Wanafunzi wa kizazi hiki wanafaulu sana. Je, ni bora kuliko nyie?

Acha janja janja wewe, kubali tu kizazi chenu kilikua cha vilaza kuliko generation Z ya sasa.

Kizazi chenu cha vilaza, madomo zege na washamba.

Sent using Jamii Forums mobile app
Zamani sekondari jitu linasoma zee limeacha mke hadi nyumbani masomo yatapandaje? Umri ulichangia kizazi cha zamami kutofaulu sana
 
Ili niamini madogo wapo vizuri niwape ile paper ya Advance Maths, Chemistry na Physics ya 2013...alafu nione izo One zao wakitoboa nitajua madogo wapo vema
Hizo past paper madogo wamesha solve sana

Kuna hadi vitabu vya past examinations papers na solution zake za hiyo miaka it is not a big deal wape tu

Wakimaliza zamu yako na wao wakupa ya kwao utakaa chini biology uliyosoma wewe sekondary sasa hiivi inafundishwa primary school darasa la nne
 
Mchukue MLETENI tupige naye stori mbili tatu za masomo hayohayo mfano Mimi ni EGM ... Mtafute wa kombi nyingine mkalishe nao pia uone ... Hawana uelewa wowote wachache sana ..wengi wao ni kumeza na kutema ...
 
Urahisi wa kupata materials, urahisi wa kuhama shule, urahisi wa maisha pia.

Zamani ukipangiwa pugu basi ni pugu tu, huwezi kuhama, utakomaa hapo hapoa hata kama magonjwa nyemelezi yanakushambulia, hata kama hamna walimu na changamoto kama hizo.

Ila miaka hii, ukiona shule haikufai kuna uwezekano wa kuhama kwenda private schools au government school unayoona inakufaa.

Sababu ni nyingi mkuu, na huenda maswali hayatofautiani saana ila ule urahisi wa kupata majibi ya hayo maswali umerahisishwa zaiidi.

Je zamani mlikua na past papers?? Lakini sasa kuna past papers za hadi miaka ya 90 huko ni mwanafunzi mwenyewe achague maswali ya kukomaa nayo, na uzuri au ubaya ni kua maswali yanajirudia.
 
1. Mitihani inatungwa simple sana, kama unabisha chukua mitahani ya form six 2000 hadi 2010 kisha linganisha na ile ya 2014 hadi 2024.

2. Siasa, baada ya sakata la mwaka 2013 juu ya ufaulu wa kidato cha nne, kila kitu kilibadilishwa.

3. Uwepo wa walimu na vitendea kazi. Binafsi nimehitimu kidato cha 6 sijui hata mtaala wa elimu ukoje na sikuwahi ona kitabu chochote cha T.I.E cha advance. Tulikuwa tunasoma vitabu vya wahindi na waswahili kidogo kama kile cha Shayo kwenye advanced mathematics.
 
Usomaji umekuwa rahisi sana siku hizi, vitabu vingi, vitini, walimu wanafundisha sana.
Nakumbuka enzi hizo nasoma A Level mwalimu wa physics alikuwa anaingia darasani mara moja kwa mwezi.
 
Ukitaka kujua wazee wa zamani walisoma ujinga angalia nchi hii walivyoipeleka

Walileta azimio la Arusha wakataifisha mali za watu waliojipatia mitaji na biashara kwa nguvu zao .Halafu wakaja na ujinga mwingine siasa ya ujamaa na kujitegemea uliotia umaskini wananchi na taifa wakaja kuua na elimu wakaanzishe shule za UPE ambazo mwalimu alikuwa aliyemaliza darasa la saba

Kizazi cha sasa kikagomea yote na kufuta ujinga wao walioanzisha kwenye hii nchi

Mzee akisema ohh sisi eliim8 yetu ilikuwa kubwa muulize cha maana mlichoifanyia nchi nini? Mashirika ya umma hivyo vizee viliua yote.Zero competence kwenye uendeshaji mashirika

Kuna haja kuwa na siku maalumu ya generation Z ya kuvizomea hivyo vizee vya zamani.Iwe ni siku ya kitaifa na ya mapumziko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…