Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Wanafunzi Dar na Dharau kwa Wakubwa Wao

Hata kama analipa nauli ndogo bado ana haki ya kukaa. Mtizamo upo kwamba mwanafunzi ni mdogo anatakiwa kumpisha mkubwa kiti. Hii sio kwenye daladala tu hata majumbani mwetu iko. Huwezi kukaa kwenye kiti wakati aliekuzidi umri amesimama. Ila kama mtoto ana kitu kinachomfanya ashindwe kusimama anajibu tu kwa adabu sio majibu ya kujiona mbabe

Tukopamoja katika hili. Nami nilimaanisha mtazamo kuwa anasimama kwa sababu analipa nauli kidogo ni potofu. Otherwise tupo pamoja.
 
Kama yule alikua anamuona yule mama atamwambia nini sasa. Kuna muda naogopa sana malezi ya watoto wetu zama hizi. Nikiona watoto wengine nawaza wangu itakuaje akifika hapa. Wakati mwinginr hata wazazi wanakua wameshachoka ila ndo mtoto keshakengeuka huna namna
Sasa hapo unaweza kukuta mama mtoto huyu kavurugwa kama alivyoimba Snura.

Utategemea nini kwa mtoto?

 
Hahahahahaaa. Eti anamuuliza mwenzie kwani leo lini?? Aah kumbe mwisho wa mwezi ndo maana mama anataka kik kwangu kumbe ana stress za mshahara
ila dunia ya sasa hivi kuwa mzazi inahitaji moyo,just imagine wewe ndiyo mzazi wa huyo mtoto-you just exhausted your money,time,mind,e.t.c to raise such a lil Monster!!
 
Mngemshusha tu maana kumpiga ingewapa kesi nadhani unaona majibu ya baadhi ya wadau (inasikitisha)

Kujibishana naye nayo ni km mwehu kukuibia nguo na wewe ukaanza kumkimbiza

Kuna siku nilikiwa huko kwenu sasa kitoto kama cha darasa la nne kikawa kimepanda daladala kuanzia asbh mpk saa sita kimo kwenye gari hakishuki abiria wakakishtukia wakaanza kumuhoji huyo mtoto akawa anajichanganya tu kwenye maelezo mweeee niliiona nguvu ya jamii mbona walimtafuta mpaka mzazi wake wa kiume (aliwapa no ya baba yake) baba ndo kueleza shida za mwanae na hapo alikuwa kadanganywa pale pale nakumbuka ilikuwa maeneo ya tazara walimshusha wakampeleka kituo cha polisi

Hiyo ndo jamii tunayoitaka huyo ilitakiwa mumfunze lkn kumuachia hivyo tu atafanya huo ushenzi mahali pengine
Mimi ningekaa karibu na yule mwanafunzi ningemwambia alichofanya sio kizuri japo aliemwambia asimame pia alikosea. Lakini nikasema yanini kupigizana kelele. Na watu walimind wengi sema yule mwanafunzi alivyoonekana sio mtu mwenye adabu wakaa kimya. Waliona ukiongea atakujibu sasa kuliko kuaibishana na mtoto mdogo bora ukae kimya tu. Nikawaza angetokea mtu pale ana muda wake anamshika mkono mpaka shule akamshtakie vitendo vyake vya ukosefu heshima alivyoonyesha
 
Mtu mzima ukishapanda kwny usafiri wa umma inabidi nawewe uache kuwaambia watu wakupishe siti ukiona mwanafunzi hataki kusimama achana nae,hawa watoto nao wanachoka jamani
Kweli kabisa kuna watu wanataka waheshimiwe kila mahali utafikiri anaongoza dunia yeye
 
Hata mimi kuna wakati hua siwachii siti wazee kwa sababu ya ukorofi wao. Unakuta stend magari yapo kibao mengine hayajajaza unakuta bado mzee anaforce kuja kupanda daladala lililojaa mie watu kama hao hua siwaachii siti akili zao zipate akili siku nyingine wawe wanajiongeza
 
Nilihisi hivyo tuu, atakuwa wa kike, ndiyo walivyo wanafunzi wa kike wengi wao adabu hawana wanajiona washakua...

Wakiume ni watukutu ila adabu wanazo kwa wakubwa zao...


Cc: mahondaw
Wa kiume wanaangaliaga pa kufanyia ujeuri. Wa kike kama hajielewi akishaanza michezo ya wakubwa tu anajiona na yule mkubwa
 
Sasa hapo unaweza kukuta mama mtoto huyu kavurugwa kama alivyoimba Snura.

Utategemea nini kwa mtoto?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
ila dunia ya sasa hivi kuwa mzazi inahitaji moyo,just imagine wewe ndiyo mzazi wa huyo mtoto-you just exhausted your money,time,mind,e.t.c to raise such a lil Monster!!
Unaweza ukapiga ukaua. Basi tu yani.
 
Sana yani halafu haoni aibu anaongea kwa sauti watu wote tunamsikia. Badala angejibu chini chini ila anavyojiamini hakujali tutamchukuliaje ye anampa maneno tu mama wa watu
Mgejibu tu na nyie mngejibiwa mpaka mngelia
 
Back
Top Bottom