Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Asante kwa somo mkuu
 
Mi sipendagi UNAFIKI, tupunguze ubinafsi na kunyoosheana vidole. Kwani, suala la mzee kupishwa kiti ni la kikatiba au kiubinadamu?

Namna nzuri ya kumkosoa na kumfundisha aliye mdogo kwako ni kwa mifano. Ninayo imani wengi wa wachangiaji hawajui kuwa nao wana wajibu wa kumpisha huyo mzee, wanalisukumia kwa mwanafunzi. Huyo mwanafunzi hana adabu, kama walivyo wengine wote waliokuwamo kwenye basi na ndio maana ukazuka mjadala as if wengine wasingeweza kumpisha.

Jamii hii ifundishane upendo na sio kuwalazimisha wengine kukidhi matarajio yao. Mleta mada anaamini mambo yangekuwa sawa kama mwanafunzi angejibu politely 'nalipa nauli ya mtu mzima' ... seriously? Kwa hiyo akilipa nauli ya mtu mzima, huyo mzee wenu anapata nafuu ya kusimama kwake? Kwa mentality hii, atapatikana kweli mkubwa wa kumsaidia mdogo endapo itatatokea mdogo kachoka sana?

Huyo mwanafunzi ni zao la hizi firka zetu mbovu.
 
Mungu anisamehe ila yule anaonekana anaenda shule kusindikiza wenzie tu. Form four yake naona zero kabisa
Na amsamehe kwa kweli maana huenda ikawa hajui atendalo kutokana na malezi aliyopitia kuanzia chini hivyo anajionea sawa tu.
 
ila huyo mwanafunzi mdomo wake mchafu unaohusu "stress za kutokulipwa mshahara" umenifunza kitu!!....Kumbe hata watoto wadogo siku hizi wanaelewa kuwa kuajiriwa ni utumwa,haya ndiyo maendeleo tunayoyataka katika nchi!!....Asante mtoto kwa mdomo wako mchafu ulionifunza kitu!!
 
Kwa majibu hayo ndio maana zero zinawaandama kila kukicha....

Kwanza sijawahi ona wanafunzi wahuni kama wa mji huo....
 
Sababu moja situkanani na mtu nisiemjua humu ni hiyo.
 
Kati ya watu nawatetea kwenye daladala ni wanafunzi. Tena nikisikia konda anamwambia mpishe mkubwa nitalipa nauli ya huyo mwanafunzi ili akae tu kwenye siti. Hata mimi nikiona mtu mzima sana au mtu mwenye tatizo nampisha siti anakaa bila kuambiwa.
Narudi sipendi hilo jambo la kumwambia mwanafunzi ampishe mkubwa kiti ila huyu mwanafunzi hana nidhamu. Ni haki yake kukalia siti ila alichomjibu yule mama kilivuka. Angemwambia tu nalipa nauli ya mtu mzima angepungukiwa nini? Na hata muonekano wake yule mtoto anaonekana kashindikana.
 

Kama huyo mama mtu mzima alikuwa anamuonea huruma huyo mzee basi angempisha yeye.

Ya nini kubishana na watu tena watoto kwenye usafiri? Ni kukosa busara tu.
Sawa
 
Maskini sijui huyo mama alijisikiaje. Sio kwa Dar pekee, watoto wengi wamekua na maadili mabaya.

Halafu nidhamu inaanzia nyumbani, kila mzazi ni lazima amjenge mwanae kitabia na kiimani ili ajue kuishi na jamii inayomzunguka.
Lazima alijisikia vibaya kujibishwa na mtu kama binti yake halafu anamwambia mwanao angekua kalingana na mimi angekua kwenye hili gari. Yule mtoto ana dharau sana
 
Hata kama analipa nauli ndogo bado ana haki ya kukaa. Mtizamo upo kwamba mwanafunzi ni mdogo anatakiwa kumpisha mkubwa kiti. Hii sio kwenye daladala tu hata majumbani mwetu iko. Huwezi kukaa kwenye kiti wakati aliekuzidi umri amesimama. Ila kama mtoto ana kitu kinachomfanya ashindwe kusimama anajibu tu kwa adabu sio majibu ya kujiona mbabe
 
Wanaomtetea huyo mtoto sijui wanawaza nini. Wanadhani hapa kinachoongelewa kumpisha siti mtu mzima.
 
Ingekua kijijini angekula fimbo. Sema yule anaonekana hata kwao anawasumbua. Unapata wapi ujasiri wa kumsema vibaya mama mtu mzima tena bila woga kwenye daladala ilojaa jamani.
Mngemshusha tu maana kumpiga ingewapa kesi nadhani unaona majibu ya baadhi ya wadau (inasikitisha)

Kujibishana naye nayo ni km mwehu kukuibia nguo na wewe ukaanza kumkimbiza

Kuna siku nilikiwa huko kwenu sasa kitoto kama cha darasa la nne kikawa kimepanda daladala kuanzia asbh mpk saa sita kimo kwenye gari hakishuki abiria wakakishtukia wakaanza kumuhoji huyo mtoto akawa anajichanganya tu kwenye maelezo mweeee niliiona nguvu ya jamii mbona walimtafuta mpaka mzazi wake wa kiume (aliwapa no ya baba yake) baba ndo kueleza shida za mwanae na hapo alikuwa kadanganywa pale pale nakumbuka ilikuwa maeneo ya tazara walimshusha wakampeleka kituo cha polisi

Hiyo ndo jamii tunayoitaka huyo ilitakiwa mumfunze lkn kumuachia hivyo tu atafanya huo ushenzi mahali pengine
 
Kama yule alikua anamuona yule mama atamwambia nini sasa. Kuna muda naogopa sana malezi ya watoto wetu zama hizi. Nikiona watoto wengine nawaza wangu itakuaje akifika hapa. Wakati mwinginr hata wazazi wanakua wameshachoka ila ndo mtoto keshakengeuka huna namna
 
Hakuomba ampishe yeye. Yule mama alikaa dirishani na yule mwanafunzi alikaa siti inayofuata. Ingekua pia kama laana fulani mtu mzima aliekaa dirishani ampishe mtu wakati kuna mwanafunzi kwake yeye kumpisha ilikua rahisi zaidi.
 
Umerukia hata kichwa cha habari sikuandika mwanafunzi ampishe mtu mzima kiti ila majibu ya dharau. Hata asingempisha kiti kwangu mimi ingekua poa tu kwa sababu hakuna sehemu mwanafunzi anatakiwa ampishe mtu mzima kiti. Nilichoongelea ni majibu aliyotoa yule mwanafunzi kabla hajatoka kwenye kiti.
 
Hahahahahaaa. Eti anamuuliza mwenzie kwani leo lini?? Aah kumbe mwisho wa mwezi ndo maana mama anataka kik kwangu kumbe ana stress za mshahara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…