sifa
 
Yule kidomodomo wa kinyaru ajitokeze kutoa utetezi wake
 
Binafsi nitaanza kwenda kariakoo usiku, huwa sipiti kariakoo sipendi zile purukushani.

Zamani wakati mtaa wa Congo wanauza Sangara kabla wauza mitumba kuvamia nilikuwa naenda kula pilau pale club ya nyota nyekundu, lile jengo wajanja wameshalinywa sasa limebomolewa kuna ghorofa jipya la Bazaar.

Usijifijirie wewe tu kuna watu wanatoka mikoani anataka afunge mzigo kesho ageuge, kuna Wacongo na Wazambia wanategemea kariakoo hii ni fursa nzuri kwao.

Ukifika Johannesbur uptown Hillbrow hapo ni pilika 24 hours.

Sasa Polisi ule ushamba wao wa kutusumbuwa kwenye mapub usiku tukiwa tunachangia pato la Taifa wahamishie nguvu zao kufanya patrol kariakoo.
 
Hongera kwa kula pilau saa 9 Alfajiri Mtaa wa Congo
 
Ila nadhani ni Swala la muda tu na kuna baadhi ya Mambo yanapaswa kuwa sawa.

Mfano usafiri wa uhakuka wa maeneo yote Hasa mwendokasi , Pili kuboresha au kuongeza security Systems kama Cctv maeneo yote mpaka huko Buza na Kuhakikisha Mataa ya kutosha kila mahali. Nadhani baada ya hapo utaanza kuona watu wanaanza kuzoea Taratibu.

Mimi binafsi ni Bora nikaenda Kariakoo Usiku wa manane kuliko Mchana na Hili jua la daslamu.

Natamani sana Hii issue ifanikiwe. Mchana jua ni kali sana jamani
 
Hatuwrzi kupinga kila kitu, nyakati zinatutaka bi yo.

Sinza hata ukihitaji spare ya gari usiku kuna maduka yapo wazi
 
Ni suala la mda tuu na kuzoea unadhani itakuwa overnight full business? Tumia akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…