Pre GE2025 Wanafunzi wa vyuo wamchangia Rais Samia na Rais Mwinyi fedha ya fomu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ningewaona wa maana kila Mwaka wangekuwa wanachangia wenzao wengi waliokosa mikopo sababu ya hao hao watunga sera kushindwa ku deliver

Lakini I know better hao wapo kazini ukizingatia na hizi njaa hapo akaunti zao zimesoma extra digits
 
Wamemchangia fomu ya nini au wamempa pesa ya kununua Abbaya
 
Hivi kweli pocket money za wanafunzi zinatumika kumchangia Samia fedha?
 
Hao ni mwendelezo wa kizazi cha kujikomba, sio ajabu siku hizi wawekexaji wanapenda kuja na staff wao kutoka nje na mimi naona ni sawa, Hao hakina kitu wanacho kijua zaidi ya uchawa.

Na hii ni only in Tanzania hakuna Taifa utakutana huo ujinga.
 
Hao hakuna wanacho waza vichwani mwao zaidi ya uchawa, na wana ona dio nji pekee ya wao kuajiriwa,
 
Hao njia pekee wanayo ona ya wao kuajiriwa au kupata kazi ni kupitia kujikomba hao hata kushikishwa ukuta ni rahisi sana
 
Mwaka wa Uchaguzi huu, tutaona na kusikia mengi

Ila ninachokumbuka, wakati nasoma Chuo Kikuu hatukuwahi kumchangia Rais kumlipia Fomu ya kugombea Urais

Maana hata boom lenyewe lilikuwa halitoshi, ila hawa Wanafunzi wetu Wana fedha hadi nyingine kufanya ziada ya kumnunulia Fomu ya kugombea Madam President šŸ™Œ
 
Ndio maana nikiona kijana msomi kakosa ajira nafurahi.
Vijana wa kulikomboa Taifa wao wanamuunga mkono muuza rasilimali zao
 
Adui namba moja wa nchi yetu ni chawa. Bila kupata dawa ya chawa tutaendelea kupiga mark time tu!
 
Mzungumzaji hajakaa kimkakati na ushawishi, amekaa kipambe🤣🤣 Mkitangaza nafasi za kazi ajirini watu wenye sifa sio watoto wa mjomba🤣🤣
 
Mtu aliyeanzisha mchango kusaidia walioangukiwa na jengo Kariakoo alikamatwa na polis kwa kuchangisha. Wasomi wanachangishana kwa ajili ya fom, polisi wapo kimyaaaa.
Hii ndio Tanzania.
 
Naomba orodha ya waliochanga kama kuna mdogo wangu amefanya huu upumbavu asahau support na asiniombe hela hata mia.
 
Mtu aliyeanzisha mchango kusaidia walioangukiwa na jengo Kariakoo alikamatwa na polis kwa kuchangisha. Wasomi wanachangishana kwa ajili ya fom, polisi wapo kimyaaaa.
Hii ndio Tanzania.
sahivi hatuna vyuo tuna shule za msingi zilizochangamka, mtu ana degree hawezi hata kujieleza yeye mwenyewe hata akiambiwa aeleze historia yake mwenyewe kwa kiswahili achana na kiingireza.
 
Uchawa ata best. Pesa yenyewe inatokana ima na uchawa, umalaya au kujikomba mbali na mikopo ya kuvutana. Namna hii, hakuna wasomi bali watu wanaopoteza muda darasani bila kuelimika. Huwa naita hii education for ignorance vinginevyo hiyo pesa wawe wapewa na yule wanaye 'changia' kupata ujiko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…