Uchaguzi 2020 Wana JF, nipeni Pole. Msinicheke wala msinibeze; nimegombea ubunge Kawe kupitia CCM nimeambulia kura 1. Ama kweli CCM ina wenyewe!

Najua mleta mada alisema tusicheke.

Ni vigumu sana kujizuia kucheka.

Na kutoweza kujizuia kucheka sio kwa sababu hakuchaguliwa; sijui kama nitaeleweka hapa!

Asikate tamaa, teuzi muda wake bado. Jasho ni lazima litafutwa tu safari hii.

Kama wengi hawaelewi maana ya hilo alilofanya, i.e., ni njia ya kuingilia kwenye uteuzi unaofuata baada ya Oktoba.
 
Subiri teuzi. Tunajua hiyo ilikuwa gia ya kuingilia ili uonekane kwa wateuzi. Hongera sana kwa first stage
 
Kwanza nakupa pongezi sana na wala sikupi pole ni hongera nyingi sana,na pia usihofu nata mwandishi mwenzio deo nsokolo kapata kura moja tu kule nsimbo alipoenda kugombea
 
Naunga hoja..mnafiki hatari huyu jamaa...njaa mbaya sana aisee
 
Pole sana . Ila umethubutu.

Mara nyingine CCM SIO MAHALI SALAMA KWA MTU ANAETAKA KUISIMAMIA NCHI KWA KUTOA MICHANGO TUKUKA. Sasa wewe ulivyo na msimamo kuwa ccm usingepata hata kura moja. Huyo aliyekupigia nae sijui kama alilewa ama!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…