Wanajeshi wa Uingereza wanaacha kazi ya jeshi licha ya malipo bora

Wanajeshi wa Uingereza wanaacha kazi ya jeshi licha ya malipo bora

Na hivyo basi vita zote ambazo Uingereza hupigana inavuka bahari. Same effect, kama ni vigumu kuvamiwa kisa ni visiwa basi vilevile ni vigumu yenyewe kuvamia adui maana itatoka visiwani.

Kama bahari inaifanya Tanzania isiivamie Madagascar, bahari hiyohiyo si inaifanya Madagascar isiivamie Tanzania?
uingereza aliwahi kumvamia nani akiwa peke yake?
unaongelea historia ya miaka ya 1900 huko sio?
 
Vita hizo uingereza huzifuata mwenyewe, uingereza ingepakana na ujerumani kama poland, ingekua mhanga wa kwanza,kwa kipindi kile isingewezekana hitler avuke nchi zote aingie uingereza
Lakini Uingereza ikaweza kuvuka bahari kuifuata Ujerumani si ndio?

Hitler alijaribu kuvuka bahari kuifuata Uingereza ila Royal Navy ilikuwa na nguvu kuzidi Kriegsmarine. Royal Airforce iliweza kukabiliana na nguvu za Luftwaffe.
Kasome The Battle of Britain, Hitler alibeba maelfu ya ndege na melivita kupigana Uingereza. Zilikuwepo Britz ambapo Wajerumani wanadondosha mabomu kwenye miji ya Uingereza, nayo ikadondosha mabomu kwenye miji ya Ujerumani kama Dresden na Munich. Na ikalipua mabwawa ya umeme kusababisha mafuriko ya Ruhr industrial region ili silaha zisitengenezwe.

Hitler alivamia nchi alizoona ni wanyonge. Hadi aliivamia USSR baada ya kuona performance yao mbovu kwenye vita na Finland. Uingereza ndio ilitangaza vita kwa Ujerumani, na ilikuwa ya kwanza bila woga kwa kujiamini. Isingetangaza vita wala isingepigana na Ujerumani.
 
uingereza aliwahi kumvamia nani akiwa peke yake?
Na ni nani aliwahi mvamia Uingereza akiwa peke yake?

Anyway, Falklands war mwaka 1982 Uingereza iliendesha melivita na ndege umbali wa kilomita 11,000 kwenda kupigana na Argentina.
unaongelea historia ya miaka ya 1900 huko sio?
Miaka ya 1900 hizo nchi nyingine si zilikuwepo? Na si zilikuwa na majeshi?

Hata tukirudi miaka ya 1700 bado hizo nchi zote zilikuwa na majeshi. Britain ilipigana na kina Napoleon, Russian Empire, France, Ottomans na ilikuwa kwenye alliances nyingi na vita mchanganyiko za wakati mmoja na sometimes adui wa leo ni rafiki wa kesho.

Kuwatishia Waingereza na vita ni sawa na kumtishia Masai kunywa maziwa.
 
Lakini Uingereza ikaweza kuvuka bahari kuifuata Ujerumani si ndio?

Hitler alijaribu kuvuka bahari kuifuata Uingereza ila Royal Navy ilikuwa na nguvu kuzidi Kriegsmarine. Royal Airforce iliweza kukabiliana na nguvu za Luftwaffe.
Kasome The Battle of Britain, Hitler alibeba maelfu ya ndege na melivita kupigana Uingereza. Zilikuwepo Britz ambapo Wajerumani wanadondosha mabomu kwenye miji ya Uingereza, nayo ikadondosha mabomu kwenye miji ya Ujerumani kama Dresden na Munich. Na ikalipua mabwawa ya umeme kusababisha mafuriko ya Ruhr industrial region ili silaha zisitengenezwe.

Hitler alivamia nchi alizoona ni wanyonge. Hadi aliivamia USSR baada ya kuona performance yao mbovu kwenye vita na Finland. Uingereza ndio ilitangaza vita kwa Ujerumani, na ilikuwa ya kwanza bila woga kwa kujiamini. Isingetangaza vita wala isingepigana na Ujerumani.
Si kweli, bunge la uingereza walikaa vikao kujadili kupambana na ujerumani au waache , kwa maana hadi hapo Uingereza ilijua wazi haitoweza kupambana na ujerumani, ilikuwa mshike mshike bungeni, hawa wakisema hii vita hatuwezi wengine wakisema tupambane.

Haya masuala ya WWII ndio ilipelekea Chamberlain aka resign. ..

Haikuwa vyepesi hivyo, UK ilipambana kufa na kupona ..

Ujerumani ilipomnyong'onyeza UK ikaondoka kwa kufahamu itarudi baadae kummalizia, kipindi hiko UK imepigwa vibaya japo nakubali walikomaa piga nikupige.... Germans ndipo wakahamia kupambana kwa nguvu zote na wasovieti.
 
kuvamia kisiwa na ardhi tambarare ni sawa?
uingereza haiwezi kuvamiwa kirahisi kwa sababu ni kisiwa, na Urusi kuvamiwa na ukraine ni jambo la kawaida maana Urusi mara zote imekuwa ikivamiwa tokea upande huu wa ardhi ya Ukraine.....
Then mbona Uingereza huwa inatoka kwenye visiwa vyake inavamia hizo ardhi tambarare kupitia kwenye fukwe?

Kwani naval landing ya kwenye kisiwa na naval landing ya nchi iliyopo mainland ina tofauti gani? Wanajeshi wanaoenda kutua pwani ya kisiwa cha Unguja wanakumbana na kipi cha tofauti na wale wanaotua pwani ya bara pale Lindi au Mtwara?

Pote kuna mchanga, matumbawe, fukwe zenye kina kirefu na kifupi, wote wanatokea baharini ugumu ni uleule. Sasa mbona Britain always huwa inatoka visiwani inaenda kumpiga mtu kisha inarudi na meli?

Sasa kwa taarifa ni hivi, ni rahisi kuvamia kisiwa maana unakiwekea naval blockade kinakosa supplies. Ila ni vigumu kuivamia nchi kavu sababu ina njia nyingi za kupita, ndio sababu Japan ilipigwa na Marekani.
Na Uingereza ni ndogo kwa size haiifikii hata Tanzania ila inamudu kujilinda.

Tanzania ikipigana na Madagascar (assume wote tuna melivita na nyambizi) ni rahisi sisi kuweka naval blockade hata kwa sea mines tukasumbua meli za mizigo wafe njaa wakose na supplies, mafuta, spare parts, silaha, ammunition, vyakula. Ila wao wakizuia pwani yetu tuna options za kupitisha silaha Rwanda au Kenya au Uganda au Malawi au Congo au Msumbiji. Na hizo zote ni nchi huru ambazo hazingehusika na vita yetu.

Hakuna nchi iliwahi weka naval blockade kwa Britain wakati wako na disadvantage kijiografia.
kisiwa cha uingereza hakiwezi kuichukulia poa urusi kwa sababu hawajawahi kupigana......
btw uingereza haina uwezo mkubwa kijeshi, hata ingetokea akapigana na Ukraine atapigwa tena ukraine asingehitaji msaada kama anavyotegemea msaada leo!
Urusi na Uingereza huwa wanakutana kwenye alliances ambazo Urusi inapoteza wanajeshi wengi sana. Vita ya kwanza ya dunia Urusi ilipigwa na Ujerumani hadi ikakimbia vita mpaka mapinduzi yakafanyika. Walikula hasara kiuchumi na hawakuambulia kitu, hawakutimiza hata lengo moja.
Wakati Uingereza ilibaki na ikashinda.

Kwenye WW2 Urusi ikawa upande uleule wa Uingereza. Warusi wakafa wengi zaidi ya milioni 20 kuliko nchi nyingine wakati walikuwa front moja kwao. Waingereza hata pua ya Mjerumani haikuonekana kwenye ardhi yao. Walipigania North African theater hasa Misri na Tunisia, Mediterranean sea, Atlantic, mainland Europe kwenye Western front kuanzia Ufaransa, Holland, Belgium na Ujerumani kwenyewe.

Na sio Waingereza tu, hata Wafini hawawachukulii Warusi kama wazuri kimedani.
 
Si kweli, bunge la uingereza walikaa vikao kujadili kupambana na ujerumani au waache , kwa maana hadi hapo Uingereza ilijua wazi haitoweza kupambana na ujerumani, ilikuwa mshike mshike bungeni, hawa wakisema hii vita hatuwezi wengine wakisema tupambane.

Haya masuala ya WWII ndio ilipelekea Chamberlain aka resign. ..

Haikuwa vyepesi hivyo, UK ilipambana kufa na kupona ..

Ujerumani ilipomnyong'onyeza UK ikaondoka kwa kufahamu itarudi baadae kummalizia, kipindi hiko UK imepigwa vibaya japo nakubali walikomaa piga nikupige.... Germans ndipo wakahamia kupambana kwa nguvu zote na wasovieti.
Nilichoandika ambacho si kweli ni nini mkuu. Si kweli kwamba Uingereza ndio ilitangaza vita dhidi ya Ujerumani?
Bila Ujerumani kuivamia Uingereza wala kuitishia. Kasome tena.

Chamberlain alijiuzuru sababu alikuwa na Appeasement Policy, ile mtoto wa jirani ni mwizi ila tumuonyeshe upendo tuyazungumze. Wakati Churchill alikuwa anaamini hakuna kucheka na mwizi. Hitler alipovamia Poland ikaonekana Appeasement ni upuuzi, Chamberlain akaachia ngazi na akapendekeza Churchill ndio ashike usukani wakati enzi za amani Churchill alionekana warmonger na bungeni alitolewa.

Ujerumani haikuondoka Uingereza eti itarejea. Iliondoka sababu uwezekano wa kuipiga Uingereza ulikuwa ni sifuri ilikuwa inapoteza ndege na meli bure, wakati Uingereza haina kitu in return endapo itatekwa. Ni visiwa hata kilimo hawana, mafuta hawana, population hawana, madini hawana yani ni hasara na ni wakorofi wako organized. Ikatafutwa nchi yenye kila kitu na ni ya kinyonge ni Urusi, ikavamiwa hiyo.

Ila Uingereza ikawafuata ingawa Hitler alitaka waache vita. Sasa unasemaje iliwekwa kiporo, wakati iliwadhibiti vitani Hitler akaleta mazungumzo tena bila sharti lolote.
 
Nilichoandika ambacho si kweli ni nini mkuu. Si kweli kwamba Uingereza ndio ilitangaza vita dhidi ya Ujerumani?
Bila Ujerumani kuivamia Uingereza wala kuitishia. Kasome tena.

Chamberlain alijiuzuru sababu alikuwa na Appeasement Policy, ile mtoto wa jirani ni mwizi ila tumuonyeshe upendo tuyazungumze. Wakati Churchill alikuwa anaamini hakuna kucheka na mwizi. Hitler alipovamia Poland ikaonekana Appeasement ni upuuzi, Chamberlain akaachia ngazi na akapendekeza Churchill ndio ashike usukani wakati enzi za amani Churchill alionekana warmonger na bungeni alitolewa.

Ujerumani haikuondoka Uingereza eti itarejea. Iliondoka sababu uwezekano wa kuipiga Uingereza ulikuwa ni sifuri ilikuwa inapoteza ndege na meli bure, wakati Uingereza haina kitu in return endapo itatekwa. Ni visiwa hata kilimo hawana, mafuta hawana, population hawana, madini hawana yani ni hasara na ni wakorofi wako organized. Ikatafutwa nchi yenye kila kitu na ni ya kinyonge ni Urusi, ikavamiwa hiyo.

Ila Uingereza ikawafuata ingawa Hitler alitaka waache vita. Sasa unasemaje iliwekwa kiporo, wakati iliwadhibiti vitani Hitler akaleta mazungumzo tena bila sharti lolote
Si kweli, Nazi Germany haikuiona Soviet kama vibonde, Urusi ndio ilipelekea Hitler na wenzake kujimaliza na familia zao baada ya kusikia msoviet akigonga hodi kutoka eastern front na si Britain wala USA....

WW2 UK haikuwa na uwezo kijeshi kama USSR acheni ushabiki na history ambazo ni biased... UK alipigana akashukuru Mungu Germany ameondoka, lakini USSR akiwa peke yake eastern front aliwasukuma askari wa Germany hadi Berlin na ndio walikuwa wa kwanza kuingia Berlin, Allies wasingeshinda hivyo vita pasipo msoviet...

Britain walikuwa urojo tu mbele ya USSR tuacheni story za kwenye kahawa....
 
Anyway, Falklands war mwaka 1982 Uingereza iliendesha melivita na ndege umbali wa kilomita 11,000 kwenda kupigana na Argentina.
Nina swali kwanini 1982 hawakuendesha melivita mpaka kisiwa cha Hong-Kong kwenda kupigana na China ?
 
kuvamia kisiwa na ardhi tambarare ni sawa?
uingereza haiwezi kuvamiwa kirahisi kwa sababu ni kisiwa, na Urusi kuvamiwa na ukraine ni jambo la kawaida maana Urusi mara zote imekuwa ikivamiwa tokea upande huu wa ardhi ya Ukraine.....

kisiwa cha uingereza hakiwezi kuichukulia poa urusi kwa sababu hawajawahi kupigana......
btw uingereza haina uwezo mkubwa kijeshi, hata ingetokea akapigana na Ukraine atapigwa tena ukraine asingehitaji msaada kama anavyotegemea msaada leo!
Kumekucha
 
Si kweli, Nazi Germany haikuiona Soviet kama vibonde, Urusi ndio ilipelekea Hitler na wenzake kujimaliza na familia zao baada ya kusikia msoviet akigonga hodi kutoka eastern front na si Britain wala USA....

WW2 UK haikuwa na uwezo kijeshi kama USSR acheni ushabiki na history ambazo ni biased... UK alipigana akashukuru Mungu Germany ameondoka, lakini USSR akiwa peke yake eastern front aliwasukuma askari wa Germany hadi Berlin na ndio walikuwa wa kwanza kuingia Berlin, Allies wasingeshinda hivyo vita pasipo msoviet...

Britain walikuwa urojo tu mbele ya USSR tuacheni story za kwenye kahawa....
Lakini kumbuka, nguvu ya Russia ya wakati wa ww2 hauwezi linganisha na nguvu iiliyonayo leo, sielewi ni mazingira ama utawala!

Iweje Ukraine nchi iliyokuwa ni mkoa wake ihangaike nayo kwa zaidi ya miaka miwili, je ikipambana na Uingereza sasa, jino kwa jino, bado utaitabiria ushindi Russia?
 
Nina swali kwanini 1982 hawakuendesha melivita mpaka kisiwa cha Hong-Kong kwenda kupigana na China ?
Kwa sababu Hong Kong sio sehemu ya Uingereza. Wala China haikuishambulia Uingereza. Wala raia wa Hong Kong hawajawahi omba rescue kutoka kwa Uingereza.

Soma kwanini Uingereza iliingia Falklands.
 
Uingereza hawalipi vizuri wanajeshi hasa sailors. Report yako inasema "malipo yameongezwa" ila haitokaa itokee malipo ya civilian market yawe juu ya malipo ya defence contractors. Kwa nchi nyingine ni hivyo ila kwa Uingereza ni vibaya zaidi.

Mfano ili mtu awe Royal Navy submarine captain anatakiwa awe na akili sana, experience kubwa, uwezo binafsi wa hali ya juu, ana risk kubwa ya kuachishwa kazi, hana option ya kuhama kazi sababu submarines zinamilikiwa na serikali na hawezi hama jeshi kutoka Uingereza kwenda labda Spain. Na bado submarines ni chache na zina kazi ngumu.

Wakati mtu mwenye uwezo mdogo nusu ya submarine captain anaweza ajiriwa na shirika la ndege la Uingereza, British Airways akalipwa mshahara uleule, kazi nyepesi kabisa, uzoefu wa kawaida, options za kuacha kwenda mashirika mengine zipo nyingi, risks za kuachishwa kazi ni chache, kuna uhuru wa kufanya kazi, na ndege zipo nyingi shirika hilo au mashirika mengine. Na kazi ina bonus.

Popote pale mtu mwenye uwezo mkubwa anaweza kupata kazi nzuri kwenye civilian market kuliko jeshini. Ford, Tesla, BYD, Volkwagen wanatengeneza mamilioni ya magari models mpya kila mwaka na kila miaka kama mitano magari yanaharibika wateja wananunua mengine. Wakati mfano kampuni ya Nexter ya Ufaransa tangu iunde Leclerk main battle tank mwaka 1992 mpaka leo haijawahi unda type nyingine na wateja ni nchi kama tatu tu, na vifaru vyote vilivyoundwa tangu mwaka huo bado vipo. Imagine design engineer wa hiyo kampuni ana miaka kadhaa hajawahi lipwa bonus wakati waliopo Volkwagen wanafyatua magari tu.

Boeing B-52 Stratofortless zimeanza kuundwa tangu 1952 na ya mwisho iliundwa 1962 ila mpaka leo zipo zinafanyiwa upgrade tu. Wakati Boeing za abiria zinauzwa maelfu kila mwaka na kila muongo wanatoa products kadhaa mpya kwenye assembly line na kila miaka kama 20 ndege inaacha kutumika. Hivyo kimauzo huwezi tegemea engineer wa military market alipwe sawa na civilian market. Same thing na jeshini.

Hata kwenye software, engineers waliounda NATO Link 16 walimaliza 1970s, Link 22 ni ya 1980s na mpaka leo ndio zinatumika kwenye communications zote za ndege za NATO. Wakati kwenye civilian market consumers huwa wanachoka kitu bila sababu za msingi. Windows 11 na 10 zina tofauti ndogo sana, ila watu wamelipwa kutoa Windows 11. Android versions kila mwaka, iOS kila mwaka. 3G, 4G, 5G na 6G iko njiani.

Hela zinamwagwa kwenye research na kuna malipo, marupurupu, zawadi, recognition na sense of accomplishment. Kwenye soko huru its likely watu wenye uwezo mkubwa wasiende jeshini.
Kenyan Airforce miaka ya 70s ndio ilikuwa inapeleka marubani kusoma bure ili waendeshe ndegevita, matokeo yake wakirudi wanaenda civilian market kuendesha East African Airways, last week Rais wa Nigeria amesaini sheria maofisa wa jeshi lazima watumikie miaka si chini ya 15. Walikuwa na tabia ya kusomeshwa bure wanapata ujuzi unaolipa vizuri mtaani kisha wanafanya kazi miaka michache jeshini na kuacha kazi. Mnahisi kwanini Wahindi waliacha kujiunga na JWTZ?
Vita ya chupa bar umetumia icbm
We jamaa heshima Yako kubwa kwangu ktk maswala hayo
Ningependa kujua kwanini wahindi hawaendi jwtz
 
Wanajeshi wa Uingereza wanaacha kazi ya jeshi bila sababu za msingi,licha ya mshahara mzuri wanaolipwa,sababu. Ni Nini?

UK soldiers quit in thousands despite Labour's pay rise

Soldiers are quitting the British Armed Forces at an alarming rate, despite a pay rise over the summer, Report informs via The Telegraph. For the first time on record, there are now just two servicemen or women per thousand people in Britain. Some 15,119 left the Armed Forces in the year to October.8 hours ago
Report İnformasiya Agentliyi › other-countries

Soldiers are quitting the Armed Forces at an alarming rate, despite a pay rise over the summer.

For the first time on record, there are now just two servicemen or women per thousand people in Britain.

Some 15,119 left the Armed Forces in the year to October. Of these, 7,778 were counted as “voluntary outflow”, those choosing to leave of their own accord.

*****†**********
December 22, 2024 15:04
UK soldiers quit in thousands despite Labour’s pay rise
UK soldiers quit in thousands despite Labour’s pay rise
Soldiers are quitting the British Armed Forces at an alarming rate, despite a pay rise over the summer, Report informs via The Telegraph.

For the first time on record, there are now just two servicemen or women per thousand people in Britain.

Some 15,119 left the Armed Forces in the year to October. Of these, 7,778 were counted as “voluntary outflow”, those choosing to leave of their own accord.

The forces recruited just over 12,000 personnel in the same period, resulting in a net shrinkage of the military.

Soldiers are leaving despite the Government’s attempt to stem the recruitment crisis with a 6 per cent pay rise.
Sio kwamba wote ni mashoga na hawapendi kazi ngumu ni sex tu
 
Wanajeshi wa Uingereza wanaacha kazi ya jeshi bila sababu za msingi,licha ya mshahara mzuri wanaolipwa,sababu. Ni Nini?

UK soldiers quit in thousands despite Labour's pay rise

Soldiers are quitting the British Armed Forces at an alarming rate, despite a pay rise over the summer, Report informs via The Telegraph. For the first time on record, there are now just two servicemen or women per thousand people in Britain. Some 15,119 left the Armed Forces in the year to October.8 hours ago
Report İnformasiya Agentliyi › other-countries

Soldiers are quitting the Armed Forces at an alarming rate, despite a pay rise over the summer.

For the first time on record, there are now just two servicemen or women per thousand people in Britain.

Some 15,119 left the Armed Forces in the year to October. Of these, 7,778 were counted as “voluntary outflow”, those choosing to leave of their own accord.

*****†**********
December 22, 2024 15:04
UK soldiers quit in thousands despite Labour’s pay rise
UK soldiers quit in thousands despite Labour’s pay rise
Soldiers are quitting the British Armed Forces at an alarming rate, despite a pay rise over the summer, Report informs via The Telegraph.

For the first time on record, there are now just two servicemen or women per thousand people in Britain.

Some 15,119 left the Armed Forces in the year to October. Of these, 7,778 were counted as “voluntary outflow”, those choosing to leave of their own accord.

The forces recruited just over 12,000 personnel in the same period, resulting in a net shrinkage of the military.

Soldiers are leaving despite the Government’s attempt to stem the recruitment crisis with a 6 per cent pay rise.
Mrusi mtu m badi
 
Back
Top Bottom