Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini wamefanya harambee ya kuwachangia Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassani pamoja na Rais wa zanziba Dkt.Hussein Mwinyi Fedha za kuchukua fomu ya ugombea Urais 2025 ikiwa ni katika hatua za kuwaonga mkono kutokana na kazi nzuri walizozifanya tangu kuingia madarajani.
Kwa vimbwanga na vituko vingine kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ruka hapa: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Wakiongozwa na rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini Zaynab Kitima kupitia kikao cha seneti kilichofanyika jijini Mbeya wanafunzi hao wamesema moja kati ya sababu zilizowafanya kumuunga mkono Dkt Samia ni pamoja na mazingira bora aliyoyaweka kwa wanafunzi ikiwemo bajeti ya fedha ya mikopo kuongezeka zaidi sambamba na wanafunzi wa vyuo vya kati kupata mikopo ya elimu ya juu.
Katika harambee hiyo wanafunzi hao wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni moja ambayo wamesema wataikabidhi kwa mkuu wa mkoa wa mbeya Juma homera ili aweze kuzikabidhi kwa Rais Dkt Samia.
Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini wamefanya harambee ya kuwachangia Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassani pamoja na Rais wa zanziba Dkt.Hussein Mwinyi Fedha za kuchukua fomu ya ugombea Urais 2025 ikiwa ni katika hatua za kuwaonga mkono kutokana na kazi nzuri walizozifanya tangu kuingia madarajani.
Kwa vimbwanga na vituko vingine kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ruka hapa: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Wakiongozwa na rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini Zaynab Kitima kupitia kikao cha seneti kilichofanyika jijini Mbeya wanafunzi hao wamesema moja kati ya sababu zilizowafanya kumuunga mkono Dkt Samia ni pamoja na mazingira bora aliyoyaweka kwa wanafunzi ikiwemo bajeti ya fedha ya mikopo kuongezeka zaidi sambamba na wanafunzi wa vyuo vya kati kupata mikopo ya elimu ya juu.
Katika harambee hiyo wanafunzi hao wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni moja ambayo wamesema wataikabidhi kwa mkuu wa mkoa wa mbeya Juma homera ili aweze kuzikabidhi kwa Rais Dkt Samia.