Wananchi Chunya wamwambia RC Chalamila wagonjwa wanaotapika damu wako 22, RC aagiza wapelekwe hospitali ya Rufaa

Wananchi Chunya wamwambia RC Chalamila wagonjwa wanaotapika damu wako 22, RC aagiza wapelekwe hospitali ya Rufaa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Chalamila na mbunge wa Chunya wamezuru kijiji cha Ifumba wilayani Chunya kupata taarifa za ugonjwa usiojulikana.

Wananchi wamesema ugonjwa huo ni kweli upo na umeshaua watu zaidi ya 30 na kwa sasa kuna wagonjwa 22 ambao wamelazwa na wengine wanaugulia majumbani.

Ndipo mbunge wa Chunya akamuomba RC Chalamila aingilie kati swala hilo kwani wapiga kura wake wanateketea.

RC Chalamila akatoa agizo kwa mganga wa wilaya kuhakikisha wagonjwa wote 22 wanapelekwa hospitali ya Rufaa Mbeya kwa uchunguzi zaidi na matibabu.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
 
Mabibi na mabwana kuna habari kuwa kwa habari hii serikali imekwazika:



Nini makosa ya broadcaster kwenye hili?

Nini makosa ya watu kwenye sehemu ya tukio kuthibitisha mambo kama wanavyoyaona kama ilivyokuwa kwenye hili?

Ninawasilisha.
 
Sasa ule waraka unakuwaje? Kiukweli yule mama ni mkurupukaji mno na alimuoteshea kibarua majani daktari wa watu...kazi kujali kumfurahisha mwamfulani wkt watu wanateketea.... ITV sa itakuwaje..wataombwa radhi?
 
RC amekurupuka kusema wasafirishwe

Wanatakiwa kuwapa huduma apo apo
Kama ni mlipuko usisambae

Lakini tume ya waziri imeenda angalia MTUHA kitabu ambacho hakijazwagi OPD

Sasa KILA mtu apambane na hali yake
 
Sasa ule waraka unakuwaje? Kiukweli yule mama ni mkurupukaji mno na alimuoteshea kibarua majani daktari wa watu...kazi kujali kumfurahisha mwamfulani wkt watu wanateketea.... ITV sa itakuwaje..wataombwa radhi?
Sasa yule mama waziri hata hajafika kuwaona wahanga kaja na maamuzi juu kwa juu ya kumsimamisha kazi DMO..
Huyu mama hayuko sawa hata kidogo kazi kufanya sinema tu...
 
Back
Top Bottom