Mkuu; huo mfumo hauna tatizo . Tatizo lipo kwa WATUMIAJI. Kama mtumiaji anashindwa kufuata maelekezo na Tahadhari zilizotolewa au kuelekezwa namna mfumo huo unavyofanya kazi na ni Tahadhari gani za kuzingatiwa, hiyo inakuwa ni uzembe wa mtumiaji na kwa mantiki hiyo sio sahihi kusema Mfumo huo ukatazwe. Wakatazwe wale wazembe wanaoutumia mfumo huo bila ya kuuelewa vizuri au kuwashirikisha wataalam husika.