#COVID19 Walitumia nguvu kubwa kuwatisha watu juu ya chanjo, leo wanashangaa wananchi kuogopa chanjo

#COVID19 Walitumia nguvu kubwa kuwatisha watu juu ya chanjo, leo wanashangaa wananchi kuogopa chanjo

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Toka chanjo imetoka, serikali chini ya Magufuli imekuwa inaweka hofu kwa wananchi juu ya usalama wa chanjo. Rais alisema waziwazi kauli za kupinga chanjo. Alisema kama wazungu wanaweza kutengeneza chanjo basi wangetengeneza chanjo ya UKIMWI. Watu kama Kigwangalla wakatoa kauli kupinga chanjo kijanja.

Wakiunga mkono malimao na sauna kuwa ni salama huku wakipinga usalama wa chanjo. Gwajima askofu akapiga kelele bungeni kupinga chanjo huku Gwajima daktari akipiga meza kwa nguvu na kutingisha kichwa kuunga mkono. Na waliwaaminisha ugonjwa huo haupo Tz, wanafikiri ni rahisi kuwaaminisha watz kuwa upo te

Baadaye kidogo ndiyo wakaja na habari kuwa wanasubiri wataalamu wa ndani wapitie chanjo kuona kama ni salama. Ghafla bila hata kusema huo utafiti wa wataalamu wa ndani umesemaje wanaanza kuwaaminisha wananchi kuwa chanjo ni salama, na kushangaa watu kupinga kuchanjwa.

Watanzania hawajawahi tilia shaka usalama wa dawa wala chanjo mpaka serikali ilipoanzisha hilo. Serikali inabidi iombe msamaha kuwa ilikosea namna ya kupambana na Korona, na iwekeze nguvu kweli kuwapa watu elimu na kuwaaminisha watu kuwa chanjo ni kitu kizuri, na si stunts za kina Gwajima daktari kukimbia.
 
Ni hiari sio lazima,watu wengine watachanja hasa wanaosafiri nje ya nchi.
Lengo la chanjo sio kwa ajili watu wansafiri nje ya nchi Bali ni kuzuia ugonjwa wa corona.

Nakuweka sawa hapo, maana naona hata raisi nae anakazania kuwa ooh watu wanafanya biashara nje ya nchi hivyo ni muhimu chanjo ziwepo.

Mnapotosha sana, lengo la chanjo ni kuzuia corona na sio eti kwa ajili ya wanaoenda nje ya nchi
 
Lengo la chanjo sio kwa ajili watu wansafiri nje ya nchi Bali ni kuzuia ugonjwa wa corona.
Nakuweka sawa hapo, maana naona hata raisi nae anakazania kuwa ooh watu wanafanya biashara nje ya nchi hivyo ni muhimu chanjo ziwepo.
Mnapotosha sana, lengo la chanjo ni kuzuia corona na sio eti kwa ajili ya wanaoenda nje ya nchi
Huwezi kupita mkuu bila chanjo!Jaribu uone kutaka kwenda nje,ndo utapata jibu.
 
Lengo la chanjo sio kwa ajili watu wansafiri nje ya nchi Bali ni kuzuia ugonjwa wa corona.
Nakuweka sawa hapo, maana naona hata raisi nae anakazania kuwa ooh watu wanafanya biashara nje ya nchi hivyo ni muhimu chanjo ziwepo.
Mnapotosha sana, lengo la chanjo ni kuzuia corona na sio eti kwa ajili ya wanaoenda nje ya nchi
Wanachoshindwa kuelewa watu wengi ni kuwa, iwapo watakaochanja watakuwa wachache sana, then chanjo zitakuwa hazina maana yoyote, na hapo ndio utasikia sasa serikali inakuja juu na kulazimisha chanjo. Mwisho wa siku ili kuweza kweli kupambana na corona ni lazima wengi wachanje.
 
Wanachoshindwa kuelewa watu wengi ni kuwa, iwapo watakaochanja watakuwa wachache sana, then chanjo zitakuwa hazina maana yoyote, na hapo ndio utasikia sasa serikali inakuja juu na kulazimisha chanjo. Mwisho wa siku ili kuweza kweli kupambana na corona ni lazima wengi wachanje.
ni kweli maana wale wasiochanjwa watakuwa ni mazalia ya strains zisizosikia chanjo.
 
Mie naona maarifa ya awali jinsi yalivyofubaza maarifa mapya kuwaingia,

Endapo maarifa ya awali yangekuwa chanya nazani Jambo hili lisingetumia nguvu kubwa katika kulitekeleza,
 
Wote mnaosupport hii chanjo kama itakuwa na madhara hakika mtajibu kwa MUNGU.
 
At least umeelezea tatizo kwa upana wake na namna ya kutafuta ufumbuzi (elimu iongezwe kuhusu mambo ya chanjo na kukiri kwamba tulikosea toka mwanzo)
 
Mie naona maarifa ya awali jinsi yalivyofubaza maarifa mapya kuwaingia,

Endapo maarifa ya awali yangekuwa chanya nazani Jambo hili lisingetumia nguvu kubwa katika kulitekeleza,
Kwahio kama ni kudhurika tungedhurika bila kujua? Dah.
 
Ni kweli, serikali iombe radhi hadharani kuwa walikengeuka na walipotosha…. wasitubebe ujinga na kuanza kuanza kutushangaa tulioamua kuamini kauli zao ambazo hawajazifuta.
 
Hili nalo neno!!!! Ni kweli kabisa waliaminisha sana watu kuwa chanjo ni njama za mabeberu kutumaliza!!! Sasa hivi ngumu kumeza kuwa mabeberu hawataki kutumaliza ila wanatusaidia!!!!
 
Toka chanjo imetoka, serikali chini ya Magufuli imekuwa inaweka hofu kwa wananchi juu ya usalama wa chanjo. Rais alisema waziwazi kauli za kupinga chanjo. Alisema kama wazungu wanaweza kutengeneza chanjo basi wangetengeneza chanjo ya UKIMWI. Watu kama Kigwangalla wakatoa kauli kupinga chanjo kijanja.
Wakiunga mkono malimao na sauna kuwa ni salama huku wakipinga usalama wa chanjo. Gwajima askofu akapiga kelele bungeni kupinga chanjo huku Gwajima daktari akipiga meza kwa nguvu na kutingisha kichwa kuunga mkono. Na waliwaaminisha ugonjwa huo haupo Tz, wanafikiri ni rahisi kuwaaminisha watz kuwa upo te

Baadaye kidogo ndiyo wakaja na habari kuwa wanasubiri wataalamu wa ndani wapitie chanjo kuona kama ni salama. Ghafla bila hata kusema huo utafiti wa wataalamu wa ndani umesemaje wanaanza kuwaaminisha wananchi kuwa chanjo ni salama, na kushangaa watu kupinga kuchanjwa.

Watanzania hawajawahi tilia shaka usalama wa dawa wala chanjo mpaka serikali ilipoanzisha hilo. Serikali inabidi iombe msamaha kuwa ilikosea namna ya kupambana na Korona, na iwekeze nguvu kweli kuwapa watu elimu na kuwaaminisha watu kuwa chanjo ni kitu kizuri, na si stunts za kina Gwajima daktari kukimbia.
elimu gani itolewe kuhusu ugonjwa huu wa ajabu, ww unaijua corona unajua hata chanzo chake. Umewahi hata kukohoa kama hujawahi tulia. Kama umewahi nenda kapate chanjo. Watu hawahitaji elimu kila mtu inailewa corona
 
elimu gani itolewe kuhusu ugonjwa huu wa ajabu, ww unaijua corona unajua hata chanzo chake. Umewahi hata kukohoa kama hujawahi tulia. Kama umewahi nenda kapate chanjo. Watu hawahitaji elimu kila mtu inailewa corona
Corona siyo ugonjwa wa ajabu.
 
Back
Top Bottom