Wanachama wa JamiiForums waliotangulia mbele ya haki (Fariki) R.I.P

Wanachama wa JamiiForums waliotangulia mbele ya haki (Fariki) R.I.P

ni neno hilo mtoa mada...sema na hivi hatujuani zaidi ya haya majina ya humu, waweza shangaa unakwenda kwenye msiba wa ndg au rafiki yako au mtu yeyote tu unayemjua kumbe ndo mwana jamii forums mwenzako!...bila kujua hio...dah tumuachie Mwenyezi Mungu tu mtu ikitoea imejuliana amefariki basi tujaribu kushiriki na km haitajulikana basi tuomeane kheir tu ila wakati...
Ni kweli humu unaweza jibishana na baba mkwe au baba mwenye nyumba bila kujua
 
Nimesukumwa kuanzisha uzi huu ili tuweze kuwajua wenzetu waliotangulia/wanaotangulia mbele za haki kwa wale mnaofahamiana. Marehemu walikuwa kama sisi tu humu,wakielimisha,kuburudisha n.k lakini kwa sasa wamerudi mavumbini. Bahati mbaya wengine hatufahamiani kabisa physically,binafsi sina ninayemjua humu hivyo hata nikifa sio rahisi kupata habari zangu hivyo likitokea tutakutana Mbinguni kwa Baba.
Hivyo kwa wale mmnaojuana,ni vema mkawa mnatupa taarifa ili tuweze kuwaombea wenzetu katika sala zetu za kila siku. Mpaka sasa,kwa kumbukumbu zangu inaonyesha wanaJF wafuatao wameishafariki kadiri ya habari zinavyoripotiwa humu😔
1.Fasi Dwasi
2.Dena Amsi
3.Straton Mushi
4.Kennedy Lufulondama

Najua kuna wengine zaidi,tujuze humu...Mungu awalaze mahali pema peponi...Amina
 

Folk alifariki kimasikhara maskhara tu. Alinihuzunisha kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Folk alifariki kimasikhara maskhara tu. Alinihuzunisha kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
aseee.. very sad,ilizibithishwa alikufa?anaitwa folk
 
Back
Top Bottom