Wanajeshi 60 wa Tanzania huko Afrika ya kati kurejeshwa nyumbani kwa tuhuma za unyanyasaji wa kingono

Wanajeshi 60 wa Tanzania huko Afrika ya kati kurejeshwa nyumbani kwa tuhuma za unyanyasaji wa kingono

Hawabaki, sawasawa na chuoni mwanachuo kuwa na mahusiano na lecture au mkufunzi, kutaka unafuu fulani, kwakuwa wanakuwa watoto ndo kubaka kwenyewe, Kama mtu unabakwa si unakimbia kambi, unatoroka pori kwa pori, unarudi home.
 
jeshi la nchi za kiarabu misri algeria sudan uae kuweit yemen rusia saudia china korea wapi ulisikia jeshi la nchi hizi zinabaka wanawake?
Fuatilia kabla hujataja jeshi la nchi yeyote , kutowasikia haimaanish hawafanyi , bali fuatilia kwanza
 
Mkuu, Una Experience na nchi gan zingine ulowahi fika na kufaham tabia na vipaumbele vyao, hadi uka conclude kuwa Tanzania ndo giant wa ngono?
Sw ila tukemee hao wachache , lasivyo utakemea siku umebakwa ww au kabakwa mtu wa karibu yako
 
Walinda amani wa Tanzania kurejeshwa nyumbani kutokana na madai ya utovu wa nidhamu CAR

9 Juni 2023Haki za binadamu

Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) chenye makao yake makuu mjini Bangui, kimetangaza uamuzi wa Sekretarieti, kuwarudisha nyumbani kikosi cha wanajeshi 60 wa Tanzania, waliokuwa wametumwa katika kambi ya muda ya operesheni katika eneo la magharibi mwa nchi hiyo kufuatia madai makubwa ya matendo ya unyanyasaji wa kingono yanayodaiwa kutekelezwa na walinda amani hao, msemaji wa Umoja wa Mataifa amewaeleza walinda waandishi wa Habari hii katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani.

Msemaji wa Katibu Mkuu wa UN, Stéphane Dujarric, amesema, "Uamuzi huo unakuja baada ya uchunguzi wa awali ambao ulipata ushahidi wa kuaminika kwamba walinda amani 11 wa kitengo hicho walidaiwa kujihusisha na unyanyasaji wa kingono kwa waathirika wanne.”

Akifafanua zaidi Dujarric amesema, “Waathiriwa waliotambuliwa wanapatiwa matunzo na usaidizi kutoka kwa wadau wa operesheni za kibinadamu. MINUSCA pia imetuma timu ili kuzungumza zaidi na jamii.

Tanzania imetuma wachunguzi

Kwa mujibu wa Dujarric, “Mamlaka za Tanzania zimearifiwa rasmi na zimetuma maafisa wa uchunguzi wa kitaifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. Katika kuthibitisha dhamira yao ya kutovumilia kabisa unyanyasaji wa kijinsia na kingono, mamlaka za Tanzania zilibaini uzito wa tuhuma hizo na wamejitolea kuchukua hatua zinazohitajika kushughulikia masuala haya.”

Msemaji huyo amesema, “Kikosi kimehamishwa na kupelekwa katika kambi nyingine huku uchunguzi ukiendelea, na wahusika wa kitengo hicho wamezuiliwa kwenye kambi, hii ni kwa ajili ya kuwalinda waathirika na bila shaka uadilifu wa uchunguzi. Kikosi hicho kitarejeshwa nyumbani pindi ambapo uwepo wao hautahitajika tena kwa wachunguzi.”

Vilevile Dujarric ameeleza, “Uamuzi wa Sekretarieti kurudisha kikosi hiki ni kwa mujibu wa azimio namba 2272 la Baraza la Usalama, ambapo Baraza 'linaidhinisha uamuzi wa Katibu Mkuu wa kurudisha nyumbani kikosi fulani cha kijeshi au kuunda kitengo cha polisi cha kikosi wakati kuna ushahidi wa kuaminika wa unyanyasaji wa kingono ulioenea au wa kimfumo unaofanywa na kitengo hicho'.

Msemaji huyo wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, "Umoja wa Mataifa unasalia na nia ya kutekeleza kwa dhati sera ya Katibu Mkuu ya kutovumilia kabisa unyonyaji na unyanyasaji wa kijinsia."


=====
The United Nations will send home a unit of 60 Tanzanian peacekeepers over allegations of sexual exploitation and abuse in the Central African Republic, the UN announced on Friday.

A preliminary investigation found “credible evidence” that eleven members of the unit were involved in sexual exploitation and abuse of four victims, UN spokesman Stephane Dujarric said.

Two of the alleged victims are children, according to UN figures.

Investigators also identified a breakdown in commanders’ authority and management of staff, according to a press release by the UN’s mission in the country.

The victims have received care from humanitarian groups working with the UN, according to their “medical, psychosocial and protection” needs, it said.

The UN has had a mission in the conflict-torn Central African Republic since 2014, where thousands of peacekeepers have been deployed.

The eleven suspects had been working at a temporary base in the west of the country. The Tanzanian unit has now been relocated to another base and its members confined to the barracks.

“The unit will be repatriated once their presence is no longer required by the investigation,” Dujarric said.

Tanzanian authorities have also dispatched investigation officers to the Central African Republic.

There have been allegations of sexual abuse or exploitation against Tanzanian peacekeepers – largely in the Democratic Republic of Congo – every year since at least 2015, UN figures show.


Hii taswira mbaya sana kwa Jeshi letu.
Yote haya wameyataka ccm
 
We hujui wale mademu wanatumia kama fursa ya kupata msaada wa UN hawajabakwa hao basi tu jumba bovu ili wapone njaa zao
Kwamb hao wanajeshi hawajui kuwa ni htr kuwa krb na hao wenyej wanaolindwa ?
 
Sio kwamba wanabaka directly Mzee..once ukitoka uku kwenda kulinda amani hutakiwi kufanya mapenzi na raia yeyote wa kule ata kama mmekubaliana inahesabika umebaka,ikijulikana au ukionwa tu kibarua huna tena uko Kwa taratibu zilivyo
Je wao hawaamim kuwa hao wanajeshi wana hisia , au ndo uchochez wa ushoga huu , tungekuwa na kiongoz timamu angekuwa anaomba wanajeshi wake wawe wanapewa muda wa kuja kufurahi na familia ili hisia zipungue
 
Je wao hawaamim kuwa hao wanajeshi wana hisia , au ndo uchochez wa ushoga huu , tungekuwa na kiongoz timamu angekuwa anaomba wanajeshi wake wawe wanapewa muda wa kuja kufurahi na familia ili hisia zipungue
Ndo maana wanapewa likizo kiongozi baada ya miezi.6
 
Umoja wa Mataifa ilitangaza Ijumaa (Juni 9) kuwa kikosi cha walinda amani 60 kutoka Tanzania kitarejeshwa nyumbani kutokana na madai makubwa ya unyanyasaji wa kingono.

Akiongea kutoka New York, msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alisema uchunguzi wa awali ulibaini kuwepo kwa waathirika 4.

"Mamlaka za Tanzania zimearifiwa rasmi na wamewatuma maafisa wa uchunguzi wa kitaifa kwenda Jamhuri ya Afrika ya Kati..."

Ushahidi ulioaminika ulipatikana dhidi ya wanajeshi 11 wa kikosi hicho kilichokuwa katika kituo sehemu ya Magharibi mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati.

"Kikosi hicho kimehamishwa kwenye kambi nyingine wakati uchunguzi unaendelea, na wanajeshi wa kikosi hicho wamezuiliwa kwenye makambi ya kijeshi, hii ni ili kulinda waathirika pamoja na uadilifu wa uchunguzi," alisema Dujarric.

"Kikosi hicho kitarejeshwa nyumbani mara tu uwepo wao hautahitajika tena katika eneo la tukio kwa mujibu wa wachunguzi..."

Dujarric alifafanua: "Uamuzi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kuwarejesha nyumbani wanajeshi hawa" ulizingatia azimio 2272 la Baraza la Usalama "ambapo Baraza linakubali uamuzi wa Katibu Mkuu wa kuwarejesha nyumbani kikosi cha kijeshi au kikosi cha polisi cha kikosi cha walinda amani fulani wakati kuna ushahidi unaokubalika wa unyanyasaji wa kingono uliokithiri au wa mifumo kutoka kwa kikosi hicho."

Umoja wa Mataifa ilirekodi kwenye tovuti yake kuwa tangu 2015, kulikuwa na tuhuma 254 za unyanyasaji wa kingono dhidi ya wanajeshi wake katika Ujumbe wake wa Umoja wa Mataifa wa Kuhuisha na Kuleta Utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati au MINUSCA.

Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, alitangaza mapema katika utawala wake sera ya "kutovumilia" unyanyasaji wa kingono na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, akiwataka Mataifa Wanachama kusaini mkataba wa hiari kuhusu kuzuia na kushughulikia janga hilo, mwaka 2017.

Tuhuma za unyonyaji na unyanyasaji wa kingono na wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa kote duniani ni pana.

Africa News
 
Back
Top Bottom