Wamiliki shule za EMs waumizwa na mtaala Mpya. Wazazi wengi sasa wanawatoa watoto Wao shule za EMs kiwarejesha Kayumba

Tafuta pesa upeleke mtoto wako shule nzuri. Mtu mwenye uchumi mzuri hawezi peleka mtoto wake Kayumba school.

Mtaala mpya haujabadili lolote la kufanya English Medium schools zikose relevance.
Shule za serikali bado kuna changamoto za kutosha. Kwa mfano Kuna shule moja huko Mbagala Darasa moja lina wanafunzi 700. Kila mkondo wanafunzi takribani 100.
 
Nimefurahi sana ndoto yangu ya kuandikishwa la kwanza 2025 imetimia changamoto nintutoto kunivutavuta ndevu tukinnita babu
 
Shule za serikali bado kuna changamoto za kutosha. Kwa mfano Kuna shule moja huko Mbagala Darasa moja lina wanafunzi 700. Kila mkondo wanafunzi takribani 100.
700 au 70 mkuu?
700 hilo darasa kama uwanja wa mpira ama!?
 
English medium schools ni hizi ; Tanganyika international school, Shaban Robert, Olympio, Moshi international school, etc. Kama mtoto wako hasomi hizo hapo, jua unasomesha mtoto wako St. Kayumba B🤣🤣🤣
St Kayumba iliyochangamka 😅😅😅
 
Kuna medium jirani na nilipo ....wamejaza Hadi wanawakataa watoto....ni uchumi wako tu ndo unafanya uwaze tofaut
 
Mtaala unataka mzazi/ mwalimu wahakikishe form one anachagua tahasusi anayoipenda mfano michezo kilimo, ufundi biashara n.k asome hicho anachokitaka hadi form 4.

Hio January waalimu wenyewe hawawajui wanafunzi, wazazi wanachojua mwanangu asome sekondari, kila mwanafunzi akiulizwa anataka kuwanani utasikia.... injinia. Hakuna anahetaka mziki, michezo Wala kilimo

Muulize mzazi wa form one, mtoto wako afanye kazi gani baadae... Utasikia .. aendeshe ndege!!! Atakapo kutana na physics form three ndio atagundua kumbe anatakiwa kuendesa bodaboda badala ya ndege
 
September 2024 ulikuja hivi


Leo tena umekuja kivingine tena
 
700 au 70 mkuu?
700 hilo darasa kama uwanja wa mpira ama!?
Ni 700 sio 70. Yaani 70 hadi 100 ni idadi ya mkondo mmoja. Jaribu kuwaza mwalimu anayefundisha darasa lenye wanafunzi 100. Hata matokeo ya darasa la 7 mwaka jana ya hiyo shule wengi wamepata alama wastani wa C na D. Waliopata wastani wa daraja A hawazidi 10.
 
Wakati huo watoto wa wenzako wakilamba teuzi za ukurugenzi wa mashirika na ukuu wa mikoa.

Wewe mtoto wako yuko dukani anahesabu vijisenti.
Mashirika yako mangapi na wanaosoma wapo wangapi??? Ukuu wa mkoa wenyewe sahau kabisaa.
Namtengenezea mwanangu misingi ya kujitegemea na sio kuwa chawa wa wanasiasa
 
Hahaha
Kataa ndoa, single mothers, English medium schools....
Kanyaga twende!!!!
What next????
Tunasubiri....
Ila Tanzanians tupige kazi jamani, kila mtu Kwa nafasi yake...
Aina za posts tu zinasadifu kinachoendelea nchini.
Ha ha ha Ikifuatia kauli kataa uvivu na umaskini tufanye kazi itakuwa tumefika mahali hakika, hiki kinachoendelea ni kauli tu za wakosaji zinazotafuta justification za wajinga wenzao.
 
Mbona mnatumia nguvu nyingi sana kushawishi watu wapeleke watoto st kayumba?
Tusipangiane maisha Kila mtu acheze ngoma anayoiweza. Acheni ufala
 
Mimi nilikuwa na mtoto wa ndugu yangu ,alichelewa kwenda shulelni basi nikampeleka kayumba kwa kuwa nisingeweza kumwanzisha kg1 kutokana na age yake ems walikataa kumpokea.Kweli kayumba vitu vyao basic wanafundisha ni kusoma kwa kiswahili na kuhesabu.Baadae first born wanguni nikampeleka ems.huko kwa kweli wanafundishwa mambo mengi ,na mtoto anajua reasoning na kufanya vitu kwa logic kuliko yule wa kayumba,huko sisikii kuwa mtoto kaibiwa pencil,Wala daftari Kila siku anarudi na homework yake.lakini kayumba lazima daily usikie wameiba peni,kama sio peni basi daftari moja Hana,
 

Unajua kuna tatizo la msingi lilikuwepo kwenye ajira za waalimu wa shule za msingi huko miaka ya nyuma ambapo watu waliajiriwa hovyo hovyo bila kujali anaenda kufundisha somo gani
Matokeo yake somo kama Hesabu halina waalimu huko mashuleni huku somo kama kiswahili/historia nk yakiwa na waalimu zaidi ya mahitaji
Ukitaka kujua ukweli wa ninachokisema, angalia matokeo ya shule za msingi hata miaka 20 mfulululizo, utagundua kuwa, wanafunzi 80%+ wanapata alama sifuri kwenye hesabu kila mwaka.

Vivyo hivyo kwenye Kiingereza, waalimu hawakuangaliwa ufaulu wa somo husika ili wakalifundishe kwa maana hiyo kuna uhaba mkubwa wa waalimu wa Hesabu ukifuatiwa na waalimu wa Kiingereza. Nafikiri Lugha inatumika kutokana na mahitaji; sasa kama wanataka mwalimu wa kufundisha kiingereza watamhoji kwa kiswahili?
 
Rai yangu ni kuwa kila mtu asomeshe mtoto kulingana na hali yake ya kiuchumi, na sio kujiumiza na kujibana ili mtoto asome
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…