Wanafunzi wa shule za upili wa Taasisi ya Confucious UDSM Tanzania watembelea kijiji cha kale cha Siping na jumba la maonyesho la mji wa Jinhua

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121

Tarehe 22, Juni, wanafunzi wa shule za upili wa Taasisi ya Confucious katika chuo kikuu cha Dar es Salaam Tanzania (UDSM) wametembelea kijiji cha kale cha Siping na jumba la maonyesho la mji wa Jinhua.

Kijiji cha Siping kilichoko katika mlima Jiufeng mjini Jinhua, kilijengwa mwanzoni mwa enzi ya Ming, ambacho ukubwa wake ni mita za mraba 6,000. Ukuta wa majengo kijijini umechongwa picha mbalimbali za ndege, wanyama, maua na kadhalika, ambao una thamani kubwa ya kihistoria na kiutamaduni. Kijiji hicho kimewekwa kwenye orodha ya vijiji maarufu vyenye historia na utamaduni vya China mwaka 2010.

Wanafunzi hao walitembea katika kijiji hicho, kujionea mandhari nzuri ya kijiji na kuzungumza na wanakijiji.



Wanafunzi na walimu wanapiga picha kwa pamoja nje ya lango la kijiji cha Siping



Wanafunzi wanatazama samaki wa rangi aina ya “Koi Fish”.



Wanafunzi wanatembea kwenye vichochoro kijijini Siping



Wanafunzi wanapiga picha pamoja na wanakijiji



Wanafunzi wanatazama vinyago vya kichina


Wanafunzi wanajifunza chesi ya Go



Wanafunzi wanajaribu mchezo wa Touhu



Wanafunzi wanatazama kisima





Wanafunzi wakikaa ndani ya shule ya Chongde​

Siku hiyo mchana, wanafunzi hao walikwenda jumba la maonyesho la mji wa Jinhua. Jumba hilo linaonyesha historia ya maendeleo ya mji wa Jinhua na mpango wa maendeleo ya mji huo kwa kutumia teknolojia ya VR, modeli ya kidijitali, 3D na teknolojia nyingine za kisasa. Wanafunzi hao walishangaa kuona kasi ya maendeleo ya mji wa Jinhua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…