Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Tungekuwa na idadi ndogo ya watu mbinu zingekuwa ni nyingine. Hiyo ecology ikivurugika kabisa sisi ndio tutakaokuwa wa kwanza kuilaumu serikali.Naona unatamka tuu sayansi bila kujua inahusu nini.
Hujui kuwa kuna njia za kisayansi endelevu zinazoweza kutumika hata bila ya kufanya hayo inayotaka kufanya serikali, huku 'ecology' ya eneo hilo ikihifadhiwa?
Kwa misingi hiyo, una maana nchi zisokuwa na sehemu kubwa za watu kuishi, wao waanze kupunguza raia zake ili kulinda 'ecology'?
Mkuu, hili jambo lijadiliwe nje ya siasa hizi za siku hizi.Tungekuwa na idadi ndogo ya watu mbinu zingekuwa ni nyingine. Hiyo ecology ikivurugika kabisa sisi ndio tutakaokuwa wa kwanza kuilaumu serikali.
Kwa masikitiko makubwa sana ninakubaliana nawe moja kwa moja juu ya haya uliyoandika hapa.Kwa katiba hii mtu anaweza kuiuza Tanganyika halafu akaenda kuishi zake Zanzibar ama Oman na asishitaiiwe popote wala kuhojiwa.
Kabisa, kwanza wa shenzi tuPale sio kwa wamasai ni ardhi ya wahadzabe waliohamishiwa wilaya nyingine. Wamasai walihamia pale 1959.
Mnavyowatetea wamasai utadhani ni watu wenye kuheshimu tamaduni za wengine. Ni jamii ya hovyo sana.
Kwa katiba hii mtu anaweza kuiuza Tanganyika halafu akaenda kuishi zake Zanzibar ama Oman na asishitaiiwe popote wala kuhojiwa.
Hawa wazanzibar mpaka watoke madarakani, tanganyika itakuwa hoi bin taabani.
Hili suala analopambana nalo Samia lilikuwa limalizwe na utawala wa awamu ya pilii ya Mzee Mwinyi miaka ile 1990.Mkuu, hili jambo lijadiliwe nje ya siasa hizi za siku hizi.
Hakuna asiyependa uhifadhi. Hakuna anyependa kuvuruga 'ecology'; kila mmoja wetu anaelewa umuhimu wake. Kwa hiyo hili swala halipingiki.
Kinachoudhi ni haya mambo mengine ya nayojitokeza kuwa ndiyo kichocheo cha watu kuyumbishwa hovyo.
Hakuna sababu ya serikali kuonekana kutokuwa wawazi kwa wananchi wao.
Watu wa kwanza kabisa ambao wangeelezwa juu ya hiyo 'ecology', ni hao hao wananchi wanaoishi huko mika yote tokea wazaliwe.
Hawa ndio wangekuwa watu wa mwanzo kabisa kupambania raslimali hii isiharibiwe, na wao wenyewe ndio wangekuwa ni walinzi namba moja wa raslimali hiyo.
Hali ni tofauti kabisa, serikali inaamini kutumia uongo, na uongo ukikataliwa, wanatumia mabavu!
Ninaamini kabisa, kuwashirikisha wananchi kungefanya hali kuwa rahisi zaidi; lakini serikali haifanyi hivyo kwa sababu kuna watu wenye maslahi yao humo. Hili ndilo kosa kubwa.
Mara nyingi sana mnashindwa vita kwa kuwa katikati ya vita mnajikuta mnaonesha kilicho nyuma ya mnachopiganiaHawa wazanzibar mpaka watoke madarakani, tanganyika itakuwa hoi bin taabani.
Kuna uzi mmoja uliuliza watu wakati wa msiba wa Mwalimu Nyerere mwaka 1999 ulikuwa wapi?. Siku ile ndio nilijua wengi humu ndani ni vijana wadogo.Mara nyingi sana mnashindwa vita kwa kuwa katikati ya vita mnajikuta mnaonesha kilicho nyuma ya mnachopigania
Na katika muda wote ule wa ucheleweshaji hawakuweza kuona njia nzuri mbadala za kulifanya bila kuonekana kuwa la kilaghai lghai kama linavyoonekana sasa?Hili suala analopambana nalo Samia lilikuwa limalizwe na utawala wa awamu ya pilii ya Mzee Mwinyi miaka ile 1990.
Waliahirisha tu, hivyo kinachoendelea ni lazima kilikuwa kifanyike.
Ni katiba ya hovyo snKama katiba ingelikuwa nzuri. Wa-Loliondo wasingeondoka kwenye ardhi ya mababu zao. Zuio la kimahakama lingewekwa na rais angeburuzwa mahakamani.
Lakn katiba yetu inamlinda rais kuhojiwa na kushitakiwa na chombo chochote kwa kosa lolote atakalolitenda akiwa anatekeleza kazi zake za urais.
Yaani rais Samia anaweza kushitakiwa na mumewe kwa kutofua nguo na kuosha vyombo nyumbani lkn akiharibu kazi ya urais haguswi. Hatari Sana!
Kwa katiba hii atatokea rais chizi awafurushe watu wa kabila fulani waondoke nchi hii. Kama ilivyotokea kwa warohingya kule Myamar.
Tutengeneze katiba nzuri yenye meno inayojilinda yenyewe. Asiwepo mtu wa kucheza na katiba. Iwe inamkata kila anayejaribu kuigusa vibaya.
GoodNaona unatamka tuu sayansi bila kujua inahusu nini.
Hujui kuwa kuna njia za kisayansi endelevu zinazoweza kutumika hata bila ya kufanya hayo inayotaka kufanya serikali, huku 'ecology' ya eneo hilo ikihifadhiwa?
Kwa misingi hiyo, una maana nchi zisokuwa na sehemu kubwa za watu kuishi, wao waanze kupunguza raia zake ili kulinda 'ecology'?
Mazingira ya kisiasa yangeruhusu wewe Kalamu usingekuja na hoja hizi. Kazi ya urais ni ngumu sana, hata ukiamua kugawa biskuti na chakula cha mchana kwa kila mtanzania utatafutiwa kona ya lawama.Na katika muda wote ule wa ucheleweshaji hawakuweza kuona njia nzuri mbadala za kulifanya bila kuonekana kuwa la kilaghai lghai kama linavyoonekana sasa?
Hata kule kuwaelemisha wananchi tu, kuwaanda vyema ili misuguano isiwe mikubwa hawakuweza; ila wakaona wasubiri tu kuwauza wananchi hawa kwa mwekezaji?
Ninaweza kuelewa ucheleweshaji huo wa wakati huo, kwamba mazingira hayakuruhusu kisiasa kufanya kazi hiyo. Pengine wangeifanya wakati huo, sasa hivi tungekuwa ni tofauti sana, kwani huenda hata CCM isingekuwepo leo.