Anyone who is mentally and interlectually perfect can describe this person speaking in this voice note as following:
KWANZA: Huyu mzungumzaji he himself a fool 100% lakini hajijui kuwa he's a fool...
PILI: Kwa namna anavyoongea tu, anaonesha wazi kuwa ameumizwa sana na ushindi wa Tundu Lissu na ameumizwa zaidi kushindwa kwa mtu wake Freeman Mbowe. This shows that he's not politically tolerant...!
TATU: Na haina shaka yoyote kuwa ana chuki na Tundu Lissu isiyo na kichwa wala miguu na simply ni kwa sababu tu aligombea uenyekiti ambao kwenye kichwa chake yeye anaamini kuwa hiyo ilikuwa ni "mali ya Freeman Mbowe" na hivyo Tundu Lissu alifanya kosa la jinai kuutwaa uenyekiti wa Mbowe mali ya mtu binafsi...!
NNE: Analalamikia njia aliyotumia Tundu Lissu kugombea uenyekiti lakini anajikanyaga tu bila kutoa maelezo tatizo ni nini. Kwamba TL alitumia njia za mkato zisizozingatia taratibu na kanuni za chama kuomba kugombea uenyekiti, au nini..?
TANO: Kila mtu inabidi amshangae jamaa huyu, maana njia na hatua alizofuata Tundu Lissu ni njia halali za kikatiba na kikanuni. Alifanya kila jambo hatua kwa hatua na kwa uwazi akieleza kila kitu bila kumvunjia heshima mtu awaye yeyote..
➡Kwanza alianza na hatua ya kwanza ya kutangaza nia....
➡Pili, akaenda akachukua fomu ya maombi ya kuteuliwa kuwa mgombea...
➡ Akapewa, kisha kuijaza....
➡Akairejesha hiyo fomu ndani ya muda wa kikanuni...
➡Akafanyiwa usaili....
➡Akapitishwa na kamati ya uchaguzi na akawa mgombea rasmi....
➡Uchaguzi wa wazi ukafanyika....
➡Akapigiwa kura...
➡Hizo kura zikahesabiwa hadharani...
➡Akamzidi Freeman Mbowe kwa kura nyingi tu...
➡Mwisho akatangazwa mshindi na sasa ndiye mwenyekiti
##Sasa huyu jamaa anaumizwa na nini hasa? Tundu Lissu kakiuka utaratibu gani hasa hata imuumize kiasi hicho?
SITA: Kama ni "character assassination", basi Tundu Lissu kawa assassinated characteristically kwa kiwango kikubwa sana. Na ukiacha tabia hii kufanywa na timu yake Freeman Mbowe ya kampeni, Mwenyekiti mshindwa mwenyewe kwa kinywa chake mara nyingi kila alipopata nafasi ya kuongea kwenye interview mbalimbali za media alimshambulia Tundu Lissu sio kisera bali kwa kushambulia personality na utu wa Tundu Lissu vigorously..
Mathalani Freeman Mbowe alikosa kabisa hoja za kuutetea uenyekiti wake dhidi ya Tundu Lissu kiasi kwamba akaanza kuyatumia mambo binafsi kati yao na Tundu Lissu waliyofanyiana miaka mingi iliyopita kama marafiki na binadamu kama hoja za kushawishi watu na wapiga kura kumwelewa ili aonewe huruma na kupigiwa kura..
Freeman Mbowe alitumia ishu ya kumwazima Tundu Lissu gari lake (which is so personal and completely irrelevant na maswala ya uchaguzi badala yake hili yeye akalifanya kama hoja ya kiuchaguzi...)
Kama tu huyu bwana (mzungumzaji kwrnye vouce note hii) anavyolalamika hapa, can you imagine kuwa Freema Mbowe ktk kuutetea uenyekiti wake alithubutu mpaka kutoa kufuru ya wazi kabisa mbele ya watu na Mungu kuwa asingekuwa yeye, Tundu Lissu mwaka 2017 mara baada ya shambulio la jaribio la kuuwawa Dodoma basi huyu Tundu Lissu wa leo asingekuwa hai..?
Hii nayo eti Freeman Mbowe akaifanya kuwa hoja ya kiuchaguzi. This was terrible na kwa hakika kabisa hili Mbowe alijishushia hadhi yake sana na no wonder kuwa alishindwa uchaguzi ule...!
Yapo mengine mengi ambayo tukiyaorodhesha hapa, tutajaza server za JF zote..
HOJA ZA FREEMAN MBOWE kumwazima TL gari, kusaidia wakati akiumwa, kula naye pamoja na uongo mwingine uliokuwa ukisemwa na Team Mbowe, Tundu Lissu alikuwa akifuatwa na medias kutakiwa atolee maelezo
Shida ilikuwa inakuja, kila Tundu Lissu alipoinua kinywa chake kujibu hoja za Freeman Mbowe ndipo hapo alipoonekana kuwa NI MTU ASIYE NA SHUKRANI sawasawa na anayojieleza huyu ndugu hapa..!
Yaani umsemee uongo mtu, akikanusha uongo huo basi huyo mtu anakuwa hana shukrani? Really...?
Na iliyotia fora zaidi ni hii video👇🏻👇🏻
View: https://youtu.be/prMmQ-gW4Nk?si=-NMpQFAKc3n234eh
Sasa hapa kwa mfano tulitaka Tundu Lissu ajibu kitu gani kama tuhuma zilizotolewa na Freeman Mbowe dhidi yake ni uongo? Auache uongo uenee bila kuukanusha?
Hapana. Hapa hakukuwa na jinsi isipokuwa ifanyike hivi ilivyotokea na kufanyika...
Sanasana kikubwa kilichopaswa kufanyika, ilikuwa nI Freeman Mbowe mwenyewe kujifunza kuchunga mdomo wake kunenea watu wengine uongo maana mwisho wa siku, uongo ungekanushwa tu na kumrudi mwenyewe kama ilivyotokea hapa☝🏻☝🏻
Pole sana ndugu...
Lakini hiyo imeshatoka na kubali tu kuwa Tundu Lissu ndiye Mwenyekiti CHADEMA sasa. Na hiyo kadi ya "Platinum membership" ondoka na uende nayo huko uendako iwe ni CCM na huko huko uliko iwe ni Marekani au shimoni...