Wanafunzi watatu wafariki kwa kukosa hewa wakati wanatoa mahindi kwenye kihenge cha shule, mwalimu aliwaacha na kwenda kunywa chai

Wanafunzi watatu wafariki kwa kukosa hewa wakati wanatoa mahindi kwenye kihenge cha shule, mwalimu aliwaacha na kwenda kunywa chai

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Wanafunzi sita wa shule ya mtakatifu John Paul II ya mkoani Shinyanga walienda kutoa mahindi kwenye kihenge cha shule lakini yalishindwa kutoka wakiwa na mwalimu wa zamu katika usimamizi wa chakula, mwalimu alielekeza wanafunzi watatu waingie ndani kutafuta namna ya kuyafungulia kisha akaenda kunywa chai. Baada ya muda kupita, wanafunzi watatu waliobaki nje wakaona wenzao hawatoki na kutoa taarifa kwa walimu.

Walimu walipofika waliita bila mafanikio, wakavunja kihenge na kukuta wamezirai. Baada ya kufikishwa zahanati ya shule matibabu hayakuleta majibu na kukimbizwa hospitali ya Kahama ikathibitishwa wamefariki kutokana na kukosa hewa safi.

Kaimu kamanda wa Polisi, ACP Kennedy Mgani amesema Mwalimu wa zamu, Morris Sileo anashkiliwa na Jeshi la Polisi kwa kushindwa kusimamia vyema ili kubaini uchunguzi na chanzo cha vifo cha wanafunzi hao.
 
So bad, so sad

 
Wanafunzi sita wa shule ya mtakatifu John Paul II ya mkoani Shinyanga walienda kutoa mahindi kwenye kihenge cha shule lakini yalishindwa kutoka wakiwa na mwalimu wa zamu katika usimamizi wa chakula, mwalimu alielekeza wanafunzi watatu waingie ndani kutafuta namna ya kuyafungulia kisha akaenda kunywa chai. Baada ya muda kupita, wanafunzi watatu waliobaki nje wakaona wenzao hawatoki na kutoa taarifa kwa walimu.

Walimu walipofika waliita bila mafanikio, wakavunja kihenge na kukuta wamezirai. Baada ya kufikishwa zahanati ya shule matibabu hayakuleta majibu na kukimbizwa hospitali ya Kahama ikathibitishwa wamefariki kutokana na kukosa hewa safi.

Kaimu kamanda wa Polisi, ACP Kennedy Mgani amesema Mwalimu wa zamu, Morris Sileo anashkiliwa na Jeshi la Polisi kwa kushindwa kusimamia vyema ili kubaini uchunguzi na chanzo cha vifo cha wanafunzi hao.
Hivi hatujifunzi tuu kuhusu hivi vihenge?, vimeshaua watu sana
 
Hizi matukio mbona ni zile zile za kujirudia. Hatujajifunza bado?
Poleni wafiwa.
Huenda mahindi yalikuwa na dawa ya kuhifadhi nafaka ambayo imehusika kurahisisha vifo vya watoto hao.
Pia nadhani hakuna wataalam wa management ya wahanga wa matukio kama hayo.
Kama zahanati ya Buzwagi ingekuwepo huenda wangeokolewa.
 
Kwa hiyo limejirudia tena ?
Kwanini hawakutangaza nchini nzima na shule zote madhara haya? Mpaka watoto wanakufa?

Lazima wabebe lawama waalimu au mwalimu, ina maana hajui madhara
 
Back
Top Bottom