Wamiliki wengi wa majokofu/friji wanauelewa mdogo juu ya utendaji kazi wake

Wamiliki wengi wa majokofu/friji wanauelewa mdogo juu ya utendaji kazi wake

Hongera mtoa mada

Ila kuna vitu umechanganya kidogo

Uhalisia ni kwamba

Gesi ikitoka kwenye compresor huwa inashika joto so direct inapitishwa kwenye condensor ili ipoozwe na hata ikipoozwa haiwi na ule ubaridi kabisa, ubarid unatokea kwenye expansion valve

Expansion valve inaletaje ubaridi?

Natolea mfano wa perfume, ukijipulizia perfume kuna kaubaridi fulan huwa unakapata na kale kaubaridi kanazalishwa na ile valve unavyoibonyeza pale ili kujispray, same same to refrigeration system expansion valve ndiyo inazalisha ubarid kwa kuspray freon gas kabla haijaingia kwenye evaporator.

Mengine upo sawa ila hapo tu ndo ulichanganya mtoa mada
Wabongo bhana,
Mtoa mada amesema anatupa maarifa mepesi na uelewa wa kawaida kwa wanaotumia majokofu na viyoyozi ili tuelewe utendaji kazi wa hivyo vifaaa, pia mafundi wasitudanganye na kutuibiaa.

Sasa ndugu yangu hayo mambo ya valvu sijui nini fungua uzi wa mpya kwa ajili ua mafundi
 
Wabongo bhana,
Mtoa mada amesema anatupa maarifa mepesi na uelewa wa kawaida kwa wanaotumia majokofu na viyoyozi ili tuelewe utendaji kazi wa hivyo vifaaa, pia mafundi wasitudanganye na kutuibiaa.
Sasa ndugu yangu hayo mambo ya valvu sijui nini fungua uzi wa mpya kwa ajili ua mafundi
Hii ni elimu huru wapo watakao hitaji kujua zaid kupitia uzi huu. Halaf hyo valve niliyoitaja hapo ni vile umeichukulia poa tu ila nayo ikizingua na ukikutana fundi wa hovyo ataweza kukumalizia hela zako bure.

Thanks in advance
 
Je naweza kutumia freezer kujiomgezea ubaridi ndani wakati wa joto? Yani unalifungulia tu unaacha lifanye kazi yake
Hapana, Hewa ya nje itakapoingia Kwa muda mrefu itadhoofiaha utendaji kazi, Kwahiyo badala ya Friji kutengeneza Baridi litatengeneza joto na litatumia Umeme mara 3 zaidi ya kawaida
 
Hongera mtoa mada

Ila kuna vitu umechanganya kidogo

Uhalisia ni kwamba

Gesi ikitoka kwenye compresor huwa inashika joto so direct inapitishwa kwenye condensor ili ipoozwe na hata ikipoozwa haiwi na ule ubaridi kabisa, ubarid unatokea kwenye expansion valve

Expansion valve inaletaje ubaridi?

Natolea mfano wa perfume, ukijipulizia perfume kuna kaubaridi fulan huwa unakapata na kale kaubaridi kanazalishwa na ile valve unavyoibonyeza pale ili kujispray, same same to refrigeration system expansion valve ndiyo inazalisha ubarid kwa kuspray freon gas kabla haijaingia kwenye evaporator.

Mengine upo sawa ila hapo tu ndo ulichanganya mtoa mada
Shukrani kwa elimu.
Kwangu gesi inaisha na ninajaza kila baada ya miezi 3 au 4, kama wewe ni fundi na upo Dar es salaam au sehemu za karibu, naomba namba yako.
 
Shukrani kwa elimu.
Kwangu gesi inaisha na ninajaza kila baada ya miezi 3 au 4,Kama wewe ni fundi na upo Dar es salaam au sehemu za karibu,naomba namba yako.
Pole sana kiongozi, bahati mbaya sipo huko kwa sasa halafu pia sifanyagi kazi za individual. Ila naweza kukusaidia kutambua leakage

Fanya hiv

Chukua maji weka kwenye ndoo kisha changanya na sabuni (napendekeza ya unga kwasabab ya povu).

Ukishachanganya hakikisha unapata povu jingi.
Pia tafuta sponji au kipande cha godoro.

Washa friji lako na hakikisha compresor inafanya kazi.

Baada ya kuwasha sasa unaweza kuanza kazi ya kuitafuta hiyo leakage

Unachukua lile povu kwa sponji halafu unalikamulia kwenye viungio vyote bila kusahau ile sehem unayoingizia gesi.

Ukishakamulia lile povu kama kuna leakage lazima itaonekana.

Kwa msaada zaid ingekua vema uniambie huwa unaona dalili zipi mpaka unamuita fundi akujazie gesi (mafundi wetu muda mwingne sio waaminifu).

Ref na chiller huwa zina matatizo mengi na mengine yanataka kufanana dalili hivyo ni venga ungefunguka kodogo nikuambie wapi ukaguse kwenye friji lako
 
Shukrani kwa elimu.
Naomba namba ya fundi aje kuziba kwangu,maana inaisha na kujaza kila baada ya miezi 3 au 4.
Pole sana kwa kuingia gharama za mara kwa mara. Nakutumia number ya mtaalamu ninayemuamini mimi. Ana nyenzo na weledi mkubwa tu. Natumai lazima utapata suluhisho.
 
Asante mtoa mada
Kuna mafundi baada ya kugundua kuwa kuna tundu kwenye pipe, wanashauri kununua pipe nyingine na kusuka upya.

Swali langu:
Hakuna njia tofauti ya kuziba ile pipe iliyokuja na jokofu, ukiacha hii ya kusuka upya na kuharibu muonekano wa ndani wa jokofu ?
 
Sawa mtoa mada, ila lengo langu nilitaka ujue kitu unachokichanganya, i hope hii kitu umeitoa darasani ila mm hii mimi haya mambo kila siku nacheza nayo.

Ubard unazalishwa kwenye expansion valve hapa inabd ukubali tu mtoa mada hata kama huelewi ww ameza kama lilivyo.

Kuna mengi kwenye hizi system
Hata mimi kanichanganya sana pia nimeshangaa ameshindwaje hata kusoma hiyo picha aliyoiweka mwenyewe.
 
Pia kama una AC, hapa panakuhusu.

Twende moja kwa moja kwenye mada. Watu wengi tunamiliki majokofu au friji lakini tunauelewa mdogo juu ya utendaji wa hichi kifaa. Kimsingi, kama mtumiaji hautakiwi kuwa na uelewa sana juu ya utendaji wa jokofu lako. Wataalamu au mafundi wanaohudumia jokofu lako wakati wa matatizo ndio wanatakiwa wawe na uelewa na wakupe miongozo mbalimbali juu ya kifaa chako. Kwa bahati mbaya sana, mafundi wengi wa majokofu hawana uelewa huo. Hapa ndipo tatizo linapoanzia na kukulazimu mmiliki wa jokofu uwe na ABC fulani juu ya kifaa chako, kitu ambacho si cha lazima sana. Na hapo ndipo nilipoona kuna haja ya kuleta kwenu uzi huu.

Kiini cha uzi huu ni kuhusu tatizo la ujazaji wa gesi kwenye majokofu yetu Pamoja na AC za majumbani kwetu.

Ili tuweze kuelewana vizuri, naomba nielezee jinsi mfumo wa upoozaji ndani ya jokofu unavyofanya kazi.

Kimsingi mfumo wa upoozaji kwenye jokofu lako una sehemu kuu kama tatu hivi. Yaani COMPRESSOR, CONDENSER, NA EVAPORATOR.

Compressor kazi yake ni kuisukuma gesi iweze kuzunguka kwenye mfumo wa upoozaji. Inaisukuma gesi kwenda kwenye EVAPORATOR, ikitoka kwenye EVAPORATOR inaenda kwenye CONDENSER na kurudi tena kwenye COMPRESSOR, mzunguko unaanza tena na kuendelea. CONDENSER na EVAPORATOR ni mirija au tube katika muundo wa zigizaga zilizotengenezwa kwa shaba au malighafi nyingine yoyote inayoweza kubadilishana jotoridi kwa wepesi kama kielelezo cha mchoro kinavyoonyesha hapo chini.

View attachment 2278705
Wakati gesi inafanya mzunguko au inazungushwa kati ya CONDENSER na EVAPORATOR ndipo inapofanya upoozaji. EVAPORATOR huwa iko ndani ya jokofu, yaani mule kwenye kabati ya baridi. CONDENSOR huwa nje ya jokofu upande wa nyuma. Gesi wakati inazunguka, ikipita kwenye EVAPORATOR inachukua lile joto na kwenda nalo nje kwenye CONDENSOR. Ikifika kwenye CONDENSOR inaliachia lile joto na gesi kuwa imepoa, inarudi tena kwenda kukusanya joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Kwa gesi kufanya mzunguko huo na kazi ya kutoa joto ndani ya jokofu, ndani ya jokofu hubaki na ubaridi. Hapo chini kuna kielelezo cha picha
kikionyesha jinsi mpangilio wa COMPRESSOR, EVAPORATOR, na CONDENSER unavyokuwa kwenye jokofu.



View attachment 2278707

GESI

Tumeona kwamba, gesi kwenye jokofu kazi yake ni kuzunguka, kuchukua joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Inasukumwa kurudi ndani kuchukua tena joto kupitia EVAPORATOR, inakujanalo nje na kuliachia kupitia CONDENSER.

TAMBUA

Katika hali ya kawaida, gesi katika jokofu lako haitakiwi kuisha. Tumeona hapo juu jinsi gesi inavyofanya kazi ndani ya jokofu lako. Haiungui kama mafuta ya gari tuseme kwamba inaisha. Gesi ipo kwenye mzunguko wa mduara ambao umefungwa na hufanya kazi kupitia mirija kama tulivyoelezana hapo juu. Yaani unaweza ukazaliwa mpaka unazeeka, jokofu lako likawa linapoza kama kawaida. Na bahati mbaya sana mafundi wengi wa mifumo ya kupooza hawajui kwamba gesi haitakiwi kuisha katika hali ya kawaida.

Sababu moja kubwa ya kuisha gesi kwenye jokofu ni kuvuja kwa gesi. Pale ambapo kunakuwa na tundu kwenye mfumo wa mzunguko wa gesi na gesi kuanza kuvuja.

Kwanza fundi anatakiwa atatue tatizo la kuvuja kwa gesi ndipo ajaze gesi kwenye kifaa chako. Tofauti na hapo anakupa suluhu ya muda mfupi tu kwa kujaza gesi bila kuzuia kuvuja. Baada ya muda mfupi utamtafuta akujazie tena gesi. Kisheria huu ni wizi. Yawezekana wanafanya makusudi, inawezekana pia hawajui kwamba lazima kutakuwa na tatizo la gesi kuvuja sababu katika hali ya kawaida gesi haitakiwi kuisha. Pia inawezekana fundi anajua ila hataki kujisumbu. Au anajua ila anauhakika hutamlipa gharama za kutafuta leakage au panapovuja.

Kama una jokofu lako ambalo unajaza gesi kila baada ya muda Fulani, sasa ni wakati wa kulitengeneza na kuzuia kuvuja ili kuepuka gharama zisizo za lazima. Fundi anatakiwa atafute gesi inapovujia, adhibiti hiyo sehemu. Baada ya hapo atafanya majaribio ya kuhakiki kama mfumo hauna sehemu inayovujisha gesi. Jaribio hilo atalifanya kabla ya kujaza gesi. Na jaribio hilo la kuhakiki afya ya mfumo linaitwa ‘pressure test’. Baada ya kufanya pressure test na kujiridhisha afya ya mfumo wa upoozaji, atafanya ‘vacuum’. Hapa ataondoa hewa iliyoingia kwenye mfumo wa upoozaji. Sababu baada ya gesi kuvuja na kuisha, hewa ya kawaida huchukua nafasi na kuingia kwenye mfumo. Hii hewa haitakiwi. Endapo gesi itajazwa bila kutoa hewa iliyoingia, ufanisi wa gesi kupooza utapungua na utashangaa kwamba jokofu langu sikuhizi halipoozi vizuri. Ni kama mafuta ya gari uchanganye na kimiminika kingine. Lazima ufanisi wa mafuta utapungua. Ndani ya mfumo wa kupooza inatakiwa iingie gesi peke yake ili ifanye kazi kwa ufanisi wa juu.

Katika pitapita yangu na kukutana na mafundi wa mifumo ya kupooza, sikumbuki kumuona fundi ana ‘vacuum pump’. Yaani pump au kifaa cha kuondolea hewa kwenye mfumo wa kupooza wa jokofu au AC.

Nawatakia upambanaji mwema.



Wakatabahu

Infopaedia
Mkuuu umejitahidi kufungua uzi lakini kuna baadhi ya maelezo nkusahihishe.. nikuhusu refrigerant circle..

Gas ya ac/fridge circle yake ina anzia kwenye compressor, then kwakua compressed gas inakua ya moto, so inabidi ipite kwenye condenser ili kuipoza gas , then inapita kwenye expansion valve au capillary au orifice tube (depends on system design) hapo gas u expand na ku drop temperature na ndipo baridi utokea, sasa gas ile ya baridi ndo inaenda jikusanya kwenye evaporator then ubaridiwa evaporator ndo unapoza compartment ya fridge na kupoza vitu vilivomo ndan ya fridge (so kama fridge ikiwa ni non frost itakua inatumia fan kusambaza ubaridi ulio kwenye evaporator, na kama ni frost basi utakuta pipe za evaporator zimo ndani ya compartment zinazunguka-visible pipea kwa ajili ya kutengeza baridi)... Then gas ikisha toka kwenye evaporator inarudi kwenye compressor kipitia low side pipe , then the circle continues endlessly... But ku-control temperature kuna kua na thermostat.

Kuhisiana na ujazaji wa gas ni kweli kabisa mafundi wengi hawafanyi vacum kutoa moisture na hewa ndani system, na pia hawapimi oil ya compressor vizur, na hawana vipimo vya kupima uwingi wa gasi, na hawatumii gaugesi matokeo yake wakijaza gas performance yake inakua na changamoto.hizi shida zipo hata kwa mafundi AC za magari...na ndo maana hata nikienda kufanya service ya ac ya gari yangu uwa naenda na vifaa vyangu mwenyewe...yaan manifold gauges, oil ya compressor, na condenser, original refrigerant, mzazi wa kupima gas..then namuelekeza fundi afanye vile namuelekeza..


Note; kama unaenda fanya marekebisho ya ac ya gari na gari iliua compressor kwa kuisaga, hiyo gari ili ipone inavotakiwa mi kubadilisha the entire system mpaka pipes..ukijifanya unabadili compressor na condenser alafu una flush evaporator na ac pipes basi ujue ndani ya muda mfuli ile compressor itakufa hata kama una compressor ya pump (fixed displacement compressor) au compressor ya kipumbu (lugha ya mafundi wetu bongo)
 
Asante mtoa mada
Kuna mafundi baada ya kugundua kuwa kuna tundu kwenye pipe, wanashauri kununua pipe nyingine na kusuka upya.

Swali langu:
Hakuna njia tofauti ya kuziba ile pipe iliyokuja na jokofu, ukiacha hii ya kusuka upya na kuharibu muonekano wa ndani wa jokofu ?
Fridge yako ni frost au non frost
 
Nashukuru kwa pongezi kaka. Wakati naandika huu uzi niliwalenga watumiaji wa majokofu. Hivyo sikutaka kuwachosha sana na habari za kitaalamu.
Mkuu Buzitata kazi ya Thermostatic expansion valve ni kuibadili gesi kutoka maji maji na kuwa mvuke. Hii gesi ikiwa katika mfumo wa mvuke ina tabia ya kufyonza joto, hata liwe kidogo italifyonza. Yaani inatabia ya kuhitaji joto ikiwa kwenye mfumo wa mvuke ndani ya evaporator. Baada ya hapo ikipita kwenye compressor huwa imesharudia tena kwenye hali yake ya kimiminika. Na ikiwa kwenye hali ya kimiminika, gesi ya Freon huwa na tabia ya kutoa joto. Yaani inakuwa kinyume na wakati ikiwa kwenye hali ya mvuke. Inakuwa inafyonza au inahitaji zaidi ubaridi. Baada ya hapo inapita tena kwenye expansion valve, expansion valve inaigandamiza na kui-spray ndani ya evaporator kuwa hali ya mvuke na mzunguko unaendelea.
Jokofu hutumia kanuni ya kuondoa joto ili kupata ubaridi. Nikupe mfano wa giza na mwanga. Kwa asili dunia ni giza. Taa au jua likiwaka ndio hulizidi giza japokuwa wakati wote giza lipo. Kinachotokea ni kwamba mwanga unalizidi uwiano giza, basi giza halionekani.
Na kwa habari ya joto na baridi ni hivyo hivyo. Dunia yetu ni baridi isipokuwa msuguwano ndio husababisha joto na kuja kuiondoa baridi, japo baridi wakati wote ipo ila uwiano na joto au jotoridi huegemea upande wa joto hivyo tunahisi joto zaidi. Ama jotoridi ikiegemea upande wa baridi tunasema kuna baridi.
Kwahiyo jokofu hutumia kanuni ya kuliondoa joto, kinachobaki ni ubaridi. Hakuna kitu kinachotengeneza ubaridi kwenye jokofu.
Umeongea kitaalamu lakini unasahau kuwa hizo ni. Chemical reaction za specific elements
Pressure varies diirect proportional to temperature , freon inapokuwa compressed huzalisha joto, ndipo hapo hulazimika kupelekwa kwenye condenser ili ipunguzwe joto, ikitoka hapo ndipo inaenda kwenye expansion valve au evaporator ( ac) , kinachofanyika hapo sasa ndo kinyume cha compression, those freon molecules zinapoachwa huru huwa zina tabia ya kutoa baridi na ndo hasa huleta barafu.
 
Sawa mtoa mada, ila lengo langu nilitaka ujue kitu unachokichanganya, i hope hii kitu umeitoa darasani ila mm hii mimi haya mambo kila siku nacheza nayo.

Ubard unazalishwa kwenye expansion valve hapa inabd ukubali tu mtoa mada hata kama huelewi ww ameza kama lilivyo.

Kuna mengi kwenye hizi system
Ndio sababu tunazisitiza elimu isiwe ya kukariri ili tupate wataalam wazuri , nimemsoma mtoa mada vizuri sana , anajua na kujitahidi , ila kuna vitu unaona kabisa kavimeza kama vilivyo , na hawezi tena kutoka nje ya hiyo knowledge cycle ,
Ubaridi kwenye freezer na fridge unaaznia kutoka kwenye expansion valve ,
 
Ndio sababu tunazisitiza elimu isiwe ya kukariri ili tupate wataalam wazuri , nimemsoma mtoa mada vizuri sana , anajua na kujitahidi , ila kuna vitu unaona kabisa kavimeza kama vilivyo , na hawezi tena kutoka nje ya hiyo knowledge cycle ,
Ubaridi kwenye freezer na fridge unaaznia kutoka kwenye expansion valve ,
Ahsante mkuu kwa kunisaidia maana mtoa mada alishaanza kuniona kirusi.

Mimi kila siku huwa nasema bongo tunachanganya sana kati ya experience na qualification.


Mtoa mada ana qualification ila hana experience ya kitu alichoanzishia uzi ndomaana nilivyo mrekebisha akaanza kuniletea uongo wake wa darasani as if sijui nilichomsahisha.

Siku akibahatika kufanya kazi kwenye plant lazima atakuja kufuta huu uzi wake
 
Naomba mtushauri na fridge nzuri ni lile linaloweka mabarafu au lisiloweka barafu?
 
Naomba mtushauri na fridge nzuri ni lile linaloweka mabarafu au lisiloweka barafu?
Inategemea na aina za kazi unazofanya, non frost ni nzuri na very efficient ila linataka kuwe na umeme wa uhakika ,
Yale ya frost ni ya kizamani na hayapo effiecient ila unaweza ukainjoi barafu hata kama umeme umekatika kwa muda
Kwa matumizi ya nyumbani non frost ipo poa ila kibiashara chukua tu yale ya kuweka barafu
 
Ahsante mkuu kwa kunisaidia maana mtoa mada alishaanza kuniona kirusi.

Mimi kila siku huwa nasema bongo tunachanganya sana kati ya experience na qualification.


Mtoa mada ana qualification ila hana experience ya kitu alichoanzishia uzi ndomaana nilivyo mrekebisha akaanza kuniletea uongo wake wa darasani as if sijui nilichomsahisha.

Siku akibahatika kufanya kazi kwenye plant lazima atakuja kufuta huu uzi wake
Lawama zoote ni mfumo wa elimu unaotukuza pass marks na si uelewa ,
Watoto wapo busy kutafuta past papers na possible questions , unapataje experts kwa mtindo kama huo? Watu wanakariri na kufaulu imeisha hiyo.
 
Back
Top Bottom