Wanafunzi wa kizazi hiki wanafaulu sana. Je, ni bora kuliko nyie?

Wanafunzi wa kizazi hiki wanafaulu sana. Je, ni bora kuliko nyie?

Ukichunguza matokeo ya wanafunzi wa form six 1960-2014 walikua ni miamba kweli kweli, yaani mtu anatambulika karibu kijiji kizima kwamba kijana wa flani kafaulu, mimi binafsi nilikua nikikutana na mtu ameenda form five nilikua namuona watofauti saana, heshima nyingi mtaani, na matokeo yao miaka hiyo yalikua ni mabaya sana.

Refers matokeo ya ACSEE 2012. Hapa hata PCB mwenye three ya 15 alisoma udaktari...

View attachment 3042266View attachment 3042267View attachment 3042268View attachment 3042270View attachment 3042270
View attachment 3042271

Baada ya hapo kikaingia kizazi cha 2000, ambapo tunawaona kama wazinguaji, wasiokua na maadili lakini wananyoosha balaa, fikiria zamani shule zilikua zinajulikana, minaki, Milambo, pugu, n.k...

Lakini sasa hivi madogo wanaenda shule za hovyo, shule inaitwa kasangezi, sijui Ziba ya huko igunga lakini wanapasua balaa.
Miaka hii kusoma udaktari bila division 1 point 6 hupati udaktari...

View attachment 3042275View attachment 3042276

Swali je madogo wa siku hizi wanauelewa kuliko wa miaka ya zamani? Mtaala hujabadilika sana waliosoma biology 2005 bs, ndio wanachokisoma watoto wa sikuhizi.

Pia soma:Matokeo Kidato cha Sita 2024 yatoka. Ufaulu wapanda kwa asilimia 0.26
Now Days mwanafunzi wa Form Three na yy anatumia Mathematics Calculator. Je Elimu inakwenda wap....? Wanafunzi wa siku hizi weng hawajua Mathematics Table
 
Kiukweli tuache kubeza kupanda kwa ufaulu wa madogo. Sisi tuliohitimu form six zamani mazingira yetu ya kufaulu vizuri yalikuwa magumu kutokana na sababu zifuatazo;
1.Ukosefu au upungufu mkubwa wa walimu mashuleni
2.Ukosefu/upungufu mkubwa wa vitabu sahihi vya kuendana na syllabus
3. Miundombinu mibovu na isiyojitosheleza ilipunguza morali ya kusoma kwa bidii, mfano
4. Maabara za masomo ya sayansi hazikuwa vizuri kwa majengo na vifaa kama sasa
5. Ukosefu wa njia mbadala za kupata materials ya kujisomea kama vile google search au youtube.
6. Ukosefu wa tuition bora hasa kwa masomo ya science.
Mimi ni mhitimu wa mwaka 2000 HGE, tuwape maua yao vijana kwa ufaulu mzuri.
 
Ukichunguza matokeo ya wanafunzi wa form six 1960-2014 walikua ni miamba kweli kweli, yaani mtu anatambulika karibu kijiji kizima kwamba kijana wa flani kafaulu, mimi binafsi nilikua nikikutana na mtu ameenda form five nilikua namuona watofauti saana, heshima nyingi mtaani, na matokeo yao miaka hiyo yalikua ni mabaya sana.

Refers matokeo ya ACSEE 2012. Hapa hata PCB mwenye three ya 15 alisoma udaktari...

View attachment 3042266View attachment 3042267View attachment 3042268View attachment 3042270View attachment 3042270
View attachment 3042271

Baada ya hapo kikaingia kizazi cha 2000, ambapo tunawaona kama wazinguaji, wasiokua na maadili lakini wananyoosha balaa, fikiria zamani shule zilikua zinajulikana, minaki, Milambo, pugu, n.k...

Lakini sasa hivi madogo wanaenda shule za hovyo, shule inaitwa kasangezi, sijui Ziba ya huko igunga lakini wanapasua balaa.
Miaka hii kusoma udaktari bila division 1 point 6 hupati udaktari...

View attachment 3042275View attachment 3042276

Swali je madogo wa siku hizi wanauelewa kuliko wa miaka ya zamani? Mtaala hujabadilika sana waliosoma biology 2005 bs, ndio wanachokisoma watoto wa sikuhizi.

Pia soma:Matokeo Kidato cha Sita 2024 yatoka. Ufaulu wapanda kwa asilimia 0.26
umezingatia alama za ufauli zamani na sasa ile iliyokua ikiitwa divisheni wanibilikua wani kweli.... aliepata 4 miaka ya 90 mpaka 2005 huyo sasa hivi angekua na tuu au wani nzuri tu hutaki saga chupa unywe
 
Walimu wana haki zaidi ya kutoa comments kwenye Uzi huu maana ndio wanaishi na wanafunzi.

Kwa kweli wanafunzi wanafaulu sana sio kwa sababu wana akili sana bali kwa sababu

1. Mitihani inavuja sana (nililokuwa form 5 nilishuhudia mabrothers form six wakisolve possibles na Kisha wakitoka kwenye mtihani wanafurahi kuwa possible ni Ile ile, kadhalika nilipokuwa nafanya NECTA ACSEE nimeshuhudia paper tulizokuwa tunasolve tunazikuta Kama zilivo kwenye mtihani.


2. Mfumo wa NECTA kwa sasa umeamua kuwabeba wanafunzi ili waonekane wanafaulu, Kuna program kama BRN, matumizi ya calculator O level, kuchagua math primary nk
_ wanafunzi huwa wanapata marks ndogo sana kwenye mitihani ya ndani, ila NECTA unashangaa hadi aliyekuwa anapata zero kapata two.


Ishu kubwa mfumo umeamua kuwabeba wanafunzi.

3. Mwanafunzi aliyemaliza miaka ya zamani, anaweza kupata three au two wakati huo huo kabla hajaenda advance akawa anafundisha tuition na anashusha nondo

ila kwa sasa mwanafunzi anapata threw form four au six ila hata ukimuambia afundishe hawezi.

Kimsingi imeongezeka quantity ila quality imepungua sana.


Haiwezekani shule za mkoa wa MTWARA karibu zote ukute hazina zero wala four

Haiwezekani shule inayochukua wanafunzi wa kawaida ije kupata one nyingi kuliko jumla ya two na three.
Hii shule inachukua wanafunzi kutoka kila mkoa ndani ya Tanzania. Si busara kuamini kwamba hao wanafunzi wote ni Wamakonde ama wamakua kisa ipo Mtwara.
 
Sidhani kama kufeli kwa form six wa zamani na kufaulu wachache sana ni sifa njema. Kuna factors nyingi zilizopelekea wengi kufeli kipindi hicho. Mimi nitataja chache hapa:

1. Ukosefu wa materials za kutosha (Chand zenyewe ulikuwa unakuta ipo Moja darasa zima, waalimu wa tuition wachache, gharama za material kubwa, and things alike).
2. Nidhamu mbovu, wanafunzi wa zamani walikuwa wakorofi sana, wanapiga waalimu, migomo kama yote, mademu wao, kudoji kama kote kwa sababu walimu waliwaogopa wanafunzi kuepuka kipigo, n.k.
3. Kusoma wakiwa umri umeenda sana. Ukisoma umri umeenda sana mambo yanakuwa mengi mbali na kuwa unajielewa hii inapunguza concentration ya shule. Wee form six wa kipindi hicho unakuta anasoma kidevu kigumu kweli, ndevu mpaka shingoni😆. Wengine walidiriki kusoma wakiwa na familia zao nyumbani. Ukilinganisha na watoto hawa wa 2000+, form six unakuta ana miaka 18 19, kwa nini asiwaze masomo tu.
4. Shule za serikali usimamizi ulikuwa duni kipindi hicho, performance imeanza kuongezeka kwa Kasi aliposhika wizara Ndarichako chini ya Rais JPM. Strategies za wizara ya Elimu hazikuleta matokeo sahihi sana kipindi hicho. Tukisema mitihani ya Sasa ni rahisi kuliko ya zamani, sio kweli, kwa sababu mitihani mingi ya sasa Afisa mitihani anachukua maswali ya mitihani ya zamani. Tena katika syllabus ya 2020 inaeleza kwamba mitihani itungwe kwa kupima uelewa zaidi ya kukariri, ila hapo sidhani kama implementation yake inafanyika inavyostahili.

"Kwa changamoto hizo zote, mwanafunzi aliyetoboa kipindi hicho alikuwa bora kweli kweli kuliko mwanafunzi anayetoboa kipindi hiki"

Sababu zinazopelekea ufaulu wa sasa kuwa mkubwa kuliko zamani, nionavyo mimi ni:

1. Kuongezeka kwa materials za kujifunzia. Toka 2019 Wizara ilipondaa vitabu vizuri vya kiada (text books) chini ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), vimerahisha sana elimu ya Advance ukilinganisha na zamani. Hakuna tena kuhangaika na mi Chandi, BS, Tom Dancun, University physics, Ally Abdallah, Mgote, Elias Kiyombo, you mention them. Baada ya vitabu vya TIE vilivyotengenezwa mwaka 2014 kufeli, awamu hii wamefaulu ktk hilo. Mbali na vitabu kuwa vingi, walimu ni wengi sana siku hizi, tuition center kila Kona, technolojia ndio usiseme. Kwa nini vijana wasifaulu bana.

2. Nidhamu imeongezeka sana, wanaosoma siku hizi ni watoto sana, ukiwatisha kidgo tu wanatii. Mwanafunzi mtiifu shuleni ana high chance ya kufaulu kuliko mtovu wa nidhamu.

3. Shule za A' level zimeongezeka sana hivo ushindani umekuwa mkubwa. Private schools kama zote na zote zinataka wanafunzi hivyo lazima waakikishe outputs zao zinakuwa nzuri na nyingi ili kuvutia umma japo zipo baadhi zinazotumia mbinu danganyifu lakini nyingi wanakuwa really. Kwa hivyo, hii lazima iongeze % ya ufaulu compared to old school.

Maoni yangu ni hayo machache, ziko nyingine nyingi sababu, sema tu ni vile watu hawataki kuzitaja.

Anyways, By for Now!
Umemaliza kila kitu
 
Mpime mtoto wako aliyefaulu vizuri kwenye vitu vya kawaida tu hapo ndio utaelewa. Shida inaweza kuwepo, mm toka napoona(ga) humu graduates wa sasa hata kuandika kiswahili vizuri hawezi huwa napata hasira sana

Au angalia EATV kipindi cha skonga. Dogo wa form three anaulizwa "kochi, viti, meza" kwa jina la pamoja kwa kiingereza vinaitwaje
Dogo anakuna kichwa, anaangalia juu anaumiza akili, alafu mwishoni anasema kwa kiingereza ni "vegetables"
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ila Cantrii wee, Em sema kweliii?
 
Ili niamini madogo wapo vizuri niwape ile paper ya Advance Maths, Chemistry na Physics ya 2013...alafu nione izo One zao wakitoboa nitajua madogo wapo vema
Akati niko Advance, wakati wa mitihani ya Pre national,
Ticha wa Maths alileta paper LA Math, 2013 Necta km lilivyo.

Tokeo lilivyotokaa, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ni full kukimbianaa, Woiiiih. Lile paper ni Konyoooo, Khaaah
 
Kuna jamaa alisema
Ukichunguza matokeo ya wanafunzi wa form six 1960-2014 walikua ni miamba kweli kweli, yaani mtu anatambulika karibu kijiji kizima kwamba kijana wa flani kafaulu, mimi binafsi nilikua nikikutana na mtu ameenda form five nilikua namuona watofauti saana, heshima nyingi mtaani, na matokeo yao miaka hiyo yalikua ni mabaya sana.

Refers matokeo ya ACSEE 2012. Hapa hata PCB mwenye three ya 15 alisoma udaktari...

View attachment 3042266View attachment 3042267View attachment 3042268View attachment 3042270View attachment 3042270
View attachment 3042271

Baada ya hapo kikaingia kizazi cha 2000, ambapo tunawaona kama wazinguaji, wasiokua na maadili lakini wananyoosha balaa, fikiria zamani shule zilikua zinajulikana, minaki, Milambo, pugu, n.k...

Lakini sasa hivi madogo wanaenda shule za hovyo, shule inaitwa kasangezi, sijui Ziba ya huko igunga lakini wanapasua balaa.
Miaka hii kusoma udaktari bila division 1 point 6 hupati udaktari...

View attachment 3042275View attachment 3042276

Swali je madogo wa siku hizi wanauelewa kuliko wa miaka ya zamani? Mtaala hujabadilika sana waliosoma biology 2005 bs, ndio wanachokisoma watoto wa sikuhizi.

Pia soma:Matokeo Kidato cha Sita 2024 yatoka. Ufaulu wapanda kwa asilimia 0.26

Ukichunguza matokeo ya wanafunzi wa form six 1960-2014 walikua ni miamba kweli kweli, yaani mtu anatambulika karibu kijiji kizima kwamba kijana wa flani kafaulu, mimi binafsi nilikua nikikutana na mtu ameenda form five nilikua namuona watofauti saana, heshima nyingi mtaani, na matokeo yao miaka hiyo yalikua ni mabaya sana.

Refers matokeo ya ACSEE 2012. Hapa hata PCB mwenye three ya 15 alisoma udaktari...

View attachment 3042266View attachment 3042267View attachment 3042268View attachment 3042270View attachment 3042270
View attachment 3042271

Baada ya hapo kikaingia kizazi cha 2000, ambapo tunawaona kama wazinguaji, wasiokua na maadili lakini wananyoosha balaa, fikiria zamani shule zilikua zinajulikana, minaki, Milambo, pugu, n.k...

Lakini sasa hivi madogo wanaenda shule za hovyo, shule inaitwa kasangezi, sijui Ziba ya huko igunga lakini wanapasua balaa.
Miaka hii kusoma udaktari bila division 1 point 6 hupati udaktari...

View attachment 3042275View attachment 3042276

Swali je madogo wa siku hizi wanauelewa kuliko wa miaka ya zamani? Mtaala hujabadilika sana waliosoma biology 2005 bs, ndio wanachokisoma watoto wa sikuhizi.

Pia soma:Matokeo Kidato cha Sita 2024 yatoka. Ufaulu wapanda kwa asilimia 0.26


Huenda idadi ya nafasi za Shule zimejengwa nyingi kuliko zamani ?!

Mwingine akasema wakati wa awam ilopita ile nidhamu ya woga ilipelekea kufaulisha kuogopa kutumbuliwa iwapo kutatokea some failures ?!

Mwingine akawaza huenda holo limeongezwa? Kitu ambacho kinatia shaka maana kanuni za size ya goli zinapaswa kuzingatiwa bila kujali kitakachojili?!
Hii Mbona inaweza kuwa ni risk kwa hatima ya elimu ya wasomi ?!

Ukweli ni upi sasa?
 
Mi naona zamani vyuo vilikua vichache sana so watu wengi wakifaulu ilikua ni hatari kwa wizara, itawapeleka wapi?. So walikua na idadi fulani ya watu wanaotakiwa kufaulu ili wasije kuzidi idadi ya vyuo vilivyopo nchini. Walikua wanastandardize matokeo.

Siku hizi vyuo ni vingi sana na vinahitaji watu, hakuna haja ya kufelisha watoto. Nina ndugu zangu wa karibu ni walimu na wanahusika kwenye marking ya mitihani ya NECTA. Wanasema kwamba mwanafunzi akiwa na idea tuu hata kama ni kidogo inatakiwa umpe marks. Ukimkosesha basi msimamizi lazima akuzingue.

Tukubali tuu zama zimebadirika pia mfumo unawabeba. Tukikaza sana hivyo vyuo tutafugia kuku 🤣🤣🤣🤣
 
Urahisi wa kupata materials, urahisi wa kuhama shule, urahisi wa maisha pia.

Zamani ukipangiwa pugu basi ni pugu tu, huwezi kuhama, utakomaa hapo hapoa hata kama magonjwa nyemelezi yanakushambulia, hata kama hamna walimu na changamoto kama hizo.

Ila miaka hii, ukiona shule haikufai kuna uwezekano wa kuhama kwenda private schools au government school unayoona inakufaa.

Sababu ni nyingi mkuu, na huenda maswali hayatofautiani saana ila ule urahisi wa kupata majibi ya hayo maswali umerahisishwa zaiidi.

Je zamani mlikua na past papers?? Lakini sasa kuna past papers za hadi miaka ya 90 huko ni mwanafunzi mwenyewe achague maswali ya kukomaa nayo, na uzuri au ubaya ni kua maswali yanajirudia.
Mkuu hakika miaka ya 1998_2003 kuhama shule ilikuwa mziki,ukimuambia mzazi naye anakushangaa.
 
Mi naona zamani vyuo vilikua vichache sana so watu wengi wakifaulu ilikua ni hatari kwa wizara, itawapeleka wapi?. So walikua na idadi fulani ya watu wanaotakiwa kufaulu ili wasije kuzidi idadi ya vyuo vilivyopo nchini. Walikua wanastandardize matokeo.

Siku hizi vyuo ni vingi sana na vinahitaji watu, hakuna haja ya kufelisha watoto. Nina ndugu zangu wa karibu ni walimu na wanahusika kwenye marking ya mitihani ya NECTA. Wanasema kwamba mwanafunzi akiwa na idea tuu hata kama ni kidogo inatakiwa umpe marks. Ukimkosesha basi msimamizi lazima akuzingue.

Tukubali tuu zama zimebadirika pia mfumo unawabeba. Tukikaza sana hivyo vyuo tutafugia kuku 🤣🤣🤣🤣
Hakika mkuu
 
Wazee mimi ntaleta mrejesho mwaka kesho nta_reseat japo imepita miaka 12 toka nihitimu kidato cha sita. ntarudia mtihani PCM matoke ntayopata ndo nta comfirm nachokiamini kuwa saivi elimu yetu kila mtu ni kufaulu tu.

mwaka huo tuliosoma PCM hakuna mtu naemjua alie pata one
, physics kuna mtu mmoja tu ndo namjua aliye pata C, kuna mshikaji wangu ni engineer alikuwa na E physics.

Mwaka jana kuna mdogo wangu PCB alipata one ya nane nilikuwa namfanyia application cha kushangaza akawa hapati chuo(alikuwa anataka medicine), huyu dogo O'level alikuwa na one ya 11 form two one ya 7, lakini nilikuwa namfundisha naona kabisa kichwani mweupe yaani hana maajabu yoyote.
Usisahau kuleta mrejesho mkuu📌
 
Back
Top Bottom