Wamiliki shule za EMs waumizwa na mtaala Mpya. Wazazi wengi sasa wanawatoa watoto Wao shule za EMs kiwarejesha Kayumba

Humu Jf naona kuna kikundi cha walimu wa shule za Kayumba na wazazi waliochanganyikiwa na hawana uwezo wa kuwasomesha watoto wao shule za EM kila leo kuanzisha nyuzi za kipuuzi mara waliosoma EMS wasipewe mikopo, mara waliosoma EMS wasipate ajira Serikalini. Ukifuatilia unagundua ni wazazi walioshindwa na walimu wa shule za Serikali wenye wivu.
 
Hahaha
Kataa ndoa, single mothers, English medium schools....
Kanyaga twende!!!!
What next????
Tunasubiri....
Ila Tanzanians tupige kazi jamani, kila mtu Kwa nafasi yake...
Aina za posts tu zinasadifu kinachoendelea nchini.
Miaka mingi kidogo iliyopita ilikuwa 1996 inawezekana ulikuwa haujazaliwa kuna ndugu zangu wa damu kabisa tulikuwa tukihimizana kusoma kwa bidii wakawa wanatoa maneno kama haya wakisema mbona mjomba sijui fulani na fulani kafanikiwa na hakwenda shule, wakaishia la saba B siku hizi wakija kulialia sababu ya kupigwa na maisha sababu hasa ya ujinga nawachana makavu na hela hawapati. SASA KAZA HILO FUVU usisomeshe watoto wako kwenye shule nzuri. WATAKUWA WATUMWA WA WATOTO WANGU. Upopoma hauna mbadala!
 
Acha Urongo wewe!kwa hiyo huko shule za serikali ndio kuna maajabu gani?mwalimu mkuu mwenyewe hata laptop hana
Kwa taarifa yako walimu wakuu wa Kayumba wana hela Kuliko walimu wakuu wa Ems.

How?

Darasa moja Lina wanafunzi mia 7. Mikondo Kumi tofauti.


700 x 7 = 4900.

Hawa watoto kila siku wanaendaga na buku buku za chakula.

1000 x 4900
= Milioni na laki 9.

Ukitoa hela ya chakula Kwa kila darasa na ganji ya waalimu, mwalimu hakosi walau laki 3 Hadi 5 per day.


Anakosaje laptop mwalimu kama huyo?

Unaishi kwa kukariri eeh?

Ticha mkuu wa Ems anasubiria mshahara mwisho wa mwezi
 
Shule nzuri ni Nini?

Shule ni Nini?
 
Walikurupuka kuanzisha shule hizo, hawaku focus hali itakuaje miaka ya mbeleni. Wanaweza kufanya enterprises kubadili biashara kwenye hayo majengo waliyoyafanya shule.
100,% Fact. Wanadilishe matumizi viwe vyuo vya vocational training studies ( Veta)
 
Hapo walipo wanahitaji kurudishwq shule hio mwanga watautoa wapi?
Huwawezi bana they are genius.


Halafu mbona una pingana na dunia nzima?

Dunia Sasa hivi inaondokana na Prussian Education System ambayo na Tanzania tunaitumia.

Au hata hujui Prussian Education System ni Nini?

Wewe unailipia kabisa whats wrong with u?


Go with what is going
 
Hujaeleza Mtaala mpya una Faida ipi kwa Shule za Serikali na Athari ipi kwa Shule binafsi?
 
Unaona akili za kayumba?kumbe watoto wenu wanaenda na buku kila siku kwa mwezi ni 30+30 ya nauli za daladala,+30 ya mitihani yenu ile ya michongo wenyewe wanaziita speed test bado mpo hapa mnajijinadi hamtumii hela?Jan _Apr anayofunga shule mshaliwa kariba 400+,Sawa toa hizo Jumamosi na jumapili bado mnaliwa na elimu yenyewe hakuna....Kimekuramba mzee..............Nikirudi kwa headteacher wa kayumba hana time ya kununua hiyo laptop hata apate mamilioni maana haina kazi,sio jukumu lake anangojea serikali imletee,kama vile vishkwambi vibovu vya sense ealivyogaiwa,Mwalimu aache kulipia ada watoto wake huko EM anununue laptop?sio shida zake
 
Kwanza hakuna umuhimu wa elimu, sio English Medium wala kayumba wote kwa asilimia kubwa wanapoteza muda mwingi wa maisha yao kujifunza vitu ambavyo havina mchango wowote kwenye maisha yao bora watoto wangejivunza kilimo, ufugaji na ujasiriamali
Tunajifunza wapi mzee? Siyo darasani?
 
Wewe mbona unailipia huko Kayumba?kila siku buku 3?
 
Kwanza hakuna umuhimu wa elimu, sio English Medium wala kayumba wote kwa asilimia kubwa wanapoteza muda mwingi wa maisha yao kujifunza vitu ambavyo havina mchango wowote kwenye maisha yao bora watoto wangejivunza kilimo, ufugaji na ujasiriamali
Ndio malengo hasa ya mtaala mpya hongera sana mama samia
 
Acha wajifariji!!!
 
Turudi kwenye Uhalisia

Kwanza Kabisa Serikali haiwezi kutengeneza Mtaala ambao utawafanya hao unaowaita EMs wafunge shule zao kwa sababu moja tu Hizi shule ni msaada mkubwa kwa Serikali, kwa hesabu ndogo tu hebu fikiria hizi.shule zingekuwa hazipo je shule.za serikali zingehimili wingi wa wanafunzi? Kwa maana sasa Wanafunzi.wa shule binafsi na wale wa serikali ni karibu nusu kwa nusu, Madarasa ya kuwatosha yangekuwepo? Walimu wa kutosha wangekuwepo kwwnye Ajira maana wimbo wa walimu wa serikali kila siku ni madarasa hayatoshi wanafunzi wengi... siku hizi.husikii kilio cha madawati kwa sababu mzigo mkubwa umepunguzwa na.shule binafsi...

Pili ni ukweli.usiofichika Ni shule chache sana za serikali zinazotoa elimu nzuri na bora lakini shule nyingi ni bora liende si ajabu huko kukuta mwanafunzi.darasa la 4 hajui kusoma wala kuandika... wakati hapo EMs mwanafunzi.wa chekechea tu anaungurumisha vitu..

Kiufupi kama huwezi jenga ghorofa jenga vyumba viwili usilale nje na kama huwezi peleka mtoto EMs mpleke Kayumba asikose elimu lakini usilete chuki.zisizo na.sababu
 

Shule za EMs hazina wanafunzi wengi. Zina wanafunzi wachache Sana. Nyingi unakuta darasa moja Lina wanafunzi wanane Hadi 15.

So serikali ina uwezo wa kustahimili idadi ya wanafunzi shule za EMs bila wasiwasi wowote.

Elimu bora ni nini?
Kiufupi kama huwezi jenga ghorofa jenga vyumba viwili usilale nje na kama huwezi peleka mtoto EMs mpleke Kayumba asikose elimu lakini usilete chuki.zisizo na.sababu
 
Kila mtu ashinde mechi zake. Mzigo wa sasa ni nafuu ya baadae.

Mpe elimu mtoto kadri ya uwezo wako usijiumize kisa ada ya mtoto.

fainali uzeeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…