Uchaguzi 2020 Wana CHADEMA tuwe tayari kwa lolote; Lissu, Mbowe, Nyalandu, Membe na gia za angani ikilazimika zisiwayumbishe tusimame pamoja

Uchaguzi 2020 Wana CHADEMA tuwe tayari kwa lolote; Lissu, Mbowe, Nyalandu, Membe na gia za angani ikilazimika zisiwayumbishe tusimame pamoja

fazili,

Weka ujumbe wako vizuri ni nini unataka kusema. Lakini kama unataka Membe au Nyalandu, ndio wawe wagombea wa urais wa upinzani, wala usipoteze muda wako. Hao viongozi wa chama tuliwaamini 2015 wakatuletea tapeli, saa hii naona wanaanza kuwa chenga chenga kurudia yale ya 2015. Kama hakuna wagombea wa urais nje ya hizo taka ngumu toka ccm, bora tusimamishe jiwe. Kama mmechukua hela kutetea hao wahuni wa CCM ili wagombee kupitia upinzani, tunawasihi mzirudishe.
Mbowe itakuwa ashakula hela, kaanza kuwatuma vijana wake wachokoze chokoze ili waone reaction ya wanachama
 
Mnajua jinsi awamu ya 5 "ilivyofanikiwa" kwa kutumia propaganda pekee. Leo hii Magufuli angekataliwa kugombea CCM sio ajabu angejiunga CHADEMA na kutimiza ndoto yake. Siasa ndivyo zilivyo, tuwe tayari kwa lolote hata kama ni "kubadilisha gia angani" kama inatusaidia sawa. Magufuli ametumia kila njia kuua upinzani kama mnavyojua, sisi tukijifanya ooh kwanini Nyalandu, kwanini Membe, Mbowe, etc tutaishia kugawanyika na kuwa dhaifu.

Tuwe na lengo MOJA, kushinda uchaguzi kwa njia yoyote ile inayokubalika na inayofanya kazi. Wana CHADEMA jueni kwamba CCM wanafuatilia mienendo yote na wanaogopa sana maamuzi ya CHADEMA. Itakuwa vibaya sana kama tutaruhusu kugawanyika kutokana na maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA. Tusimamie malengo yetu makubwa ambayo ni kuitoa CCM madarakani. Magufuli amekuwa na madhaifu mengi sana kuliko rais mwingine yeyote Tanzania ila CCM wameamua kumbeba kuliko kuanza kuzungumzia madhaifu yake, CHADEMA tunapaswa kuwa hivyo wakati huu muhimu.
Lissu anatosha
 
Nasema hivi, kama Membe kakatwa na watu watano hapo Dodoma, na hamna lolote kafanya, ndio atawaweza ccm wakiwa na mbeleko ya vyombo vya dola? Huyo Membe akawaunganishe wapinzani kama akina APPT MAENDELEO, TADEA, jahazi Asilia, UDP nk ili agombee urais kuwatoa ccm fullstop.
Pengine wewe ni wale wanaofuarilia mambo ya CDM na kuharibu. Siasa sio msaafu. Mkijifanya legalistic hamtafanikiwa. In fact kuna hekima inayosema: CDM hamjui bado kwamba hamtaiondoa CCM kwa siasa za ustaarabu? Kweli tukiendelea na "ustaarabu" huu Magufuli anaweza kutawala kwa miaka mingine 30. CCM wanafurahia woga wa watanzania na wachache wanaonufaika na CCM watatumia mwanya huu mpaka mwisho wa maisha yao.
 
Kumbuka wanachama wengi sana CDM wametoka CCM. Waliozaliwa CDM ni wachache na ndivyo siasa zilivyo. Uingereza wanabadilisha vyama kila miaka 4 au 8 unafikiri kuna wanachama wapya au ni wale wale wa upande mmoja wanaamua kusapoti upande mwingine? Tuwe flexible itatusaidia CDM sio dhehebu ni uwanja wa demokrasia.
wakutoka ccm waje kujiunga wakati ambao c wa uchaguzi,wakati wa uchaguzi wajiunge lakini wawe wanachama wa kawaida, chadema wanaviongozi walioiva wasimamishe mtu wao
 
Mnajua jinsi awamu ya 5 "ilivyofanikiwa" kwa kutumia propaganda pekee. Leo hii Magufuli angekataliwa kugombea CCM sio ajabu angejiunga CHADEMA na kutimiza ndoto yake. Siasa ndivyo zilivyo, tuwe tayari kwa lolote hata kama ni "kubadilisha gia angani" kama inatusaidia sawa. Magufuli ametumia kila njia kuua upinzani kama mnavyojua, sisi tukijifanya ooh kwanini Nyalandu, kwanini Membe, Mbowe, etc tutaishia kugawanyika na kuwa dhaifu.

Tuwe na lengo MOJA, kushinda uchaguzi kwa njia yoyote ile inayokubalika na inayofanya kazi. Wana CHADEMA jueni kwamba CCM wanafuatilia mienendo yote na wanaogopa sana maamuzi ya CHADEMA. Itakuwa vibaya sana kama tutaruhusu kugawanyika kutokana na maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA. Tusimamie malengo yetu makubwa ambayo ni kuitoa CCM madarakani. Magufuli amekuwa na madhaifu mengi sana kuliko rais mwingine yeyote Tanzania ila CCM wameamua kumbeba kuliko kuanza kuzungumzia madhaifu yake, CHADEMA tunapaswa kuwa hivyo wakati huu muhimu.
Mkuu hiyo siyo,Membe amalizane na wale wanaomwambia amefutwa.Membe ni CCM pure hana elements za Chadema.Atumie wajumbe wa NEC na mkutano mkuu kumrejesha kwenye chama na kumpa go ahead ya kupambana na Bulldozer. Ndio maana Membe anaamini bado atanogesha mchuano katika Chama chao.
Vile vile Chadema ina Mbowe jemedari mtimkavu.
Lissu ni biashara iliobuma kwa sasa,kwani CCM watamwekea pingamizi lazima.
Nyarandu nae ametokea CCM awe na subira,ni mapema mno kwa sera ya sasa.
 
Suala la kuwa jiwe hafai kukaa madarakani hilo halina mjadala. Lakini hatuko tayari tena kutumia hizo takataka toka ccm kuitoa ccm. Wazee kama mmekula hela ya hilo jizee mrudishieni. Huyo mzee muacheni abaki na hela zake akazitumie kupambana na kisukari, na sio kujifanya anaweza kuongoza wapinzani kuitoa ccm. Kama hao ccm wameweza kumkata kwenye kikao cha watu watano, na hamna alilofanya, atawezaje kuja kuwatoa sehemu walipo na backup ya tume ya uchaguzi na vyombo vya dola?
kiukweli safari hii sintakuwa tayari
 
Kuna mambo mawili ambayo wanasiasa wa upinzani na waliopo madarakani wanafikiri na yanaweza kuwa hasi au chanya,
Kwanza kumchagua mtu kwa kufuata mapenzi na chama husika bila kujua uwezo na ueledi wa unaemchagua ila tu chama kipite,
Pili kuchagua mgombea haijalishi anattokea chama gani ila tu ana sifa stahiki za kumpa kura kulingana na uwezo na weledi wake katika siasa....!
 
Pengine wewe ni wale wanaofuarilia mambo ya CDM na kuharibu. Siasa sio msaafu. Mkijifanya legalistic hamtafanikiwa. In fact kuna hekima inayosema: CDM hamjui bado kwamba hamtaiondoa CCM kwa siasa za ustaarabu? Kweli tukiendelea na "ustaarabu" huu Magufuli anaweza kutawala kwa miaka mingine 30. CCM wanafurahia woga wa watanzania na wachache wanaonufaika na CCM watatumia mwanya huu mpaka mwisho wa maisha yao.

Kwa taarifa yako sasa wanaccm ndio waliopandikiza siasa za kikondoo ndani ya cdm. Yale maandamano ya ukuta kama sio Lowassa kutoa ushauri wa kikondoo, leo hii tungekuwa tunaheshimiana. Yaani we leo ndio umejua kuwa ccm haiwezi kutoka madarakani kwa siasa za kistaarabu? Huoni kila siku tunasema humu kushiriki uchaguzi ili kupata wagombea ni kupoteza muda, bali tudai tume huru ya uchaguzi, na kama hakuna tume huru ni uchaguzi. Sio lazima viongozi wote wapatikane kwa njia ya kura.
 
Chadema kama chama kikuu cha upinzani kimeshakomaa, huu ni wakati wao kuwa na mgombea wao, wapime uungwaji mkono watakaoupata toka kwa wananchi, waijue nguvu yao.

Hili suala la kuchukua watu toka CCM waje kupewa nafasi ya kugombea Chadema linatakiwa kufa, likiendekezwa litajenga tabia, halafu litashusha hadhi ya chama.
Uko sahihi Mkuu maana hawakawii kupata gizani then baada ya uchaguzi wanarbudi kuunga juhudi na maning' uniko kibao
 
Kwa taarifa yako sasa wanaccm ndio waliopandikiza siasa za kikondoo ndani ya cdm. Yale maandamano ya ukuta kama sio Lowassa kutoa ushauri wa kikondoo, leo hii tungekuwa tunaheshimiana. Yaani we leo ndio umejua kuwa ccm haiwezi kutoka madarakani kwa siasa za kistaarabu? Huoni kila siku tunasema humu kushiriki uchaguzi ili kupata wagombea ni kupoteza muda, bali tudai tume huru ya uchaguzi, na kama hakuna tume huru ni uchaguzi. Sio lazima viongozi wote wapatikane kwa njia ya kura.
Siamini kwamba ccm ndio wamepandikiza siasa za kikondoo CDM eti kwa njia ya Lowassa. Lowassa alishaondoka siku nyingi, tatizo ni sisi wana CDM kufikiri siasa siku zote lazima ufuate ustaarabu, hayo labda baadhi ya nchi za Ulaya, lakini hata wao kabla ya kufika hapo vumbi ilitimka. CDM tunaogopa hata kubadilisha gia angani je tutaweza kuingila mtaani kudai tume huru?
 
Siamini kwamba ccm ndio wamepandikiza siasa za kikondoo CDM eti kwa njia ya Lowassa. Lowassa alishaondoka siku nyingi, tatizo ni sisi wana CDM kufikiri siasa siku zote lazima ufuate ustaarabu, hayo labda baadhi ya nchi za Ulaya, lakini hata wao kabla ya kufika hapo vumbi ilitimka. CDM tunaogopa hata kubadilisha gia angani je tutaweza kuingila mtaani kudai tume huru?

Kabla ya Lowassa na mafuriko yake uliwahi kusikia siasa zinazoitwa za kistaarabu zikisifiwa ndani ya cdm? Lowassa na mitume wake walipokuja cdm m, ndio tulisikia wakisema cdm kisiwe chama cha kiharakati bali kiwe chama cha siasa. Sasa hivi watu wameingia woga, inahitajika viongozi majasiri wa kuinua tena moral ya kutokuwa waoga. Na hili haliwezi kuletwa na mwanaccm yoyote yule. Lisu pekee ndio anaweza hilo.
 
Mnajua jinsi awamu ya 5 "ilivyofanikiwa" kwa kutumia propaganda pekee. Leo hii Magufuli angekataliwa kugombea CCM sio ajabu angejiunga CHADEMA na kutimiza ndoto yake. Siasa ndivyo zilivyo, tuwe tayari kwa lolote hata kama ni "kubadilisha gia angani" kama inatusaidia sawa. Magufuli ametumia kila njia kuua upinzani kama mnavyojua, sisi tukijifanya ooh kwanini Nyalandu, kwanini Membe, Mbowe, etc tutaishia kugawanyika na kuwa dhaifu.

Tuwe na lengo MOJA, kushinda uchaguzi kwa njia yoyote ile inayokubalika na inayofanya kazi. Wana CHADEMA jueni kwamba CCM wanafuatilia mienendo yote na wanaogopa sana maamuzi ya CHADEMA. Itakuwa vibaya sana kama tutaruhusu kugawanyika kutokana na maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA. Tusimamie malengo yetu makubwa ambayo ni kuitoa CCM madarakani. Magufuli amekuwa na madhaifu mengi sana kuliko rais mwingine yeyote Tanzania ila CCM wameamua kumbeba kuliko kuanza kuzungumzia madhaifu yake, CHADEMA tunapaswa kuwa hivyo wakati huu muhimu.
Bila kudai na kupigania tume huru ya uchaguzi, mbinu zote mtakazochukua ni sawa na bure. "Count yourselves as losers".
 
Siamini kwamba ccm ndio wamepandikiza siasa za kikondoo CDM eti kwa njia ya Lowassa. Lowassa alishaondoka siku nyingi, tatizo ni sisi wana CDM kufikiri siasa siku zote lazima ufuate ustaarabu, hayo labda baadhi ya nchi za Ulaya, lakini hata wao kabla ya kufika hapo vumbi ilitimka. CDM tunaogopa hata kubadilisha gia angani je tutaweza kuingila mtaani kudai tume huru?
Good.
 
Bila kudai na kupigania tume huru ya uchaguzi, mbinu zote mtakazochukua ni sawa na bure. "Count yourselves as losers".
Hakuna atakayetupatia tume huru ya uchaguzi. Naamini tume hiyo haitapatikana kwa ustaarabu bali kwa mapigano, hata CDM wakiingia madarakani hawataweka tume huru.
 
Mnajua jinsi awamu ya 5 "ilivyofanikiwa" kwa kutumia propaganda pekee. Leo hii Magufuli angekataliwa kugombea CCM sio ajabu angejiunga CHADEMA na kutimiza ndoto yake. Siasa ndivyo zilivyo, tuwe tayari kwa lolote hata kama ni "kubadilisha gia angani" kama inatusaidia sawa. Magufuli ametumia kila njia kuua upinzani kama mnavyojua, sisi tukijifanya ooh kwanini Nyalandu, kwanini Membe, Mbowe, etc tutaishia kugawanyika na kuwa dhaifu.

Tuwe na lengo MOJA, kushinda uchaguzi kwa njia yoyote ile inayokubalika na inayofanya kazi. Wana CHADEMA jueni kwamba CCM wanafuatilia mienendo yote na wanaogopa sana maamuzi ya CHADEMA. Itakuwa vibaya sana kama tutaruhusu kugawanyika kutokana na maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA. Tusimamie malengo yetu makubwa ambayo ni kuitoa CCM madarakani. Magufuli amekuwa na madhaifu mengi sana kuliko rais mwingine yeyote Tanzania ila CCM wameamua kumbeba kuliko kuanza kuzungumzia madhaifu yake, CHADEMA tunapaswa kuwa hivyo wakati huu muhimu.

Kila unachosema hapa ni completely opposite from the reality. CCM 2015 ilikuwa imekufa ila Magufuli kafufua chama, na kasi aliyokuwa nayo chama sasa ni imara ila wabaya wake wengi wapo ndani ya chama kwani ule ulaji, madili hamna tena! Ubinafsi
ulizika vyama vya upinzani November 2015 na hatutegemei uhai kurudi tena upinza. Upinzani sasa hauna ‘base’! Yaliyokuwa yanafanywa na Edward Moringe Sokoine na Mwl Nyerere sasa yanatekelezwa.
 
Back
Top Bottom